Kutokana na changamoto za kibiashara mkoani Geita nafikiria kuhama mkoa, naomba mnishauri

Kutokana na changamoto za kibiashara mkoani Geita nafikiria kuhama mkoa, naomba mnishauri

Uza kila kitu ila frame muachie mtu kwa muda aweke hela zake alafu hamia Dar, weka hela zako sehemu salama kama Bank, hakikisha wewe ni mcha Mungu kama unataka kutafuta pesa kweli mambo ya madem weka kando kidogo kwa muda, fikia kwa ndugu usimwambie umefuata nini na asijue una hela, ndugu zako unawajua mwenyewe, ukiwa Dar hakikisha una tembelea sehemu kama kariakoo, ilala Boma pale fika saa 12 asubuhi,tandika n.k,kazunguke hayo masoko 3 kwanza na mengine utayajulia huko.

Angalia nini kinapendwa huko Mkoani kwenu kwa kuwa tayari una mtaji Utajua cha kufanya, achana na biashara ya hlela, anza kuuza nguo za watoto za mtumba utapata ilala na tandika, za special utazipata kariakoo, au mashuka au nguo za wanawake, usijifanye mjuaji Dar na usimuamini mtu, hata kama mlikutana kijijini ukifika Dar huyo anaweza kuwa mtu mwingine kabisa. So unaweza Kuanza kusafirisha au ukakomaa kuuza hapo hapo Dar wenyeji watakuelekeza, usikimbilie kupanga nyumba hadi uujue mji vizuri.

Ukitaka kukaa kwa ndugu kwa amani ondoka alfajiri urudi jioni, ukirudi ukiingia bafuni fua nguo zako huko huko, Acha bafu safi, ukijipendekeza kubaki nyumbani utatumwa hadi ukome, hadi watoto utaachiwa uangalie, ishi kwa mahesabu. Nadhani ukisoma hapa utapata chochote.
 
Uza kila kitu ila frame muachie mtu kwa muda aweke hela zake alafu hamia Dar, weka hela zako sehemu salama kama Bank, hakikisha wewe ni mcha Mungu kama unataka kutafuta pesa kweli mambo ya madem weka kando kidogo kwa muda, fikia kwa ndugu usimwambie umefuata nini na asijue una
Dah mkuu nashukuru Sana kwa comment hii yenye nguvu. Naomba nikufate DM nikunong'oneze kitu.
 
Uza kila kitu ila frame muachie mtu kwa muda aweke hela zake alafu hamia Dar, weka hela zako sehemu salama kama Bank, hakikisha wewe ni mcha Mungu kama unataka kutafuta pesa kweli mambo ya madem weka kando kidogo kwa muda, fikia kwa ndugu usimwambie umefuata nini na asijue una
Huyu kama hapo shilabela tu analizwa daily akija Dar watamuibia hadi nywele.
Bora aende simiyu huko
 
Nenda kahama hutojuta pia pesa ipo sana,mzungoko wa pesa upo vizuri hautegemei waajiliwa pekee.
 
Yaani alitoboa bodi akaingia usiku na akachukua pesa!!!!!
Uliendaje nyumbani ukaacha pesa dukani!!!! Kwenye eneo lenye vibaka wengi hivyo?
Anyway Hama huo mkoa kama umeshaamua kuhama....ila ujue wezi na matapeli wako kila mahali..Dar ndiyo usipime.
Na kwenye biashara hasara/changamoto kama hizo zipo sana tu.
 
Skushauri ukurupuke kwenda dar narudia the skushauri ukurupuke kuacha biashara yako au uuze vitu kisha uende dar haki ya Mungu utarudi geita huna hata mia ueenda hata nauli ukakosa usifanye mzaha kabisa fatilia watu wengi WA dar maisha Yao utagundua nasema nn swala la kuwa na hela au mtaji na swala la kufanikiwa ni vitu viwili tofauti maana nakuona Kama umetamani kwenda Dar aisee siongei haya kukutisha bali Dar napajua vema sana kwa gharama kaka tulia pambana hapohapo maana naona

Tyr ni kama umeweza kutoboa ukiwa hapo zaidi jifunze namna ya kuepuka madhira ya kuibiwa Dar maisha ya vjana wengi ni ya kuungaunga sana na maneno mengi kuliko uhalisia nmeishi Dar nmesoma Dar maisha ya vjana wa mikoani ni Bora sana kuliko maisha ya vijana wa dar ni rahisi sana kukuta vijana wa mikoani wana Miji Yao na familia zao trna wamejenga kabisa lakini KW vijana wa dar wengi hata Kodi tu shida msosi shida kama kuna anayebisha ye abishe tu pambana bro pambana hapohapo usidanganywe na vijana wa dar aisee wale maneno mengi sana siongezi chochote nakutakia Kila la kheri Mzee Kama utaenda dsm
 
