kutopata haja kubwa kwa muda mrefu

kutopata haja kubwa kwa muda mrefu

habari wanajamvi.nina tatizo la kukosa haja kubwa mara kwa mara.pengine naweza kupitisha hata siku tano hadi sita na kasababisha tumbo kuvimba.nimekwenda hospitali kutibiwa na nimepewa dawa mara nyingi lakini imeshindikana.nimeshauriwa kunywa maji mengi,matunda na mboga za majani lakini imeshindikana na yenyewe.tatizo hili nimedumu nalo kwa kipindi cha miaka mitatu sasa.naomba ushauri wenu pengine nipate ufumbuzi wa tatizo hili.

nahisi we leo ndo ulikuwa kwenye daladala unatuchafulia hewa
 
Sijui upo ktk kutumia dawa gani mkuu?inawezekana labda kuna baadhi ya medicines unazozitumia ndio cause ya hilo tatizo,mfano dawa za kusaidia homoglobin huwa zina tatizo la kumfunga mtu choo,maji mengi na mboga za majani na matunda kwa wingi husaidia pia vyakula vyenye vibers ni vizuri kama vile karanga zozote zile za kukaangwa au kuchemshwa pia zitakusaidia sana,pia kama wewe ni mtu wa kula ugali basi tumia unga wa dona(whole wheat flour)usile mikate myeupe ni hatari kwako na afya yako.Kuna kitu ningekushauri uwe unatumia kila baada ya meal hasa ya jioni,sijui mwenzangu upo wapi,kama upo north America tafuta kitu inaitwa meta mucial ni powder fulani hiyo itaweza kufungua njia yako na hilo tatizo ka uta maintain hivyo vyakula vyenye fiber kwa wingi utakuwa fixed mara moja.Kama upo hizi nchi zilizoendelea labda ningekushauri ujaribu kufanya test ya damu yako ili wapate full blood picture yako wajue ni chemical gani inayosababisha hali ka hiyo kutokea mwilini mwako.Pole sana na hilo tatizo ndugu yangu hata mimi mwenzio tayari nimeisha sumbuliwa sana na hilo tatizo lakini baadaye waligunduwa kilichokuwa behind it,sasa niko sawa namshukuru m/mungu.M/Mpamba.
 
Biology haina maombi,nenda hospital kaonane na specialists watagundua tatizo lako usiwasikilize hawa walokole na confusions zao hapa.M/Mpamba.
 
habari wanajamvi.nina tatizo la kukosa haja kubwa mara kwa mara.pengine naweza kupitisha hata siku tano hadi sita na kasababisha tumbo kuvimba.nimekwenda hospitali kutibiwa na nimepewa dawa mara nyingi lakini imeshindikana.nimeshauriwa kunywa maji mengi,matunda na mboga za majani lakini imeshindikana na yenyewe.tatizo hili nimedumu nalo kwa kipindi cha miaka mitatu sasa.naomba ushauri wenu pengine nipate ufumbuzi wa tatizo hili.

Pole sana mimi nilikuwa natatizo kama lako kwa muda mrefu ila nilipata ushauri wa kutumia juice ya tunda hili kila niki maliza kula imenisaidia sana pia punguza vyakula vya mafuta ImageUploadedByJamiiForums1411436092.465142.jpg nadhani kama upo tz utapata kwenye masoko ya wahindi pale uhindini linaitwa beetroot kwa kiswahili sijui
 
habari wanajamvi.nina tatizo la kukosa haja kubwa mara kwa mara.pengine naweza kupitisha hata siku tano hadi sita na kasababisha tumbo kuvimba.nimekwenda hospitali kutibiwa na nimepewa dawa mara nyingi lakini imeshindikana.nimeshauriwa kunywa maji mengi,matunda na mboga za majani lakini imeshindikana na yenyewe.tatizo hili nimedumu nalo kwa kipindi cha miaka mitatu sasa.naomba ushauri wenu pengine nipate ufumbuzi wa tatizo hili.

MARADHI YA KUTOPATA CHOO (CONSTIPATION):

Haya ni maradhi ambayo mgonjwa huwa

hapati choo kwa wepesi. Haja kubwa inaweza kutoka baada ya siku moja au mbili au zaidi na ikitoka huwa ni kigumu na hutoka kwa shida na wakati mwingine huwa kama


choo kama cha mbuzi. Wagonjwa wengine hupata maumivu wakati wa kwenda haja kubwa.
Mtu mwenye afya nzuri hupata haja kubwa kwa kiwango cha chini mara moja kwa siku. Na choo huwa laini na hutoka bila matatizo.

SABABU ZA MARADHI HUSIKA

(1) Upungufu wa vitamini mwilini hasa vitamin B.

(2) Maradhi ndani ya utumbo mpana.

(3) Kula vitu vigumu na vikavu kama vile vyakula vya ngano.

(4) Upungufu wa ulaji matunda na mboga.

(5) Kutokunywa maji ya kutosha.

(6) Upungufu wa fibre kwenye chakula zinazopatikana kwenye maganda ya mahindi. (7) Ukosefu wa kufanya mazoezi ya viungo.


