ministrant
JF-Expert Member
- Jan 17, 2014
- 754
- 1,478
Habari za jumapili wana jukwaa. Kwa wale walio wakristu nawatakia maandalizi mema kwa kuanza juma kuu ikiwa leo ni jumapili ya matawi na jumapili ya mwisho ya kwaresma kuelekea sikukuu ya Pasaka.
Napenda kuchukua nafasi hii kuomba ushari na maoni yenu aidha unaotokana na taaluma zenu kama vile udaktari ha kadhalika uzoefu wenu hasa kwa wale ambao tayari ni wazazi.
Nimepokea taarifa za kunishangaza kidogo kutoka kwa mtu wangu wa karibu ya kuwa mke wake huwa anatokwa na damu ukeni wakati wa tendo la ndoa au pindi anapokuwa anafanya kazi ngumu kama vile kuchota maji.
Walijaribu kufika kituo cha afya na baada ya vipimo daktari alibaini kuwa ana UTI kali hivyo aliandikiwa sindano 5 ambazo alichomwa kwenye mishipa pamoja na vidonge ambavyo alitumia kwa muda wa siku tatu.
Cha kushangaza ni kuwa hali bado haijakoma na mara ya mwisho aliposhiriki tendo la ndoa na mke wake hali ya kutoka damu ukeni ilijirudia.
Kitu kinachompa wasiwasi zaidi hali ya mtoto kucheza tumboni inazidi kupungua tofauti na hapo awali. Umri wa ujauzito ni miezi 3.
Ushauri wenu tafadhali.
Napenda kuchukua nafasi hii kuomba ushari na maoni yenu aidha unaotokana na taaluma zenu kama vile udaktari ha kadhalika uzoefu wenu hasa kwa wale ambao tayari ni wazazi.
Nimepokea taarifa za kunishangaza kidogo kutoka kwa mtu wangu wa karibu ya kuwa mke wake huwa anatokwa na damu ukeni wakati wa tendo la ndoa au pindi anapokuwa anafanya kazi ngumu kama vile kuchota maji.
Walijaribu kufika kituo cha afya na baada ya vipimo daktari alibaini kuwa ana UTI kali hivyo aliandikiwa sindano 5 ambazo alichomwa kwenye mishipa pamoja na vidonge ambavyo alitumia kwa muda wa siku tatu.
Cha kushangaza ni kuwa hali bado haijakoma na mara ya mwisho aliposhiriki tendo la ndoa na mke wake hali ya kutoka damu ukeni ilijirudia.
Kitu kinachompa wasiwasi zaidi hali ya mtoto kucheza tumboni inazidi kupungua tofauti na hapo awali. Umri wa ujauzito ni miezi 3.
Ushauri wenu tafadhali.