Huyu kama hapo shilabela tu analizwa daily akija dar watamuibia hadi nywele.
Bora aende simiyu huko
Kwakua wewe sio Mimi ndo maana umenena haya ila kwa taarifa tu dar nimeish na kulingana na mazingira kwa ofisi yangu ni RAHISI kuibiwa kulingana na Aina ya biashara Ninayo ifanya. #usikalili
]
 
Yaani alitoboa bodi akaingia usiku na akachukua pesa!!!!!
Uliendaje nyumbani ukaacha pesa dukani!!!! Kwenye eneo lenye vibaka wengi hivyo?
Anyway Hama huo mkoa kama umeshaamua kuhama....ila ujue wezi na matapeli wako kila mahali..Dar ndiyo usipime.
Na kwenye biashara hasara/changamoto kama hizo zipo sana tu.
Kwa kipindi hicho ndo nilikua nimeyaanza maisha ya utafutaji hivyo nilipo kua naishi hapakua na geti huko ndo kulikua ni nyumbani kwa vibaka, kwa usalama ilikua ni Bora niache mzigo ofisini kuliko kwenda nao geto.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kifupi huna tattizo lingine zaidi ya wizi. Kontroo wizi na komaa hapohapo,kuza mtaji ndio uanze hayo mawazo ya kuhama. Unakoenda sio wizi wakuviziana ni unaporwa na silaha. Jikuze kimtaji kwanza.
 
Kifupi huna tattizo lingine zaidi ya wizi. Kontroo wizi na komaa hapohapo,kuza mtaji ndio uanze hayo mawazo ya kuhama. Unakoenda sio wizi wakuviziana ni unaporwa na silaha. Jikuze kimtaji kwanza.
Shukrani mkuu; ila kwa sasaiv pia biashara imekua ngumu kiwango Cha pesa nikicho kua nakiingiza zaman na sasaiv ni tofauti, huu mji kwa wakati huu umekua Mgumu sana.
 
Hamia Dodoma hutojuta, moro utalia pale simu zinauzwa bei rahisi kuliko dar si unajua wazee wa madili
Niko kanda ya ziwa ila natamani kufanya biashara Dodoma. Maeneo gani mazuri ya kufanyia biashara hapo? Hasa hizo za huduma za kifedha kwa mtaji wa 6M
 
Binafsi nakupa pole kwa changamoto za kibiashara unazopitia hasa kuibiwa!
Biashara hasa ya miamala ya fedha Kama hiyo unaifanya kuibiwa ndio changamoto kuu!

Ushauri wangu:
1. Kokote utakapoenda wezi wapo na wanabadilika mbinu Kila wakati.
2.Endelea kubaki hapo hapo lkn biashara yako iwe inahamishika
3. usiache fedha ndani ya kibanda, fedha zote Kama zinabakia uwe unahama nazo na asbh unazijaza ktk float zako.
4. Ongeza Umakini ktk biashara hasa kutokosea kutuma, hapa uwe unampa simu mteja aingize namba zake mwenyewe akikosea inakula kwake! Lkn pia msomee na jina ili athibitishe ili uendelee na muamala au usitishe.

Geita mm sio mwenyeji Sana, Ila huko ni kwa wakwe zangu, nilitembelea pia hapo nyankumbu na maeneo mengine Kama katoro! Ile movement ya katoro kwa biashara yako ni nzuri Sana, ikukupendeza basi hamia hapo, Ila kibanda usikiuze, kikodishe kwa mtu mwingine uendelee kupiga Senti za Kodi.

Huo ndio mtazamo wangu!
 
Binafsi nakupa pole kwa changamoto za kibiashara unazopitia hasa kuibiwa!
Biashara hasa ya miamala ya fedha Kama hiyo unaifanya kuibiwa ndio changamoto kuu!

Ushauri wangu:
1. Kokote utakapoenda wezi wapo na wanabadilika mbinu Kila wakati.
2.Endelea kubaki hapo hapo lkn biashara yako iwe inahamishika
3. usiache fedha ndani ya kibanda, fedha zote Kama zinabakia uwe unahama nazo na asbh unazijaza ktk float zako.
4. Ongeza Umakini ktk biashara hasa kutokosea kutuma, hapa uwe unampa simu mteja aingize namba zake mwenyewe akikosea inakula kwake! Lkn pia msomee na jina ili athibitishe ili uendelee na muamala au usitishe.

