Kuunguruma kwa kongamano la Wanataaluma Dar: Moto wayaka!

Kuunguruma kwa kongamano la Wanataaluma Dar: Moto wayaka!

Mh, hii ngumu kweli kwetu watanzania, ni nani tanzania anaweza kuandaa kitu kikapokewa na positive mazee?

Yaani inavunja moyo kweli

Tatizo kubwa kama msemaji mmoja alivyo tangulia kusema ni tatizo la wanansiasa wetu, Tanzania inaongozwa kisiasa zaidi ya kitaalamu au kitaluma.
Tanzania matatizo tuliyo nayo ni hapo wanasiasa uchwala watakapo dhibitiwa lazima tujiulize ni kwa nini wataalamu wetu wanakimbilia kwenye siasa(sihasa- wazungu wanasema politricks na si politics).
Hizi politricks na sihasa ndo zimetufikisha tulipo.
Kama mh. Komba anaweza kuimba uzuri wachama mlolile na akawa maarufu kuliko kina Dr.Shaba hujaona kuwa pana tatizo hapo?
wanasiasa haohao kama mh.Makamba akipata kijana au mtaalamu aliye bobea jambo la kwanza atapigwa vita mpaka akimbie nchi.
Kwani wataalamu wetu wengi walioko nje walikimbizwa na nini si ni huu ubabaishaji wa wanasiasa?
Hivyo basi tutaunda kongamano za kila aina kama hatutapata busara za kuchimgua mzizi wa matatizo hao tutakalia kupunguza matawi tu na mwisho hatutafika mahali popote.
Wanataaluma wetu sasa tusikimbilie jambo lolote kabla hatuja lekebisha mambo ya msingi ambayo yametufanya watanzania tuwe wageni katika nchi yetu.
Lazima nchi irudishwe kwa wananchi kwanza maana sasa hivi iko mikononi mwa wanasiasa kadha ambao wanafadhiliwa na watu kadha kwa manufaa yao na BIASHARA ZAO.
 
Mzee mwanakijiji unaonaje sasa na wewe kama mwanataaluma mzalendo uwe wazi sasa hakuna haja ya kuficha nyuma ya majina mengine uwe wazi ujulikane wewe ni nani ili kujenga utamaduni wa kuwajibika miongoni mwetu na kuongea kwa uwazi kama jamii zilizoendelea

Ni kweli lakini nadhani wakati haujawa mwafaka kila jambo lina wakati wake na ninaamini mkuu mkjj hilo analijua wakati ukiwadia hatahitaji kuobwa kufanya hivyo mkuu.
 
Jmushi1:

Watanzania na miradi yenu ya kumuinua mtu kifkra (mentality), mnapoteza muda na resources tu. Na ujamaa kilikuwa sio chombo cha kunyanyua fikra za mtanzania.

Kukiwa na incentives za watu kujifunza au kutafuta ufumbuzi wa matatizo yao, they will do a lot of things on their own.

Zakumi;Posting yangu uliyoijibu ambayo niliielekeza kwenye kuijibu post ya MKJJ,nilisema hivi....
jmushi1 said:
Mwalimu aliliona tatizo hilo mapema sana,na ndio maana na yeye akaja na siasa za ujamaa na kujitegemea,ile mentality ya kwamba "Hatuwezi" "Sisi ndivyo tulivyo" nk ndivyo vilivyomfanya atake kupambana na ile mentality ya kuomba omba na imani kwamba we can't do nothing,na kwasababu siasa zake zile zilikufa,kukawa na loophole,na sasa siasa zimekuwa kama michezo ya kipuuzi kwasababu as a nation hatuna vision wala mission
Na katika pita pita yangu leo hapa jeo nimekutana na uchambuzi huu kutoka kwa profesa Issa Shivji kuhusiana na siasa za mwalimu...

Sera ya kujitegemea badala ya utegemezi kwa maana ya kutegemea misaada na mikopo kutoka nchi za nje. Umuhimu wa kujitegemea ulikita kwenye mambo mawili: moja, kwamba huwezi ukawa na uhuru wa kujiamulia mambo yako kama unamtegemea mwingine; na, pili, kwa vyovyote vile, hakuna mjomba huko nje ambaye atakusaidia kukuletea maendeleo

Hitimisho langu liko pale pale,kama mentality ni ya kuomba omba bado na kumsubiria uncle sam etc hatutaweza kuprogress,ni mapambano ya kifikra,ni makovu yanayoambatana na jamii nyingi za kiafrika,ndiyo reality,tatizo kubwa la waafrika wengi ni wasahaulifu mapema,je kwenye sera yetu ya kuomba omba incentives za kutafuta ufumbuzi zitakuwa ni zipi hizo?
 
