Kuuza au kutouza nafaka nje: Serikali ichague kuumiza wengi au wachache

Kuuza au kutouza nafaka nje: Serikali ichague kuumiza wengi au wachache

Mchokoo

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2015
Posts
1,181
Reaction score
1,579
Suala la kuuza au kutouza nafaka nje.

Yaani niseme kwamba; kulingana na kiwango kidogo cha chakula tulichonacho, sikubaliani na wale wanaotaka tuuze chakula nje. Ndugu zangu msifikiri jambo hili ni rahisi kama mnavyoliona, mkaanza kuilaumu serikali kwa zuio lililopo.

Mtu yeyote mwenye akili timamu; kwanza anajitoshereza mwenyewe, kisha kilichozidi ndicho hukiuza kwa mwenzake.

Utakuwa ni upunguani wa kifkra, kama taifa, tukiuza chakula kwa shilingi, kisha baada ya miezi michache tukatumia akiba ya madola kuagiza chakula hichohicho nje ya nchi.

Pili, ni kweli wakulima wetu wataumia kidogo, nasema kidogo kwa sababu hata wao chakula hiki kitawasaidia baadaye, maana wanauzaga mpaka akiba kwa tamaa ya bei ya angalau, ndiposa baadaye wanateseka sana kwa njaa.

Nasema bei ya angalau kwa sababu kwa kweli mnufaikaji mkubwa wa hili ni mlanguzi.

Tatu, Ukiangali kwa jicho la tatu; sehemu kubwa ya nchi yetu mavuno hayakwenda vizuri. Yaani watnzania wengi hawana chakula.

Utaona ni kipindi cha mavuno lakini bado maeneo mengi bei za chakula hazijarudi mahala pake.

Hivyo ilikuwa vema kama taifa tuamue kuwaumiza wengi au wachache. Sawasawa na dereva wa basi atakayeamua kumkwepa mtu mmoja akaangusha basi zima, au kumgonga huyo na kusalimisha 65.

Mwisho, kulinga na ukame mkubwa unaoendelea kuzikumba nchi nyingi za ukanda huu wa afrika mashariki na kati, siyo vema kutegemea manchi haya makubwa yauziwe chakula na wananchi wanaojilimia kienyeji tu.

Ni kwa nini usifanyike uwekezaji mkubwa kulingana na fursa iliyopo, utakaokidhi hitaji la soko lililopo?

Kwa sababu haiwezekani chakula cha nchi moja kikategemewa na ma…nchi kibao huko ni kutengeneza njaa kwa wahusika wenyewe!

Ungekuwa wewe ni mfanya maamuzi ungefanyaje?
 
Tukuulize wewe umelima mwaka huu? Kama hujalima nyamaza. Nyie ndo mliozoea kuwaliza wakulima.
Bila shaka.wewe ni mlanguzi uliyeumizwa sana na uamuzi huo.
 
Vipi waliojiari kwenye mnyororo wa kilimo unasemaje kwa wao kukosa ajira.
Je tuendelee kuongeza idadi ya machinga na bodaboda mijini ambao hawakuzi uchumi wa nchi zaidi ya kuwa ni madalali wa kukuza uchumi wa China.
Mahindi yakiuzwa gunia laki na 20 badala ya elf 25 huoni tunapata pesa za kigeni,watu wakiwa na pesa wataagiza nje chakula
 
Mkulima,
Mkulima,
Mkulima,
Mkulima,
Mkulima,
Mkulima ni mpiga kura mwaminifu na mtiifu ingawa hana likizo.

Kuna umoja wa wenye viwanda,
Umoja wa wafanya biashara,
Vyama vya wafanyakazi, nk
Mkulima, Mmh!
 
Nakushauri ukalime chakula chako mwenyewe hata robo ekari halafu utwambie umetumia shilingi ngapi.

Kupofusha idara ya kilimo kwa kisingizio cha baa la njaa ni ukosefu wa somo la kilimo biashara (agribusiness). Kadri unavyoondoa mazao mikononi mwa mkulima ndivyo anavyofanya ubunifu kuongeza mizunguko ya kurudi shambani.

Pia kwenye mnyororo wa thamani kilimo kikiingiliwa kinasababisha uhamiaji wa hali ya juu kutoka vijijini kwenda mjini.
 