UKOSEFU WA kutopata choo kiurahisi: Soma tiba rahisi

UKOSEFU wa choo ni tatizo sugu miongoni mwa watu wengi. Bila kujua kuwa ni tatizo ambalo linahitaji tiba ya haraka, watu wengi hupuuzia na kuona siyo tatizo kubwa na ni hali ya kawaida. Ukosefu wa choo wa muda mrefu, huwa ndiyo chanzo cha magonjwa mengine hatari.

Mtu anapokosa choo kikubwa kwa siku kadhaa, uchafu hujikusanya tumboni na unapokosa sehemu ya kutokea hukimbilia kwenye damu na kuingia kwenye mfumo mzima wa damu. Uchafu huo unapoingia kwenye mfumo wa damu huwa sumu na chanzo cha maradhi mengine ambayo hujitokeza baadae na kuanza kumuathiri mtu, bila kujua chanzo chake.

Kwa kawaida mtu unapaswa kupata choo cha uhakika japo mara moja kwa siku, kutegemeana na mlo wake wa kila siku, unapokosa choo kwa siku nzima ili hali una kula milo yote kwa siku, elewa una tatizo katika mfumo wako wa kusaga chakula hivyo unapaswa kuchukua hatua haraka.

MTU MWENYE TATIZO HILI ANA DALILI GANI?
Mtu mwenye tatizo la ukosefu wa choo huwa na dalili kadhaa, ikiwemo kutumia nguvu na muda mwingi wakati wa kujisadia haja kubwa. Pili ulimi wake huwa na utandu mweupe na hutoa harufu mbaya mdomoni. Mtu huyu pia hukosa hamu ya chakula na wakati wote tumbo huwa limejaa.

NINI HUSABABISHA TATIZO?

Tatizo la ukosefu wa choo husababishwa zaidi na ulaji mbaya wa vyakula, kuacha kula matunda na mboga na staili mbaya ya maisha ikiwa ni pamoja na kutokunywa maji ya kutosha kwa siku.

NINI KIFANYIKE?
Ili kuondoa tatizo kabla halijawa sugu, fanya moja miongoni mwa haya yafuatayo: Kunywa maji ya uvuguvugu asubuhi mapema, kisha tembea tembea, baada ya muda utasikia haja ya kwenda chooni. Ili usifanye haraka na upate muda wa kutosha kujiandaa kwenda kazini, amka mapema zaidi. Kula kiasi cha kutosha cha salad ya mboga mboga na juisi ya matunda halisi asubuhi kabla ya kula chochote.

Kila siku kabla ya kwenda kulala, kunywa maji ya uvugu yaliyochanganywa na kijiko kimoja cha asali. Kunywa maji ya uvugu

yaliyochanganywa na limau asubuhi na mapema kabla hujala kitu chochote. Kunywa
‘castor Oil' Mafuta ya Nyonyo kijiko 1 muda mfupi kabla ya kwenda kulala. Ili

kujiepusha kabisa na tatizo la ukosefu wa choo, jenga mazoea ya kunywa maji mengi, kula mboga na matunda kwa wingi kila siku na

kuacha kabisa ulaji wa vyakula vilivyoondolewa virutubisho kama vile mikate myeupe, ugali wa unga mweupe, keki vyakula vyenye sukari nyingi na vyakula vingine vitamu. Ukiwa na Swali au tatizo lolote nitafute mimi kwa kubonyeza hapa.
Mawasiliano
 

Attachments

  • feeling_of_constipation.jpg
    feeling_of_constipation.jpg
    26.8 KB · Views: 131
Pole sana. Zingatia ushauri wa wengi hapo hasa kubadilisha ulaji pia ukiweza waone madaktari. lakini ukitaka msaada zaidi wa kiafya zaidi ntafute kwa simu 0689 417 472
 
Pole ndugu nakushauri pamoja na vyakula vya whole diet naomba ufanye mazoezi ya viungo dakika wala ishirini kwa siku ikiwa kama kuruka kamba dakika tatu, kuruka ruka ukitanua miguu na mikono juu kwa dakika saba, pushup dakika 3 na mazoezi mengine unayoyaweza hili kwanza litaongeza uwezao wako wa kusaga chakula, pili tafuta mayai ya kware (quail eggs) unaweza kugoogle benefit zake katika eneo hilo la usagaji wa chakula pata matatu siku ya kwanza na ya pili siku ya tatu manne na baada ya hapo matano matano kwa siku 22 naamini utaona tofauti kubwa sana
 
habari wanajamvi.nina tatizo la kukosa haja kubwa mara kwa mara.pengine naweza kupitisha hata siku tano hadi sita na kasababisha tumbo kuvimba.nimekwenda hospitali kutibiwa na nimepewa dawa mara nyingi lakini imeshindikana.nimeshauriwa kunywa maji mengi,matunda na mboga za majani lakini imeshindikana na yenyewe.tatizo hili nimedumu nalo kwa kipindi cha miaka mitatu sasa.naomba ushauri wenu pengine nipate ufumbuzi wa tatizo hili.

nina dawa inaitwa constirelax ni nzuri sana kwa tatizo lako. nitafute nikusaidie 0759077008
 
nenda ukafanye colonoscopy. kama alivyoandika mzizimkavu pengine kuna ugonjwa kwenye utumbo mpana.
 
Tafuta juice ya Prune (100% prunes) ni fibers za kutosha.
Pia kula oats sana badala ta cgai na mkate.
 
Back
Top Bottom