Kuuawa kwa kiongozi wa Hamas 'haisaidii' mazungumzo ya kusitisha mapigano, asema Biden

Kuuawa kwa kiongozi wa Hamas 'haisaidii' mazungumzo ya kusitisha mapigano, asema Biden

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
565dba30-507a-11ef-8f0f-0577398c3339.jpg

Kuuawa kwa kiongozi wa Hamas 'haisaidii' mazungumzo ya kusitisha mapigano, asema Biden​

Rais wa Marekani Joe Biden amesema kuwa mauaji ya kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh "hayasaidii" mazungumzo kuhusu uwezekano wa kusitisha mapigano huko Gaza.

g
Maelezo ya picha,Marekani imesema kuwa haikuhusika katika mauaji ya kiongozi wa kisiasa wa Hamas
Rais wa Marekani Joe Biden amesema kuwa mauaji ya kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh "hayasaidii" mazungumzo kuhusu uwezekano wa kusitisha mapigano huko Gaza.

Haniyeh aliuawa katika ziara yake katika mji mkuu wa Iran, Tehran siku ya Jumatano. Iran na washirika wake wameilaumu Israel, ingawa Israel bado haijatoa maoni yoyote kuhusu kifo chake.

Haniyeh alikuwa afisa mkuu wa Hamas na alihusika sana katika mazungumzo ya kusitisha mapigano na kuwaachilia mateka kutoka kituo chake nchini Qatar.

Bwana Biden alisema "ana hofu sana" kuhusu kuongezeka kwa mvutano katika Mashariki ya Kati. "Tuna msingi wa kusitisha mapigano. Yeye [Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu] anapaswa kuendelea nao [Hamas] wanapaswa kuendelea nao sasa."

Israel na Hamas hivi majuzi walianza tena mazungumzo ya muda, yasiyo ya moja kwa moja ili kujaribu kufikia usitishaji wa vita huko Gaza, ingawa kumekuwa na maelezo yanayokinzana kuhusu mafanikio ya mazungumzo hayo.

Mwishoni mwa mwezi Mei, Bw Biden alielezea kile alichosema kuwa ni masharti ya pendekezo la Israeli la kusitisha mapigano. Huu umekuwa msingi wa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Hamas na Israel tangu wakati huo, huku Qatar, Misri na Marekani zikiwa wapatanishi.

Mapema wiki hii, Israel na Hamas zilishutumu kila mmoja kwa kukwamisha maendeleo ya mazungumzo.
Hamas ilisema Israel imeanzisha masharti mapya, huku ofisi ya Bw Netanyahu ikisema Hamas imetaka kufanyika kwa mabadiliko 29 kwenye pendekezo hilo.

Chanzo: BBC
 
Hamas wameshatoa msimamo wao frame wanayongoja ni ya tar 2 July aliyotoa biden vinginevyo hawatashiriki sasa shida iko wapi kama sio unafiki wa Marekani wenyewe wakati kila kitu kipo mezani
 
Mpaka wakubali kuishi na binadamu wengine kwa amani dunia hii, wataendelea kufa huku wakilia lia kuwa wanaonewa, kuanzia Somalia, Sudan, Syria kote huko vita vyao vya kijinga.
 
Back
Top Bottom