Suala la kuuza au kutouza nafaka nje.

Yaani niseme kwamba; kulingana na kiwango kidogo cha chakula tulichonacho, sikubaliani na wale wanaotaka tuuze chakula nje. Ndugu zangu msifikiri jambo hili ni rahisi kama mnavyoliona, mkaanza kuilaumu serikali kwa zuio lililopo.

Mtu yeyote mwenye akili timamu; kwanza anajitoshereza mwenyewe, kisha kilichozidi ndicho hukiuza kwa mwenzake.

Utakuwa ni upunguani wa kifkra, kama taifa, tukiuza chakula kwa shilingi, kisha baada ya miezi michache tukatumia akiba ya madola kuagiza chakula hichohicho nje ya nchi.

Pili, ni kweli wakulima wetu wataumia kidogo, nasema kidogo kwa sababu hata wao chakula hiki kitawasaidia baadaye, maana wanauzaga mpaka akiba kwa tamaa ya bei ya angalau, ndiposa baadaye wanateseka sana kwa njaa.

Nasema bei ya angalau kwa sababu kwa kweli mnufaikaji mkubwa wa hili ni mlanguzi.

Tatu, Ukiangali kwa jicho la tatu; sehemu kubwa ya nchi yetu mavuno hayakwenda vizuri. Yaani watnzania wengi hawana chakula.

Utaona ni kipindi cha mavuno lakini bado maeneo mengi bei za chakula hazijarudi mahala pake.

Hivyo ilikuwa vema kama taifa tuamue kuwaumiza wengi au wachache. Sawasawa na dereva wa basi atakayeamua kumkwepa mtu mmoja akaangusha basi zima, au kumgonga huyo na kusalimisha 65.

Mwisho, kulinga na ukame mkubwa unaoendelea kuzikumba nchi nyingi za ukanda huu wa afrika mashariki na kati, siyo vema kutegemea manchi haya makubwa yauziwe chakula na wananchi wanaojilimia kienyeji tu.

Ni kwa nini usifanyike uwekezaji mkubwa kulingana na fursa iliyopo, utakaokidhi hitaji la soko lililopo?

Kwa sababu haiwezekani chakula cha nchi moja kikategemewa na ma…nchi kibao huko ni kutengeneza njaa kwa wahusika wenyewe!

Ungekuwa wewe ni mfanya maamuzi ungefanyaje?
Mimi naungana na wewe kwenye hili la kuzuia vyakula visiuzwe nje ya nchi.
Wananchi wengi hawana chakula cha kutosha msimu huu na ule ujao.
Wanaolalamika kwamba vyakula viuzwe nje ya nchi ni wale walanguzi waliowanunulia wananchi kwa bei ndogo harafu wanataka wakauze huko nje kwa bei kubwa.
 
Vipi waliojiari kwenye mnyororo wa kilimo unasemaje kwa wao kukosa ajira.
Je tuendelee kuongeza idadi ya machinga na bodaboda mijini ambao hawakuzi uchumi wa nchi zaidi ya kuwa ni madalali wa kukuza uchumi wa China.
Mahindi yakiuzwa gunia laki na 20 badala ya elf 25 huoni tunapata pesa za kigeni,watu wakiwa na pesa wataagiza nje chakula
Mwaka huu Kuna uhaba mkubwa sana wa vyakula hasa mahindi na mchele wewe kama unamahindi yalete huku kanda ya ziwa bei ni nzuri.
Huku bado gunia moja ni Tshs 1018000/.
 
Tungeboresha sera ya kilimo, kwa kuwashawishi matajiri angalau wale top 20 tulionao, wawekeze kwenye mashamba makubwa makubwa ya kilimo; na hatimaye kuzalisha zaidi, na kupeleka nje ziada ili tupate fedha za kigeni.​
 
Mwaka huu Kuna uhaba mkubwa sana wa vyakula hasa mahindi na mchele wewe kama unamahindi yalete huku kanda ya ziwa bei ni nzuri.
Huku bado gunia moja ni Tshs 1018000/.
Njombe elf 25 kwa gunia karibu njombe
 
asilimia 70 ya watz ni wakulima. Unasemaje utaumiza wachache?
Mahindi yamevunwa Februari.
Mkulima amenunua magunia ya kuhifadhia,
amenunua dawa ya kuyahifadhi au amenunua magunia maalum -PICS.
Amekodi sehemu ya kuyahifadhi kwa kuwa yeye hana stoo.

