Baadhi ya walimu waliositahili kupanda madaraja ya kiutumishi 2023 hawajapandishwa vyeo vyao kwa sababu mbalimbali. Baadhi ya sababu ni walioko masomoni, walio likizo bila malipo na walio mashtaka katika kamati za kinidhamu katika wilaya mbalimbali kwa makosa mabalimbali.
Kutompandisha mwalimu daraja la cheo kwa sababu ana kesi ya kiutumishi ni kukiuka katiba ya nchi ibara ya 13 ibara ndogo ya 6(b) inayopiga marufuku mtu aliyeshitakiwa kutendewa kama mtu mwenye kosa mpaka itakapothibitika kuwa ana hatia ya kutenda kosa. Kama akishinda kesi, au akapewa hukumu ndogo tofauti na kutompandisha cheo.
Mtumishi hataweza kuwa tena na daraja sawa na rika ya watumishi alioanza nao kazi kama Raisi Samia anavyotaka watumishi wa rika moja ya kiutumishi kuwa sawa mishahara. Ukiukwaji huu wa katiba ni kanuni mbovu za TSC zinatotungwa na watumishi wake wasio na uelewa wowote wa kisheria. Kwa sababu tume hii inashughulikia zaidi haki za kisheria na kiutumishi za walimu ifike wakati watumishi hawa wa tume wawe wanasheria na maofisa wenye weredi wa maliasili watu.
Waachane na hawa walimu wasio na uelewa wowote wa kisheria. Kanuni zao zinaweza kuwaingiza kwenye mgogoro wa kisheria pindi watumishi wanaotendewa uonevu huu wakiamua kukatwa rufaa.
Kutompandisha mwalimu daraja la cheo kwa sababu ana kesi ya kiutumishi ni kukiuka katiba ya nchi ibara ya 13 ibara ndogo ya 6(b) inayopiga marufuku mtu aliyeshitakiwa kutendewa kama mtu mwenye kosa mpaka itakapothibitika kuwa ana hatia ya kutenda kosa. Kama akishinda kesi, au akapewa hukumu ndogo tofauti na kutompandisha cheo.
Mtumishi hataweza kuwa tena na daraja sawa na rika ya watumishi alioanza nao kazi kama Raisi Samia anavyotaka watumishi wa rika moja ya kiutumishi kuwa sawa mishahara. Ukiukwaji huu wa katiba ni kanuni mbovu za TSC zinatotungwa na watumishi wake wasio na uelewa wowote wa kisheria. Kwa sababu tume hii inashughulikia zaidi haki za kisheria na kiutumishi za walimu ifike wakati watumishi hawa wa tume wawe wanasheria na maofisa wenye weredi wa maliasili watu.
Waachane na hawa walimu wasio na uelewa wowote wa kisheria. Kanuni zao zinaweza kuwaingiza kwenye mgogoro wa kisheria pindi watumishi wanaotendewa uonevu huu wakiamua kukatwa rufaa.