Kuunga kwa Soko la Kariakoo, kuna la kujifunza?

Kuunga kwa Soko la Kariakoo, kuna la kujifunza?

Kashishi yetu

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2014
Posts
3,509
Reaction score
3,741
Majanga mengi yamekuwa yakijitokeza ya moto.Sasa hivi kuna janga la moto Soko la KARIAKOO, Shule moja huko Morogoro.

Je kutokana na majanga haya na mengine ambayo yalishawahi kutokea huko nyuma na chanzo chake kusemekana ni hitilafu ya umeme, JE KUNA CHA KUJIFUNZA KUHUSU MAJANGA HAYA YA MOTO?NINI KIFANYIKE KUZUIA AU KUPUNGUZA MAJANGA HAYA YA MOTO?

Binafsi nimejifunza yafuatayo:-

Mosi,Kuwepo na ulazima wa majengo kukaguliwa mifumo mizima ya wayaringi kila baada ya kipindi fulani jengo lote kukaguliwa na wataalamu kutoka TANESCO.Hili nliilipata siku TANESCO walipokuja mtaani kwetu baada ya shoti ya umeme kuunguza vifaa na watu kutaka kulipwa fidia.Hivyo TANESCO walihoji lini jengo lako limewahi kukaguliwa na TANESCO kuona ubora wa nyaya?

Pili,Kuzingatia maelekezo ya TANESCO.Siku walipokuja kwetu. TANESCO waliuliza maswali mengi sana,Je Wakati unafanyiwa wayaringi nyumba yako, Je vifaa ulivyoandika utakavyokuwa unavitumia ndivyo hivyo hivyo au uliongeza vingine tofauti na mwanzo? Kama uliongeza vingine je ulienda TANESCO kuomba kibali ili waje wakurekebishie mfumo wako wa wayaring?

Tatu,Kuwasha pale tu unapohitaji kutumia kifaa cha umeme na kuzima mara tu baada ya kumaliza matumizi ya kifaa hicho.Wengi hapa hujisahau.Huacha feni ikiwaka na matokeo yake umeme ukikatika na ukirudi unarudi kwa kasi ya ajabu.

Nne,Kwa upande pia wa mashuleni huko.Umakini unahitajika kwani baadhi ya wanafunzi huenda mashuleni wakiwa na simu.Sehemu ya kuchajia hupanda juu ya Dali na kuchubua nyaya za umeme, wanajua jinsi ya kuunganisha hadi kufanikisha kuchaji simu zao.

Tano, Usalama wa vyombo tunavyovitumia.Visiwe vifaa chakavu sana.Vifaa chakavu husababisha shoti ya umeme.

Sita, Kwenye biashara yako hakikisha kila unapouza pesa peleka benki.Usilaze dukani pesa zako hata siku moja.

Saba, Nimejifunza kuwa na rekodi za biashara yangu sehemu mbili.Yaani uhifadhi wa kumbukumbu za biashara yangu ufanyike sehemu mbili.Dukani niache nakala na nyumbani kwangu ziwepo nakala ili ikitokea janga la moto kama hili wadeni wangu wote au taarifa muhimu au nyaraka muhimu za biashara yangu zisipotee.

Nane,Nimejifunza kuwa nijenge mahusiano mazuri na wenzangu ili ikitokea janga la moto nipate misaada lukuki kutoka kwao.

Tisa,Nimejifunza kuepukana kabisa na mafundi vishoka wa umeme.Niache ubahiri wa kukataa kuwaita Mafundi wa TANESCO kukwepa gharama na kuwatumia vishoka ambao hawana utaalamu wowote zaidi ya kutafuta pesa ya kula na familia zao huku mimi wakiniachia msalaba mzito wa kuunguliwa vitu vyangu vya thamani kubwa kabisa.

Hayo ndiyo niliyojifunza kwa upande wangu.

.Mengi nilijifunza siku TANESCO walipokuja mtaani kwetu walitupatia Elimu.

Je wewe mwenzangu umejifunza nini cha kuongezea au kupunguza katika hayo niliyojifunza?

UPDATE
SOKO LA KARUME LIMEUNGUA TENA MOTO WALOZINGATIA USHAURI WANGU HUU UTAKUWA UMEWASAIDIA WALOUPUUZA IMEKULA KWAO.

SERIKALI IFANYE UCHUNGUZI KWANINI MAJANGA YA MOTO YATOKEE USIKU TU? AU KUNA WAFANYABIASHARA WANAACHA VITU ON KWENYE VIZIMBA VYAO?
 
