Kuvunjika kwa mfupa wa Bega

OCC Doctors

Senior Member
Joined
Jul 20, 2018
Posts
113
Reaction score
172
Fupakola (Clavicle) ni mfupa unaounganisha mkono na mwili, huitwa Mfupa wa Kola (collarbone), ni mara chache sana kuvunjika kwa muundo huu wa mfupa.

Wanaume huathirika zaidi kuliko wanawake. Kuvunjika kwa kawaida husababishwa na majeraha ya michezo au ajali za barabarani au pigo kali la kushtukiza usawa wa bega.

Kuvunjika kunaweza kuumiza mishipa ya damu, mishipa ya neva na mshipa wa mapafu (pulmonary artery).


 
Jazia nyama kidogo basi mkuu
Kwa kawaida mgonjwa hulalamika kwamba alianguka au kupigwa na kitu kizito au kuangukia bega, na kupata kiwewe cha moja kwa moja kwenye mfupa huo wa kola. Huleta maumivu na huruma kwa mgonjwa, uvimbe unaweza kutokea, na ulemavu pia.

Mchubuko unaweza kuwepo, na pia rangi ya ngozi ya sehemu husika inaweza kubadilika na kuwa ya blue au zambarau ambayo hutokea kama matokeo ya kupasuka kwa mishipa ya damu chini ya ngozi (Echymosis). Pia mgonjwa anaweza kuvuja damu kutokana na kuvunjika.

Ikiwa sauti ya upuaji au sauti za pumzi zitapungua kwa mgonjwa wakati wa kutoa na kuingiza hewa kifuani, inaweza kuashiria kuathirika kwa kifua (pneumothorax) ambayo ni mkusanyiko wa hewa nje ya pafu kutokana na pigo la kuvunjika kwa mfupa huo wa kola.
 
Surgery and rest can help to fix it
Ahsante, naweza kuuliza. Nili fall barabarani bahati mbaya nikaadondokea mkono, nikapata radius infection, nikaenda kufanya surgery upande wa radius ukakaa vizuri, ila ule upande mwingine wa Ulna bone bado umenyanyuka juu kidogo. Je naweza kufix kwa kufanya mazoezi au hadi tena surgery?
 
Ikitokea umevunjika kuna namna ya kuweza kufix?
Ndio, hutibiwa kwa uangalifu, kwa kukipumzisha kiungo kwenye kombeo pana la mkono huitwa (broad arm sling)
Kiungo huanza kujihamasisha kadri faraja inavyoruhusu, na kurudi kwa shughuli kamili ndani ya wiki 3-6 mgonja hupona.

Kutokujiunga vizuri (Malunion) ni hali ya kawaida lakini kwa kawaida si tatizo la kiutendaji kwenye fupa kola.
 
Malizia basi mkuu...
 
Ahsante, naweza kuuliza. Nili fall barabarani bahati mbaya nikaadondokea mkono, nikapata radius infection, nikaenda kufanya surgery upande wa radius ukakaa vizuri, ila ule upande mwingine wa Ulna bone bado umenyanyuka juu kidogo. Je naweza kufix kwa kufanya mazoezi au hadi tena surgery?
 
Hutegemea, shida inaweza kuwepo kwenye Kifundo, Maambukizi baada ya urekebishaji wa kuvunjika kwa radius inaweza kuwa tatizo. Hali hiyo inaweza kuhusishwa na 'distal radio-ulnar joint (DRUJ).
 
To be sure naomba kuuliza tena ulipata infection au fracture?

Pia una muda gani tangu umevunjika na surgery kufannyika?

Umewekewa support ndani kwa maana ya chuma plate screw .....?

Then ntaweza kupata mwanga wa kukujibu hapa.
 
Hutegemea, shida inaweza kuwepo kwenye Kifundo, Maambukizi baada ya urekebishaji wa kuvunjika kwa radius inaweza kuwa tatizo. Hali hiyo inaweza kuhusishwa na 'distal radio-ulnar joint (DRUJ).
Sorry chief nadhan akisha specify muda utaweza jua kama bone remodeling imekwisha fanyika au bado
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…