Kuuaga umasikini........

Ukitembea utaona lakini utajengaje hoja ? anecdotal evidence haina mashiko!

Easy! Umaskini au ufukara Tanzania uko rampant kiasi cha kutohitaji hata anecdotes. Umaskini ni hali halisi ya kila siku ya walio wengi (overwhelming majority). It's real and not phantasm. Sasa kwa kitu au vitu ambavyo ni hali halisi ya kila siku wala si vigumu hivyo kuvijengea hoja na kuhitaji minamba na mitakwimu ili kuipa nguvu hoja yako. Hamna mtu yoyote mwenye akili timamu atakeyeweza kujenga hoja ya kwamba eti "bongo ni tambarare" au "bongo Nyu Yoki". Hakuna. Wanaosema hivyo hawajui walisemalo.
 
Umesikia budget ya chuo ndugu? ni sawa na seating allowance ya wabunge kwa kikao cha siku moja je wao wanawezaje kufanya kitu kizuri bila resources?..."kitu kizuri gharama" walimu wanahaingaika kutafuta outdoor incomes, (muda mchache kuandaa nondo), wanafunzi wanahangaika kutafuta madawati kabla ya kuingia darasani akipata dawati hakuna nafasi ya kukaa, cycles goes on..wanfunzi wananunua mitihani of course kwa kushirikiana na wazazi wao ambao nao wana vyeti feki...na wa hela na nafasi...maskini wanamshawishi mwalimu ambaye yuko kwenye deep shit...cycles goes on.."bottom line peleka nje system CCM tuanze upya tunaweza kuchelewa lakini ni afadhali kuanza upya na kuweka misingi ya maana before it is too late" I mean 2010 .
 
nimeweka hizo takwimu ili kufunua macho tuone kama kweli ni tambarare kama inavyofikiriwa...
Hizi takwimu ni za hali generally.... Vijijini wala usiseme!

ukipata takwimu za watanzania wanaomiliki redio na wanao mudu kuvaa kandambili ndo utachoka zaidi.
 
Naomba umalizie datas kwa kuonyesha ni aslimia ngapi ya watanzania hawajui kwa nini wawe kwenye daftari la wapiga kura na hawajui kwa nini wapige kura.

Msisahau kutafiti kwa nini tupo tunaotaka sana kuwa kwenye daftari hilo ila hatumo!
 
Ukitembea utaona lakini utajengaje hoja ? anecdotal evidence haina mashiko!

Umasikini wa Tanzania ni mzito kiasi kwamba hata watu tunaowaita matajiri tanzania nao ni "masikini"

Tajiri na Masikini Tanzania hawana Uhakika wa umeme,maji safi na salama.

Tofauti ni kuwa tajiri atatafuta "work-around" ili avipate vitu vya msingi.wakati masikini atamuachia mungu.

umasikini wa Tanzania tulitakiwa tusisubiri UN agencies,IMF na Benki ya Dunia kutukumbusha,tulitakiwa tuwakumbushe wao kuwa sisi ni masikini.(same way tunawaambia marafiki zetu-sina pesa na hawaamini)

Umasikini wetu Tanzania ulitakiwa uwasumbue vichwa viongozi wetu na kuwakosesha usingizi.ila hawa jamaa wameumbwa tofauti.kwani wanalaa fofofo.

Tanzania ni nchi yetu,tunaipenda sana lakini ni masikini sana,hatuhitaji kupayuka kuonesha hilo,ndio hali halisi ya nchi yetu.

maliasili zilizotakiwa zitusaidie ndizo zinatuangamiza.mara mia tungekuwa jangwa lisilo na kitu,labda hawa viongozi waroho wangekosa cha kugombea,tungepata viongozi wenye nia ya kuendeleza nchi tu.

sasa hivi kila mtu ninayemuona anagombea uongozi namuona ni "opportunist".ama amechoka kufanya kazi kujiingizia kipato sasa anataka kupumzika bungeni na kulipwa au ni mfanyabiashara anayetaka kuutumia mgongo wa uongozi kujinufaisha.

Ukiishi nchi za watu kwa muda ukirudi TZ.
utaliona hilo.kwa sababu zisizofahamika,watanzania wameridhika na walivyo sasa.natamani watanzania milioni 40 wangepata nafasi 1 tu ya kutembelea EU na kurudi.things would never be the same!

ni kazi kumtambua mwenye virusi sio umasikini wa watanzania
THAT IS SOO OBVIOUS.
 

R U kidding me?!Unless niwe sijakupata point yako ndugu yangu.Kuridhika kwa watanzania kama nilivyogusia huko mwanzo katika posts zangu ndilo hasa tatizo.
Kutembelea nchi za watu na kurudi hakutaleta mabadiliko kama unavyofikiria.Hao viongozi wetu kila leo wako safari hukohuko kwa wenzetu.Ni mabadiliko gani ya ajabu sana wameleta? Ukiacha viongozi, sasa hivi watanzania wengi tu wanasafiri sana kwa shughuli mbalimbali - biashara, mafunzo, kikazi n.k.Wengi wakirudi wanashindwa hata kujiletea mabadiliko kidogo katika ngazi za kaya zao sembuse kuleta katika ngazi ya nchi!
Kama ni exposure - nadhani watanzania haishi tena kwenye closed society ambapo tumejifungia hatujui nini kinaendelea nchi za wenzetu - thanks to media and different forms of communication.Kila kitu sasa kinafanyika na kuonekana kila mahali in real time.Juzi tu wamezindua THIS IS IT YA MJ DUNIA NZIMA na hata TZ watu wamejionea kama wenzao huko kwenye ustaarabu.Ninachotaka kusema ni kuwa the problem isnt so much one of lack of exposure bali kuna laxity at all levels.Gone are the days ambapo you had to wait years kuelewa trends zilizoko kwenye ulimwengu wa kwanza.
 