Hivi sasa ni msimu wa kuandaa mashamba.
Kwa bei hiI ilivyoporomoka atapata wapi pesa za kununua pembejeo na Nahitaji mengine ya kilimo.

Hali hii itawavutia vijana kuishi vijijini wakiwa wakulima?
 
Vipi waliojiari kwenye mnyororo wa kilimo unasemaje kwa wao kukosa ajira.
Je tuendelee kuongeza idadi ya machinga na bodaboda mijini ambao hawakuzi uchumi wa nchi zaidi ya kuwa ni madalali wa kukuza uchumi wa China.
Mahindi yakiuzwa gunia laki na 20 badala ya elf 25 huoni tunapata pesa za kigeni,watu wakiwa na pesa wataagiza nje chakula
Tanzania bado haijajitoshereza kwa.chakula mpaka iuze nje.
 
Wakulima mwataka waishije?
Chakula isipopanda Bei ni janga kwa wakaazi wa vijijini
 
Suala la kuuza au kutouza nafaka nje.

Yaani niseme kwamba; kulingana na kiwango kidogo cha chakula tulichonacho, sikubaliani na wale wanaotaka tuuze chakula nje. Ndugu zangu msifikiri jambo hili ni rahisi kama mnavyoliona, mkaanza kuilaumu serikali kwa zuio lililopo.

Mtu yeyote mwenye akili timamu; kwanza anajitoshereza mwenyewe, kisha kilichozidi ndicho hukiuza kwa mwenzake.

Utakuwa ni upunguani wa kifkra, kama taifa, tukiuza chakula kwa shilingi, kisha baada ya miezi michache tukatumia akiba ya madola kuagiza chakula hichohicho nje ya nchi.

Pili, ni kweli wakulima wetu wataumia kidogo, nasema kidogo kwa sababu hata wao chakula hiki kitawasaidia baadaye, maana wanauzaga mpaka akiba kwa tamaa ya bei ya angalau, ndiposa baadaye wanateseka sana kwa njaa.

Nasema bei ya angalau kwa sababu kwa kweli mnufaikaji mkubwa wa hili ni mlanguzi.

Tatu, Ukiangali kwa jicho la tatu; sehemu kubwa ya nchi yetu mavuno hayakwenda vizuri. Yaani watnzania wengi hawana chakula.

Utaona ni kipindi cha mavuno lakini bado maeneo mengi bei za chakula hazijarudi mahala pake.

Hivyo ilikuwa vema kama taifa tuamue kuwaumiza wengi au wachache. Sawasawa na dereva wa basi atakayeamua kumkwepa mtu mmoja akaangusha basi zima, au kumgonga huyo na kusalimisha 65.

Mwisho, kulinga na ukame mkubwa unaoendelea kuzikumba nchi nyingi za ukanda huu wa afrika mashariki na kati, siyo vema kutegemea manchi haya makubwa yauziwe chakula na wananchi wanaojilimia kienyeji tu.

Ni kwa nini usifanyike uwekezaji mkubwa kulingana na fursa iliyopo, utakaokidhi hitaji la soko lililopo?

Kwa sababu haiwezekani chakula cha nchi moja kikategemewa na ma…nchi kibao huko ni kutengeneza njaa kwa wahusika wenyewe!

Ungekuwa wewe ni mfanya maamuzi ungefanyaje?
Unamlaumu mlanguzi sijui na wewe unaehitaji uuziwe bei chee tukuitaje
 
Mimi naungana na wewe kwenye hili la kuzuia vyakula visiuzwe nje ya nchi.
Wananchi wengi hawana chakula cha kutosha msimu huu na ule ujao.
Wanaolalamika kwamba vyakula viuzwe nje ya nchi ni wale walanguzi waliowanunulia wananchi kwa bei ndogo harafu wanataka wakauze huko nje kwa bei kubwa.
Baada ya kuzuia mazao kwenda nje bei kwa mkulima imepanda?
 
Back
Top Bottom