Kutokana na mwenendo wa Spika wa bunge , Je, kuna haja ya Raia kuendelea kuiheshimu Katiba ya Tanzania ?

Kutokana na mwenendo wa Spika wa bunge , Je, kuna haja ya Raia kuendelea kuiheshimu Katiba ya Tanzania ?

Yaani kwa kitendo hiki cha Spika Ndugai ni dhahiri ameamua kuisigina Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977

Kilichotakiwa ni huyo Spika kuburuzwa mahakamani kwenda kujibu mashitaka yake.......

Hata hivyo ninachohofu ingawa hilo ni kosa straight forward, lakini kwa kadri nchi hii inavoendeshwa hivi sasa, usije shangaa mhimili huo wa mahakama ukaamua "kujivua" wajibu wake kwa kisingizio kuwa wanaogopa kuingilia utendaji wa mhimili huo wa Bunge!
Hilo ni dhahiri kabisa
 
Mambo ni shangala bagala...kila.mtu kwa sasa kawa boss, boss naye kakimbia lindo...patam
 
Mimi nilishaachana zamani kuheshimu katiba mkuu. Saivi naangalia fursa tu za kupiga hela ikibidi hata rushwa natoa au hata wizara naibiya bila ya wasi wasi tunaongeza tu zero. Potelea mbali mtu unajifanya kutii sheria wakati jamaa wanavunja mchana kweupe.
 
Wakuu naomba kukiri kwamba mimi si mtaalam wa sheria za Tanzania , hivyo uzi wangu waweza kuwa na mapungufu kadhaa , lakini ni dhahiri kwamba kwenye nchi hii sheria za uchaguzi zinawataka wagombea kudhaminiwa na chama cha siasa , kwa maana kwamba ili uweze kukubaliwa na Tume ya uchaguzi kuwa mgombea wa ubunge , udiwani ama Urais unapaswa kuwa mwanachama wa chama cha siasa kilichosajiliwa na Msajili wa vyama vya siasa .

Na kwamba ikiwa utavuliwa uanachama na chama hicho ama wewe binafsi kujivua uanachama basi bila shaka utakuwa umepoteza Ubunge wako na kutotambuliwa kama mbunge .

Cecil Mwambe tunataarifiwa kwamba amerejea bungeni ambako yeye mwenyewe aliondoka baada ya kujivua uanachama wa chama kilichomdhamini baada ya kumuokota barabarani 2015 na kumpa nafasi ya kugombea ubunge wa Ndada baada ya kutupwa na ccm , na amerejea kwa hisani ya Spika wa bunge hilo Mtukufu Ndugai , kwa kadri ya ufahamu wangu huku ni sawa na kudharau na kusigina kabisa katiba ya nchi , yawezekana mimi labda sielewi , naomba wanasheria mnisaidie , na ikiwa kama spika wa bunge anaamua kunyea katiba ya nchi mnadhani kuna haja ya raia wa kawaida kuiheshimu ?

Nakala : Tundu Lissu
Jiwe analiendesha atakavyo jinga sn lile gogo
 
Anayelinda katiba alipaswa awe mahakamani
 
Bado kuna watu mnajiuliza kuhusu "bunge la ndugai"?Ninachojua mimi tangu 2016 ni kuwa hatuna Bunge...Chombo cha kuisimamia serikali kama ndicho kinaitwa Bunge,basi chombo hicho hakipo nchini tangu Rais aliyepita aondoke madarakani..

Kuna chombo kingine kipya,ambacho hakijatajwa hata kwenye Katiba, ambacho kinabariki kila kitu cha serikali na kupewa maelekezo na serikali..ndo mnakiita Bunge?Kama maana ya Bunge bado haijabadilika basi tuelewe tu kuwa hakuna Bunge hapa nchini...Kuna kitu kipya kinaitwa "bunge la ndugai"...Kinafanyia shughuli zake za kubariki na kuelekezwa na serikali pale mahali ambapo Bunge lilikuwepo kabla halijafa..Nadhani labda ni sababu inayowachanganya watu kudhania ndiyo Bunge lenyewe!!
 
Bado kuna watu mnajiuliza kuhusu "bunge la ndugai"?Ninachojua mimi tangu 2016 ni kuwa hatuna Bunge...Chombo cha kuisimamia serikali kama ndicho kinaitwa Bunge,basi chombo hicho hakipo nchini tangu Rais aliyepita aondoke madarakani..

Kuna chombo kingine kipya,ambacho hakijatajwa hata kwenye Katiba, ambacho kinabariki kila kitu cha serikali na kupewa maelekezo na serikali..ndo mnakiita Bunge?Kama maana ya Bunge bado haijabadilika basi tuelewe tu kuwa hakuna Bunge hapa nchini...Kuna kitu kipya kinaitwa "bunge la ndugai"...Kinafanyia shughuli zake za kubariki na kuelekezwa na serikali pale mahali ambapo Bunge lilikuwepo kabla halijafa..Nadhani labda ni sababu inayowachanganya watu kudhania ndiyo Bunge lenyewe!!
Aibu kubwa sana !
 

Attachments

  • Isaya 10_12 Basi, itakuwa, Bwana atakapokuwa ameitimiza kazi yake yote juu ya m ( 266 X 480 ).mp4
    652.6 KB
Rais wa Kwanza na baba wataifa la kenya mzee Jomo Kenyatta aliwai kusema kua Nyerere anatawala maiti
Naona Hiyo ni kweli kabisa
Kwasababu Zifuatazo .......

1. Katiba inavunjwa na rais wao kazi yao ni kusema hapa kazi

2. Spika wa bunge anavunja katiba na Sheria za nchi watu bado wanasema muache awanyooshe

3. Wakuu wa mikoa wanavunja katiba na Sheria za nchi wao bado kazi yao ni kusifia

4. Wakuu wa wilaya wanavunja katiba na Sheria za nchi wao kazi yao ni kusifia tu

5. Police wanavunja katiba na Sheria za nchi wao kazi yao ni kusifia

Hapo tutakosa kweli kuwa maiti maana tukisifia Sana mwisho wake huzaa utumwa wa fikra na unakuwa tegemezi wa ujinga kwa kila kitu
 
Rais wa Kwanza na baba wataifa la kenya mzee Jomo Kenyatta aliwai kusema kua Nyerere anatawala maiti
Naona Hiyo ni kweli kabisa
Kwasababu Zifuatazo .......

1. Katiba inavunjwa na rais wao kazi yao ni kusema hapa kazi

2. Spika wa bunge anavunja katiba na Sheria za nchi watu bado wanasema muache awanyooshe

3. Wakuu wa mikoa wanavunja katiba na Sheria za nchi wao bado kazi yao ni kusifia

4. Wakuu wa wilaya wanavunja katiba na Sheria za nchi wao kazi yao ni kusifia tu

5. Police wanavunja katiba na Sheria za nchi wao kazi yao ni kusifia

Hapo tutakosa kweli kuwa maiti maana tukisifia Sana mwisho wake huzaa utumwa wa fikra na unakuwa tegemezi wa ujinga kwa kila kitu
Nakulilia Tanzania .
 
Back
Top Bottom