Thanx so much Veracity. we now need velocity,( with a light touch) to go ahead. Nisingependa kuongezea mengi hiyo bold na red inasema yote ila hebu tuangalie katika watu hao 18 million kwa age group halafu nenda mtaani uulizie kama wao wamejiandikisha kwenye daftari au la, jibu utakalopata hakika utashangaa.

Watu hawafuatilii matokeo, kweli kama unavyosema, lakini usisahau wahenga walisema:

Every election is a sort of advance auction sale of stolen goods. - H. L. Mencken

Those who cast the votes decide nothing. Those who
count the votes decide everything.
- Josef Stalin


Kwa hiyo usishangae kuona ile dhana ya kufuatilia baada ya kupiga kura inakuwa negated kabisa matokeo mara nyingi ni tofauti na ukweli na watu wanaishia kuzira.


 

Sasa hizi trend za maji safi na salama,umeme,huduma za afya mbona zinachukua light years kutufikia?!

sioni kwamba kuona movie ya "this is it" ya MJ kunamfungua mtu macho kwa njia yoyote ile.

Mfano wangu wa watanzania Millioni 40 ni kuonesha kuwa asilimia kubwa ya watanzania hawana "the right exposure".

Nilikuwa vijiji vya jirani na Kamtimbo,mpanda miezi kadhaa iliyopita na nadiriki kusema kuwa Tanzanaia ya "exposure" iko hapa JF tu.kule kwa wananchi wa kawaida swala zima la Umeme,maji safi na salama,"interenet",huduma bora za afya ni mtego kwao.cha kushangaza wameridhika mno na hali hiyo.kwao Kikwete anaongoza nchi vizuri mno.hawalalamiki kama sie.

Hao viongozi na wakuu wa idara tunawaona wakija huku ughaibuni,wao ni kufikiria per diem,na kushangaa tu,wachache sana wanarudi kuhimiza maendeleo.

Watanzania ninaoongelea kuwa hawana exposure ni wale wanaojaza daftari la wapiga kura huku wakiwa hawajui sifa za mtu wanayempigia kura.

inasikitisha pia kuona kuwa asilimia chini ya 10 ya wananchi ndio wana--enjoy huo umeme na maendeleo' ya Tanzania.

Watanzania waliopata nafasi ya kwenda nchi za watuu kama wewe matunda yake tunayaona hapa JF.kila siku mnakemea maovu na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike.sio kwamba hao viongozi hawajui nini kifanyike ila <<their "love" to greener life is blinding them>>.

Hata wale wananchi wa "mpanda et al" mnawaona wakifika dar,wengi wao hulowea dar,kwani maisha huyaona bora tofauti na walivyoona awali.

Sisi watanzania wengi sasa hivi ni kama vyura ndani ya kisima,tunaiona dunia kupitia upana wa kisima,laiti tungelitoka nje ya kisima' hawa watu wasingetuchezea na mgao wa umeme miaka nenda rudi.
 
R U kidding me?!Unless niwe sijakupata point yako ndugu yangu.Kuridhika kwa watanzania kama nilivyogusia huko mwanzo katika posts zangu ndilo hasa tatizo.

Sidhani na Siamini kwamba kuna "silver Bullet" ya kumaliza umasikini wa watanzania.

Umasikini wetu tumeupata kupitia mlolongo mrefu na hautaisha kwa njia/suluhisho fupi.

Sijakataa na ulichosema,Ila nilichagua kutofautiana na kauli yako kuwa umasikini wa watanzania unahitaji kujenga hoja kuulezea.upo wazi mno.

Kuridhika kwa watanzania kunaweza kuwa moja ya tatizo lakini sio tatizo pekee.

nimezaliwa Tanzania na nilikwa mridhikaji wa hali ya Tanzania,yale maisha ya kwenye "movie" nilikuwa nayaona kama ya kwenye muvi tu.miaka nenda rudi kwenye nchi za wenzetu yameniondoka uridhikaji wangu.naamini watanzania tuna uwezo,lakini hatulitambui hilo."limits" zetu ziko karibu mno.

maisha ya kwenye movie ndio yametufanya tuamini kumiliki gari,kuwa na laptop,kuwa na Runinga ndio maisha bora.

Hata Bill Gates aliwahi Tamka Hadharani kuwa "64K RAM is all that a person would ever need".guess what am typing this thread with a 32GB of RAM computer.Go figure
 
Elimu pia inachangia huu umasikini wetu.Hivi takwimu zikoje katika hili la elimu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…