spidernyoka
JF-Expert Member
- Jan 2, 2020
- 7,557
- 20,477
Bora ili vijana warudi mikoani labda wakiona mashamba wataacha kuamini instagram itawafanya wapate hela bila mpango
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwamba warudi mikoani kwenye mashamba ili wafuge nge au?Bora ili vijana warudi mikoani labda wakiona mashamba wataacha kuamini instagram itawafanya wapate hela bila mpango
Yani mtoa mada kawasaidia maisha wangeweza wangembebaNa wabongo ni wabunifu sana naamini wataboresha hii skanka iwe kali zaid!
N'ge wakubwa hawana stimu ila sio mbaya tumekosa mrejeshoDah Jana nimeua n’ge mkubwaa ningejaribuu
Mada haijaletwa kwa lengo la kuhamasisha, mtu akiamua kujaribu ni matakwa yake na akipata hasara ni juu yake mwenyeweHuu uzi hauna faida kwenye jamii zaidi ya hasara kwa vijana wanapenda kuiga.
Taifa litapoteza nguvu kazi kwa sababu ya ulevi wa mdudu nge
Wanatumia nge walio komaa, yani wakubwa ambao sumu zao zipo imara zaidiN'ge wakubwa hawana stimu ila sio mbaya tumekosa mrejesho
Kitu kikishageuka kuwa fursa huwa uoga unatoweka koboko ni nyoka mkali sana ila tu ilivyotokea fursa walitafutwa hadi walianza kujificha porini kabisa.Watanzania wengi ni waoga, hata kumshika nge kwao ni mtihani
Ngoja nimtafute mwanangu yeye ni TESTA ajaribu tuanze na nusu n'ge au kale ka mkia tuYani mtoa mada kawasaidia maisha wangeweza wangembeba
Kwa lengo la kibiashara wanaweza kujaribu, ila kwa matumizi ya ulevi wengi wataogopa kujaribuKitu kikishageuka kuwa fursa huwa uoga unatoweka koboko ni nyoka mkali sana ila tu ilivyotokea fursa walitafutwa hadi walianza kujificha porini kabisa.
Halafu kwa ulevi huo,washindwe kuchinja watu wanaokinzana nao mawazo?Bangi,heroin nk vyote vyao.
Kuvuta n'ge ili kufikia ulevi au to get high ni tatizo linalo kua kwa kasi katika ukanda wa kusini mwa Asia. Mojawapo ya nchi iliyo na matumizi makubwa ya ulevi huu ni Pakistan.
Ulevi au high hiyo inasemekana huwa maradufu zaidi kushinda heroine au cocaine, hudumu mwilini kwa zaidi ya masaa 10 hadi siku 3.
Mtumiaji hupitia maumivu makali kwa muda wa masaa yasiyo pungua sita baada ya kuvuta, kisha ndipo huanza kusikia ulevi au kuwa high.
Maumivu hayo huweza kupelekea kifo kwa mvutaji kwasababu chanzo kikuu cha ulevi huo ni sumu ambayo inapatikana katika maumbile ya n'ge.
MBINU AU NJIA ZA UVUTAJI
Zipo njia au mbinu kuu mbili ambazo hutumiwa na watumiaji ili kufikia mshindo wa ulevi.
1. Baada ya kumpata n'nge aliye komaa, wanamuweka Juani ili akauke, wengine hawatumii jua na wana kausha kwa makaa ya moto.
Baada ya n'nge kukauka wanasaga mabaki hayo na kisha kuvuta moshi kwa kutumia mrija kuelekeza puani.
2. Kunyonga au kuunda msokoto, Wengine wanaunda msokoto na kuchanganya mabaki ya nge ambayo yamesagwa na kuwa kama unga, kisha wana changanya na bangi kisha wanavuta.
Kutokana na vitendo hivi, wapo baadhi ya watu katika maeneo hayo wameona fursa na kuanza kuwatunza au kuwafuga wadudu hao na kisha kuwageuza kuwa biashara kwa kuwauzia waraibu wa ulevi huo.
Kutokana na kukosekana au ufinyu wa upatikanaji wa madawa ya kulevya ambayo yana gharama kubwa, wanatumia njia hii mbadala ambayo ni hatari zaidi kuliko madawa mengine, wengi wanakufa kwani sumu ni kali na huathiri mwili kwa kipindi kifupi.
Kadri siku zinavyozidi kwenda, dunia inashuhudia mbinu mpya za uraibu na matumizi ya madawa hatarishi zaidi.
Huku kwetu tumeona baadhi ya vijana wakitumia taulo za kike kwa matumizi ya pombe, huko kwa wenzetu nao wamekuja na style mpya ya ulevi, kuvuta sumu ya nge.
Nadhani kamkia ndo katakuwa na nguvu, na ukimchoma ananukia sana km panzi, utotoni tumewachoma sana sio kwa lengo la kuvuta ila km kuwaadhibu, halafu hayo meusi makubwa hata hayana sumu km vile vya kahawia tena upate kanakotaga,,, lazima mfeNgoja nimtafute mwanangu yeye ni TESTA ajaribu tuanze na nusu n'ge au kale ka mkia tu
Kuchinja watu sio lazima uwe mlevi, mbona wapo watu wanachinja wenzao bila kuvuta bangi au kutumia heroineHalafu kwa ulevi huo,washindwe kuchinja watu wanaokinzana nao mawazo?Bangi,heroin nk vyote vyao.
Na kimsingi kuna vitu haina haja hata ya kujaribu sasa kitu ambacho ukitumia kuna nafasi kubwa sana ya kupoteza maisha, ila sisi huku nao tuna vichwa vigumu mno kuelewa kuna watu watataka waone.Kwa lengo la kibiashara wanaweza kujaribu, ila kwa matumizi ya ulevi wengi wataogopa kujaribu
Pia ukitumia unaanza kupata maumivu makali, kwaiyo mtu akitaka kujaribu ajiandae na hayo maumivu ya mwili mzimaNa kimsingi kuna vitu haina haja hata ya kujaribu sasa kitu ambacho ukitumia kuna nafasi kubwa sana ya kupoteza maisha, ila sisi huku nao tuna vichwa vigumu mno kuelewa kuna watu watataka waone.
Hao wengine sawa.Mimi nimejikita kwenye nguvu/msukumo wa ziada unaochochea matumizi mabaya ya utu.Kuchinja watu sio lazima uwe mlevi, mbona wapo watu wanachinja wenzao bila kuvuta bangi au kutumia heroine
Sahihi, matumizi ya madawa hubadili akili za watu na wakati mwingine huwafanya watu kuwa wakatiliHao wengine sawa.Mimi nimejikita kwenye nguvu/msukumo wa ziada unaochochea matumizi mabaya ya utu.
Ni kweli kale ka mkia ni dili halafu hayo makubwa yanafaa kwa kuchanganyia tu ha haa!Nadhani kamkia ndo katakuwa na nguvu, na ukimchoma ananukia sana km panzi, utotoni tumewachoma sana sio kwa lengo la kuvuta ila km kuwaadhibu, halafu hayo meusi makubwa hata hayana sumu km vile vya kahawia tena upate kanakotaga,,, lazima mfe
We umeacha kwani kuliwa tackle???Wakati duniani wanalewa kwa nge, nyoka, vyura. Tanzania kumeingia ulevi wa kulewa kwa kutumia "duburi".
. Duburi = tundu la kutolea haja kubwa.