Kutoka Tunduru: Wakulima wa Korosho wapokea zaidi ya Sh. Milioni 500

Kutoka Tunduru: Wakulima wa Korosho wapokea zaidi ya Sh. Milioni 500

Huku Tandahimba hadi leo tar 21 Nov hakuna mkulima yeyote aliyelipwa pesa. Imedhihirika kwamba, kwa utaratibu huu wa ulipaji, wakulima wataendelea kusotea pesa zao hadi mwezi Mei 2019. Hebu fikiria, mkulima mmoja tu wa Tandahimba anavuna korosho hadi tani 35 ambayo thamani yake ni zaidi ya mil. 100 hali ambayo inaakisi kwamba kama serikali itatoa hizo mil. 500 kila awamu basi ni wakulima watano tu watakuwa wananufaika kati ya wakulima zaidi ya 50,000. Msimu uliopita chama cha TANECU (Taxdahimba na Newala) kiliuza korosho zenye thamani ya Tsh. Bil 600, halafu leo hii Magufuli anatoa bil. 2 kwa vyama vya msingi 35 then wapuuzi wanashangilia. Kwa mtazamo wangu ni kheri wangeachiwa wahindi kununua korosho. Serikali itaumiza wakulima kwa kuwasotesha kwa miezi mingi bila malipo. Korosho zinahitaji mtaji wa zaidi ya bil. 800 halafu Magufuli na benki ya TADB wanatoa bil 2 kwa awamu, hivi itachukua miezi mingapi kulipa wakulima wa korosho katika mikoa yote ilimayo korosho ambao thamani ya korosho zao inafikia zaidi ya bil. 800? Magufuli kachemka kwenye suala hili. Anaua wakulima. Hadi sasa ni vilio tu wakulima wakisotea malipo yao. Hataweza hii biashara.
Hizo bilioni 800 ziliwafikia wakulima au wafanyabiashara wa kati?Sasa hivi bilioni zitawafikia walengwa na kuwaacha watu wa kati.
 
Mafisadi kama wewe ndiyo mnalalamika kafeli kwa kuwa amewabana kwenye ufisadi wenu!! Badilikeni acha ufisadi mkuu la sivyo hutaonekana uraiani.
Vp umeenda kubangua koro-show

Ova
 
Hizo bilioni 800 ziliwafikia wakulima au wafanyabiashara wa kati?Sasa hivi bilioni zitawafikia walengwa na kuwaacha watu wa kati.
Nenda tunduru hko ukajioneee Hali halisi usikalie kupata habari za kusikilizaaaa

Ova
 
Nenda tunduru hko ukajioneee Hali halisi usikalie kupata habari za kusikilizaaaa

Ova
ITV wapo Tunduru na wametuletea hali halisi ikiwemo madiwani wa upinzani walioshikwa katika kutapeli wakulima.
 
Sio kila muda upost kitu,tsh 500 million ni sawa na wamenunua tani 152 tu.Sasa sielewi unajaribu kuwaeleza nini watanzania juu ya hatma ya zaidi ya tani 200,000 za mavuno ya korosho.
FYI Korosho zitanunuliwa zote. Wewe Tuliza mshono bado haujapona vizuri.
 
million 500 kati ya billion 600...au billion 2 kati ya billion 600.. si mwaka utaisha hawajamaliza kununua?
gervase
Mwaka utaisha kwa mahesabu gani?
By the way mwaka umebaki wiki chache sana!
 
Kakurupuka huyo Lumumba akidhani mil500 ni pesa nyingi sana.

Hta hajui kuwa kuna tani ngapi za korosho
Wakurupukaji ni nyie...Hii ni taarifa ya Tunduru tu tena kwa siku chache tu bado maeneo mengine.
Serikali itanunua Tani zote tena kwa bei ya 3300
 
x = 500,000,000/3,300 = 151,515 = ~151 Tones

Nakukumbusha kuna Tani laki 221.

% ya walionunua = 151/221,000 = 0.068%

Zero Brains wa Lumumba wanapenda namba lakini hawajui hesabu.
Mkuu, hyo umeambiwa kwa Tunduru area.. Sio maeneo yote na wala sio tani zote 220,000 ziko huko Tunduru
 
Wakurupukaji ni nyie...Hii ni taarifa ya Tunduru tu tena kwa siku chache tu bado maeneo mengine.
Serikali itanunua Tani zote tena kwa bei ya 3300
Waambie hao.. Yaan kuna mijitu humu wao wamekalia kuharibu ilimradi nyoyo zao zifurahi..
Utadhan kama wana angalau kilo 1 ya korosho
 
Huna TV wewe?Hali ya kibiashara kwa wana Kangomba lazima iwe mbaya Serikali imeamua kuwalinda wakulima wake.
Hela walizopewa na Jeshi hawazitumii? Sioni mabadiliko hayo milioni 500 hali ile ile
 
Mkuu Inawezakana Unachokiongea Ni Sahihi, Lakini Tunaomba Utuambie Ni Chama Gani Cha Msingi Kilichopokea Hiyo Hela??
Mana Malipo Yote Ya Wakulima Hulipwa Kulingana Na Chama Cha Msingi Kilichopokea Korosho....!!
Wakulima wanalipwa direct kwenye account zao...huwa hamsikilizagi hotuba?
 
Wakulima mjini Tunduru wakiri kipokea fedha zao kwenye akaunti zao baada ya kuuza korosho kwa jeshi.
Kiasi cha zaidi ya sh. milioni 500 zimeshapokelewa na wakulima bila usumbufu wowote.

Aidha vibega na wafanyabiashara ya usafirishaji wa korosho wameendelea kufanya kazi zao na kupata ujira wao bila matatizo yoyote.

Hongera JPM kwa uamuzi sahihi.

Sasa tuhamie kwenye FOREX ...!!

Nchi na wananchi lazima tukae sawa!

source:ITV NEWS
hesabu huwaga hazidanganyi....

malipo haya ni 0.08% tu ya thamani ya korosho yote iliyochukuliwa na majeshi ya serekali. haya malipo yamefanyika ndani ya siku 10.

kwa ulipaji katika speed hii, itachukua siku 12,500 (au miaka 34) kuwalipa wakulima wote.

poleni wakulima. tukutane 2020.
 
hesabu huwaga hazidanganyi....

malipo haya ni 0.08% tu ya thamani ya korosho yote iliyochukuliwa na majeshi ya serekali. haya malipo yamefanyika ndani ya siku 10.

kwa ulipaji katika speed hii, itachukua siku 12,500 (au miaka 34) kuwalipa wakulima wote.

poleni wakulima. tukutane 2020.
Korosho yote iliyochukuliwa huko Tunduru ni kiasi gani?
 
Wakulima mjini Tunduru wakiri kipokea fedha zao kwenye akaunti zao baada ya kuuza korosho kwa jeshi.
Kiasi cha zaidi ya sh. milioni 500 zimeshapokelewa na wakulima bila usumbufu wowote.

Aidha vibega na wafanyabiashara ya usafirishaji wa korosho wameendelea kufanya kazi zao na kupata ujira wao bila matatizo yoyote.

Hongera JPM kwa uamuzi sahihi.

Sasa tuhamie kwenye FOREX ...!!

Nchi na wananchi lazima tukae sawa!

source:ITV NEWS
Wakulima wa kahawa wana kilio kikubwa kuliko wa korosho, msijifanye vipofu na msidanganyike na hatua hizi zilizojaa SIASA nyingi ndani yake.
 
Back
Top Bottom