Bwana Sanctus Msimbe,

Hongera kwa kuanadaa kongamano na natumaini umevuna ulichokipanda. Je ule Waraka wa Mchungaji ulishaufanyia kazi kama ulivyoniomba mwaka mmoja uliopita?

La pili, je kama TPN na washihriki wa kongamano hili, mlilijibuje swali hili la kwanza ?

Je ni nini vipaumbele vya kitaifa kwa mujibu wa TPN au kutokana na maazimio ya kongamano? Je Vipaumbele hivi vimebainika au kubuniwa kutokana na mtazamo gani na wa nani? Je vipaumbele hivi vinamnufaisha nani na vipi?

Kama nikiamua kuweka na kubaini vipaumbele viwili vitatu, kwa ajili ya gumzo hapa kama vile Ubunifu, Juhudi, Ufanisi na Uadilifu, nyinyi kama Wataalamu mliokuwa mnachangua vipaumbele vya kitaifa, mko wapi katika kutambua vipaumbele vya Mchungaji, kuishi katika mtazamo wa Mvhungaji kwa kuwa watekelezaji bora wa vipaumbele vya Mchungaji katika ushiriki wa Vipaumbele vya Taifa vya kujenga Uchumi Imara?

Je katika vipaumbele hivi, ni Uchumi pekee ambao ni mlengwa na mnufaika? je mengine ambayo si ya kiuchumi, TPN na washiriki wanamuachia nani na yatasawazishwa vipi kama hayapo au kama yana kasoro?

Mchungaji;

Niliyoyashuhudia nashindwa kuyaelezea. Kukiwa na namna nina DVD zilizorekord proceeds zote. It was very exciting.

Kunapokutana Wanataaluma wenye uchungu na nchi yao, kuna zaidi ya utakayodhania. Kama watu wametoka ughaibuni kuja kuhudhria Kongamano hili, huku wamejilipia nauli, malazi, na gharama za hoteli nk. kisha partcipation fees, mchana hawajali hata muda wa kula kwa kuwa wana issues muhimu za kujadili, muda wa kumaliza kikao umefika, wanataka waendelee hadi usiku na hapo hawalipwi per diem, hakika si kitu cha kawaida.

Na ni nani aliyesema Wazalendo Nchi hii waekwisha au hakuna uzalendo?

Napenda kukuhakikishia kuwa, yote yanayoweza kutekelezeka chini ya Mtandao wa wanataaluma yatafanyiwa kazi.

Taarifa zaidi, kong'oli hapa:
https://www.jamiiforums.com/habari-...luma-waishio-ndani-na-nje-ya-nchi-2009-a.html
 
Mchungaji;

Niliyoyashuhudia nashindwa kuyaelezea. Kukiwa na namna nina DVD zilizorekord proceeds zote. It was very exciting.

Kunapokutana Wanataaluma wenye uchungu na nchi yao, kuna zaidi ya utakayodhania. Kama watu wametoka ughaibuni kuja kuhudhria Kongamano hili, huku wamejilipia nauli, malazi, na gharama za hoteli nk. kisha partcipation fees, mchana hawajali hata muda wa kula kwa kuwa wana issues muhimu za kujadili, muda wa kumaliza kikao umefika, wanataka waendelee hadi usiku na hapo hawalipwi per diem, hakika si kitu cha kawaida.

Na ni nani aliyesema Wazalendo Nchi hii waekwisha au hakuna uzalendo?

Napenda kukuhakikishia kuwa, yote yanayoweza kutekelezeka chini ya Mtandao wa wanataaluma yatafanyiwa kazi.

Taarifa zaidi, kong'oli hapa:
https://www.jamiiforums.com/habari-...luma-waishio-ndani-na-nje-ya-nchi-2009-a.html

Lakini hujajibu swali (maswali) langu....!
 
Back
Top Bottom