Suala la bima ya moto hujaliongelea kabisa,halafu hili tukio la mabweni ya shule kuungua linajirudia sana,kuna harufu ya hujuma inanukia,vyombo vya dola vichukue hatua thabiti za kiintenlijensia kuhakikisha matukio kama haya yanakomeshwa,manaake kuna watu hua wanasema eti Tanzania inashika nafasi ya tatu kwa upelelezi mahiri duniani ,basi kwa umahiri huo ni tegemeo langu kwamba wanaohusika na hujuma hizi wakamatwe kama kuku within short time to come.
 
Siyo mbaya ukiwa vifaa vya kuzimia moto nyumbani na eneo la biashara yako, ambavyo vipo ndani ya uwezo wako kama vile fire extinguisher n.k ili inapotokea tatizo la moto Kama upo unaweza lidhibiti mapema.
 
Conspiracy theories. Viongozi waliotumbuliwa hapo sokoni wahojiwe
 
Mioto mingi ni njama japo kweli ipo ya ajali.
 
Hujaongelea suala la bima.
Masoko makubwa kama hayo iwe lazima kuwa na bima kwa kila mfanyabiashara ili kulinda mitaji yao.
 
Sisi tunaishi ilimradi siku ziende tu, kuna haja ya kuacha kuishi kwa mazoea na kuacha kupuuza vitu vinavyoweza kuleta madhara makubwa mbeleni.
 
Suala la bima ya moto hujaliongelea kabisa,halafu hili tukio la mabweni ya shule kuungua linajirudia sana,kuna harufu ya hujuma inanukia,vyombo vya dola vichukue hatua thabiti za kiintenlijensia kuhakikisha matukio kama haya yanakomeshwa,manaake kuna watu hua wanasema eti Tanzania inashika nafasi ya tatu kwa upelelezi mahiri duniani ,basi kwa umahiri huo ni tegemeo langu kwamba wanaohusika na hujuma hizi wakamatwe kama kuku within short time to come.
😁😁 Mkuu tue serious kidogo basi Mossad, cia, mi6 kwahiyo hapo kuna mmoja tumemkalisha??
Haya matukio ya moto kile kipindi yalikua mengi mno hakuna tulichojuzwa zaidi ya upepelezi kuendelea, labda wai wana taarifa na wanatificha, hapo hatujui.

Ila hiyo ya upepelez ni chai mkuu kaulize vizuri.
 
😁😁 Mkuu tue serious kidogo basi Mossad, cia, mi6 kwahiyo hapo kuna mmoja tumemkalisha??
Haya matukio ya moto kile kipindi yalikua mengi mno hakuna tulichojuzwa zaidi ya upepelezi kuendelea, labda wai wana taarifa na wanatificha, hapo hatujui.

Ila hiyo ya upepelez ni chai mkuu kaulize vizuri.
Hapo umenena vyema manaake hii habari ya vijiweni imekuwa inaaminiwa na wengi kumbe ni upuuzi mtupu Huwezi kuwazidi mosad cia mi6 svr-rf ya huko Russia na zinginezo.
 
Ishu ya bima imekaa kimtego zaidi, kuna shirika fulani walikuja job kutuomba kujiunga na bima za majengo/ nyumba. Sasa nyumba ikipata janga la moto lazima moto huo uwe umesababishwa na short ya umeme na ithibitishwe na Tanesco. Sasa Tanesco waje kuchunguza ripoti itoke waseme wao ndo chanzo, hii ni ngumu kwa vigezo vyao.
 
Inawezekana kabisa kua chanzo au sababu ikawa pia ni vifaa fake vya umeme vinavyotumika.
 
Hapo umenena vyema manaake hii habari ya vijiweni imekuwa inaaminiwa na wengi kumbe ni upuuzi mtupu Huwezi kuwazidi mosad cia mi6 svr-rf ya huko Russia na zinginezo.
Hizo story nakumbuka tulikua tunadanganyana sana primary huko 😂😂
Mambo kibao yanatokea na hakuna majibu yoyote toka kwa hao wapelelezi.
 
Inawezekana kabisa kua chanzo au sababu ikawa pia ni vifaa fake vya umeme vinavyotumika.
Huwa nikiangalia wiring na jinsi watu wanavyounga unga nyaya pale kariakoo huwa nasema lazima kuna siku tukio litatokea.

Watu wamepasiana umeme hovyo. Hadi nyaya nyembamba za spika au solar zinatumika kufungia holder za bulb.
images (85).jpeg
images (87).jpeg
 
Janga halina hodi ila tahadhari na umakini ni muhimu...
 
Back
Top Bottom