JANUARY MAKAMBA NI MBUMBUMBU WA SUALA LA GESI NCHINI
Nimemsikiliza January Makamba akizungumzia suala la gesi na manufaa yake kwa nchi.
January anasema gesi iliyopo nchini haiwezi kuwanufaisha Watanzania hata baada ya miaka 10 ijayo akimaanisha kuwa bado mapato yake yatakuwa hayajaanza kupatikana! !
Nimeshangazwa na kauli hiyo inayodhihirisha u mbumbumbu wake katika suala zima la gesi nchini.
Makamba hajui kwamba hata sasa Watanzania wameshaanza kunufaika na gesi!
Mtoa nia huyu hajui kwamba pale Mikocheni kwenye nyumba za TPDC kuna Bomba la gesi inayotumika kupikia!
Makamba hajui kuwa hata Kiwanda cha SAO HILL kilichopo Dsm kinatumia gesi!
Kijana huyu anayeomba ridhaa ya Chama chake kuiongoza nchi, hajui kwamba kuna umeme unazalishwa kwa gesi hapa nchini hususan unaotumika mikoa ya Kusini!
Hiyo ni mifano michache tu inayodhihirisha kwamba Makamba hana ufahamu wa suala hili muhimu na hivyo ninapata wasiwasi kama anafaa kwa nafasi anayoiomba.
Namshauri Makamba asikilize Hotuba ya Profesa Muhongo wakati akitangaza nia hususan kwa suala la gesi.
Profesa Muhongo alieleza kwa ufasaha, kwa kina na takwimu jinsi gesi itakavyonufaisha Taifa na Watanzania kwa ujumla. Tujifunze kutoka kwa mtaalamu huyu mzalendo.
Nimemsikiliza January Makamba akizungumzia suala la gesi na manufaa yake kwa nchi.
January anasema gesi iliyopo nchini haiwezi kuwanufaisha Watanzania hata baada ya miaka 10 ijayo akimaanisha kuwa bado mapato yake yatakuwa hayajaanza kupatikana! !
Nimeshangazwa na kauli hiyo inayodhihirisha u mbumbumbu wake katika suala zima la gesi nchini.
Makamba hajui kwamba hata sasa Watanzania wameshaanza kunufaika na gesi!
Mtoa nia huyu hajui kwamba pale Mikocheni kwenye nyumba za TPDC kuna Bomba la gesi inayotumika kupikia!
Makamba hajui kuwa hata Kiwanda cha SAO HILL kilichopo Dsm kinatumia gesi!
Kijana huyu anayeomba ridhaa ya Chama chake kuiongoza nchi, hajui kwamba kuna umeme unazalishwa kwa gesi hapa nchini hususan unaotumika mikoa ya Kusini!
Hiyo ni mifano michache tu inayodhihirisha kwamba Makamba hana ufahamu wa suala hili muhimu na hivyo ninapata wasiwasi kama anafaa kwa nafasi anayoiomba.
Namshauri Makamba asikilize Hotuba ya Profesa Muhongo wakati akitangaza nia hususan kwa suala la gesi.
Profesa Muhongo alieleza kwa ufasaha, kwa kina na takwimu jinsi gesi itakavyonufaisha Taifa na Watanzania kwa ujumla. Tujifunze kutoka kwa mtaalamu huyu mzalendo.