Geita mm sio mwenyeji Sana, Ila huko ni kwa wakwe zangu, nilitembelea pia hapo nyankumbu na maeneo mengine Kama katoro! Ile movement ya katoro kwa biashara yako ni nzuri Sana, ikukupendeza basi hamia hapo, Ila kibanda usikiuze, kikodishe kwa mtu mwingine uendelee kupiga Senti za Kodi.

Huo ndio mtazamo wangu!
Mkuu nashukuru Sana kwa ushauri;

Kumpa mteja simu sio njia nzuri kwakua ni RAHISI Sana mtu kujaza namba yake na kusave jina M-PESA Kisha akakutumia sms ya kubumba, kuhusu kuhama na hela ndicho ninacho kifanya mpaka Sasa lakini pia bado kuna risik kwakua wenye nia mbaya wakijua una ondoka na hela wanaweza kukuvamia njiani, hapa jiran kuna mmma walimuua wakachukua milion 3 maana alikua anaondoka nazo pesa zote.

Kifupi mpesa ni biashara ya hatari Sana kwasasa nawaza kubadairi Aina ya biashara na mazingira mpaka mda huu navyo andika hapa nimekuja Katoro kuchek site.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nikusihi tu tena na tena hakuna mafanikio ya kirahisi rahisi nimeona mtu anakushauri uzunguke dar baada ya kuuza biashara uliyo nayo, heshimu kinacho kuweka mjini, umesema mauzo yameshuka sana na hali imekuwa ngumu fikiria namna ya kuuteka mtaa kivingine wewe ndio uwe mtawala wa hapo kuliko kuhama mazingira, unapo hama mazingira kuna kushuka pia maana ukienda unakuwa mgeni wenyeji wapo tayari washa teka mtaa.

Mimi dodoma wanakokuambia uende napo ni pazuri lakini mambo bado hayajakaa sawa kiivo kupata fremu au site lazima utapeliwe tu kwa pale mjini wenye nyumba wameongeza makodi yao kizembe eti laki 4 fremu ya kawaida.

Kama unahama tumia akili kubwa ila usidharau biashara yako ukafungue nyingine harakaharaka.
Wizi na utapeli upo kila mahali
 
Mkuu nashukuru Sana kwa ushauri;

Kumpa mteja simu sio njia nzuri kwakua ni RAHISI Sana mtu kujaza namba yake na kusave jina M-PESA Kisha akakutumia sms ya kubumba, kuhusu kuhama na hela ndicho ninacho kifanya mpaka Sasa lakini pia bado kuna risik kwakua wenye nia mbaya wakijua una ondoka na hela wanaweza kukuvamia njiani, hapa jiran kuna mmma walimuua wakachukua milion 3 maana alikua anaondoka nazo pesa zote.

Kifupi mpesa ni biashara ya hatari Sana kwasasa nawaza kubadairi Aina ya biashara na mazingira mpaka mda huu navyo andika hapa nimekuja Katoro kuchek site.

Sent using Jamii Forums mobile app
We mkuu ukipata site hapo katoro nicheck DM tufanye kitu mi taweka pia mtaji tushauriane kwanza
 
Mkuu nikusihi tu tena na tena hakuna mafanikio ya kirahisi rahisi nimeona mtu anakushauri uzunguke dar baada ya kuuza biashara uliyo nayo, heshimu kinacho kuweka mjini, umesema mauzo yameshuka sana na hali imekuwa ngumu fikiria namna ya kuuteka mtaa kivingine wewe ndio uwe mtawala wa hapo kuliko kuhama mazingira, unapo hama mazingira kuna kushuka pia maana ukienda unakuwa mgeni wenyeji wapo tayari washa teka mtaa.

Mimi dodoma wanakokuambia uende napo ni pazuri lakini mambo bado hayajakaa sawa kiivo kupata fremu au site lazima utapeliwe tu kwa pale mjini wenye nyumba wameongeza makodi yao kizembe eti laki 4 fremu ya kawaida.

Kama unahama tumia akili kubwa ila usidharau biashara yako ukafungue nyingine harakaharaka.
Wizi na utapeli upo kila mahali
Mkuu Asante kwa ushauri, nimekuelewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom