Huku Tandahimba hadi leo tar 21 Nov hakuna mkulima yeyote aliyelipwa pesa. Imedhihirika kwamba, kwa utaratibu huu wa ulipaji, wakulima wataendelea kusotea pesa zao hadi mwezi Mei 2019. Hebu fikiria, mkulima mmoja tu wa Tandahimba anavuna korosho hadi tani 35 ambayo thamani yake ni zaidi ya mil. 100 hali ambayo inaakisi kwamba kama serikali itatoa hizo mil. 500 kila awamu basi ni wakulima watano tu watakuwa wananufaika kati ya wakulima zaidi ya 50,000. Msimu uliopita chama cha TANECU (Taxdahimba na Newala) kiliuza korosho zenye thamani ya Tsh. Bil 600, halafu leo hii Magufuli anatoa bil. 2 kwa vyama vya msingi 35 then wapuuzi wanashangilia. Kwa mtazamo wangu ni kheri wangeachiwa wahindi kununua korosho. Serikali itaumiza wakulima kwa kuwasotesha kwa miezi mingi bila malipo. Korosho zinahitaji mtaji wa zaidi ya bil. 800 halafu Magufuli na benki ya TADB wanatoa bil 2 kwa awamu, hivi itachukua miezi mingapi kulipa wakulima wa korosho katika mikoa yote ilimayo korosho ambao thamani ya korosho zao inafikia zaidi ya bil. 800? Magufuli kachemka kwenye suala hili. Anaua wakulima. Hadi sasa ni vilio tu wakulima wakisotea malipo yao. Hataweza hii biashara.