Kutokuwepo kwa Mabalozi wa US, UK, Sweden, Norway, Denmark, EU, Japan na South Korea leo Dodoma, kuna nini kinaendelea jikoni?

Kuna kitu nahisi kinakuja, na si cha kawaida kwa kweli. Sie tulioibiwa Uchaguzi nafikiri huu ni muda sahihi kuchukua popcorn na kuangalia huu mchezo unavyozidi kuwa mtamu

Kuchukua popcorn na kuangalia tu kama movie?!?! Watu wengine wa mabara mengine ndio wafanye jambo kwenye dhulma uliyofanyiwa wewe (huku wewe ukiwa unaenjoy ‘show’)??!! SMH [emoji2296][emoji15]
 
Wameshindwa kazi waliotumwa na serikali zao ya kuhakikisha janja janja ya wazungu inaota mizizi.
 
Tanzania ni tajiri, biashara ya kuwa watumwa kwenye nchi yetu iliisha tulipopata uhuru na JPM ameamua kuiondoa nchi hii kwenye utumwa mambo leo. Sasa kama kuna makuwadi wa hizo nchi walifikiria sisi ni shamba la bibi imekula kwao. Hapa kazi tu!

 
Kuchukua popcorn na kuangalia tu kama movie?!?! Watu wengine wa mabara mengine ndio wafanye jambo kwenye dhulma uliyofanyiwa wewe (huku wewe ukiwa unaenjoy ‘show’)??!! SMH [emoji2296][emoji15]
Kuna muda inafika lazima tufurahie external support. Kama sie wanatuua na kutubambikia makesi, acha wapambane na wababe wa dunia sie tufurahie
 

Furaha atakua awe nayo asilani kwa kuwa kapora ushindi

Angekua na furaha sana kama angeshinda kihalali hata kama ni ushindi mwembamba
 
Bora tupate shida ili akili zitukae vizuri
 
Tangu lini tajiri akawa ombaomba??? Nyie ni malofa tu
 
Tanzania ni nchi huru, nchi ulizozitaja zina hiyari ya kuhudhuria au kutokuhudhuria.
 
Tanzania ni nchi huru, nchi ulizozitaja zina hiyari ya kuhudhuria au kutokuhudhuria.
Sawasawa. Sasa ndo tutaona kama ni nchi huru na inaweza ku survive bila hizo nchi kutoa pesa zake au la!!
 
Balozi mwenye akili timamu hawezi kuja kwenye uchafuzi wa demokrasia
 
Ila Saudi Arabia anaenda.
Kwani Saudi arabia wamechafua demokrasia?Wao katiba yao imepiga marufuku mambo ya vyama vya siasa,Tanzania katiba inaruhusu siasa za vyama vingi ila wapinzani wakifanya siasa wanakiona cha mtema kuni.Huo ndiyo tunaita ni uchafuzi wa demokrasia Tanzania.
 
Ha ha ha ha ha, haya bhana. Lakini tatizo wapinzani hawapo serious.
Ni haki ya kikatiba ya mpinzani kufanya siasa hata kama hayupo serious.Kwani katiba ya Tanzania inasema wapinzani walio serious pekee ndiyo wanaruhusiwa tu kufanya siasa na ambao hawapo serious wapigwe,wauawe,wateswe,wafungwe,etc kama tunavyoshuhudia sasa hivi?
 
Ya kwao yamewashinda wanaangaikaje na ya kwetu? Waambie wamarekani wakaondoe ubaguzi wa rangi uliokithiri kwako na makandokando mengi yanayofanywa na wazungu kwa watu weusi ambao ni wamarekani.
 
Hakuna kitu Kama hicho hata wakati tunaamua kuanza ujenzi wa bwawa la kufumua umeme la Mwl Nyerere mlisema hivyo hivyo na hakuna lolote.Waambieni hao mabwenyenye Tanzania ni nchi huru inajiamulia Mambo yake yenyewe.Rais Trump analalamika kuibiwa kura na kuhujumiwa kwenye uchaguzi katika mazingira hayo analalamika kwa kusema uchaguzi haukuwa huru na wa haki. Waambie wamarekani ya kwao yamewashinda kamwe hawataweza ya watanzania Mungu tuliyenae ni Mkuu kuliko wanavyofikiri ndiyo maana hata ugonjwa wa Corona kwetu hakuna
 
Balozi mwenye akili timamu hawezi kuja kwenye uchafuzi wa demokrasia
Niambie Ni Chama gani Cha upinzani Kuna demokrasia? Niambie viongozi wa vyama vya upinzani na wagombea Ubunge wa majimbo na vitimaalumu kwenye hivyo vyama vya upinzani wanapatikana kwa namna gani?Kama si kuteuana tu kwa kujuana,Rushwa na uhuni. Sasa Kama umeshindwa kujua demokrasia iliyopo kwenye vyama vya upinzani huwezi kujitambua wewe bilashaka wewe ni GUNZI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…