Kuwa mnene au mwenye makalio makubwa isiwe kigezo cha mwanamke kuwa mchekeshaji (comedian)

Kuwa mnene au mwenye makalio makubwa isiwe kigezo cha mwanamke kuwa mchekeshaji (comedian)

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Ninaandika nikiwa na masikitiko makubwa kuona maumbile ya wanawake yanatumika kwenye mambo ya kijinga. Miaka ya hivi karibuni tasnia ya uchekeshaji (comedy) imezidi kuchanja mbuga na kufanya makubwa. Kwa sasa wachekeshaji nao wanaingiza pesa nyingi kama wasanii wengine tofauti na zamani. Wachekeshaji wote walioweza kwenda sawa na uwepo wa mitandao ya kijamii wameweza kuvuna pesa nyingi kutokana na vipaji vyao. Mitandaoni vijana wanapambana ku-upload contents zitakazovuta umati kutazama. Jinsi umati unavyovutika ndo jinsi pesa zinavyoingia. Hakuna longolongo.

Wakati tasnia inavyozidi kukua ndo limejitokeza tatizo la dada zetu waliojaliwa unene na makalio makubwa kutumia maumbile yao katika kuchekesha. Hii ni mbinu ya hovyo na iliyofeli mno. Contents nyingi huwa hazichekeshi zaidi ya kuchochea ngono. Wachekeshaji wengi wenye tatizo hilo ni kutoka Nigeria na hapa Tanzania. Sintotaja majina ya hao wasanii ila mitandaoni wanajulikana. Video nyingi zilizopo ni za kujidhalilisha tu. Hazina mafunzo yoyote wala maadili.

Utashangaa wakati sisi tunakerwa na aina hii ya uchekeshaji kwa wazee wa CHAPUTA kwao ni Full Burudani 😄😄. Yaani hii mijimama inayojifanya comedians imekuwa msaada mkubwa kwa CHAPUTA. Ninawasihi wasanii wetu wajiepushe na aina yoyote ya uchekeshaji ambao hauna maadili.
 
inanikumbusha movie ya nut professor kuna uchekeshaji by attacking personality.
 
Sasa unataka hao wadada waliojaliwa neema za Allah waende wapi? Kwenye u-miss hamuwataki
 
Ninaandika nikiwa na masikitiko makubwa kuona maumbile ya wanawake yanatumika kwenye mambo ya kijinga. Miaka ya hivi karibuni tasnia ya uchekeshaji (comedy) imezidi kuchanja mbuga na kufanya makubwa. Kwa sasa wachekeshaji nao wanaingiza pesa nyingi kama wasanii wengine tofauti na zamani. Wachekeshaji wote walioweza kwenda sawa na uwepo wa mitandao ya kijamii wameweza kuvuna pesa nyingi kutokana na vipaji vyao. Mitandaoni vijana wanapambana ku-upload contents zitakazovuta umati kutazama. Jinsi umati unavyovutika ndo jinsi pesa zinavyoingia. Hakuna longolongo.

Wakati tasnia inavyozidi kukua ndo limejitokeza tatizo la dada zetu waliojaliwa unene na makalio makubwa kutumia maumbile yao katika kuchekesha. Hii ni mbinu ya hovyo na iliyofeli mno. Contents nyingi huwa hazichekeshi zaidi ya kuchochea ngono. Wachekeshaji wengi wenye tatizo hilo ni kutoka Nigeria na hapa Tanzania. Sintotaja majina ya hao wasanii ila mitandaoni wanajulikana. Video nyingi zilizopo ni za kujidhalilisha tu. Hazina mafunzo yoyote wala maadili.

Utashangaa wakati sisi tunakerwa na aina hii ya uchekeshaji kwa wazee wa CHAPUTA kwao ni Full Burudani 😄😄. Yaani hii mijimama inayojifanya comedians imekuwa msaada mkubwa kwa CHAPUTA. Ninawasihi wasanii wetu wajiepushe na aina yoyote ya uchekeshaji ambao hauna maadili.
Kwani wanene pekeee wafanyao hivyo..!!? Wachekeshaji wengi hutumia maumbile yao..!! Mfano Eric Omondi, ule wembamba wake anautumiaga sana kwenye kuchekesha. Haya kuna huyu anaitwa WABOGOJO, aliyeshiriki kwenye wimbo wa Mr. Nice uitwao kikulacho, naye pale si katumia maumbile yake..!? Inawezekana wewe ni mnene na unachukizwa na wanene wafanyao vichekesho kwa kutumia maumbile yao manene, lakini wote wapo hivyo. Kila mmoja akichukia kisa maumbile yanayofanana na yake yametumika asivyopenda, basi hakutakuwa na wachekeshaji
 
Kila mtu ashinde mechi zake.

Mambo yao waachie wenyewe.

Tukutane kileleni.
 
Sasa unataka hao wadada waliojaliwa neema za Allah waende wapi? Kwenye u-miss hamuwataki
Wawe na vipaji vya comedian!

Siku moja nikasikia mtu anasema:"hata kwenye uongozi, kigezo cha kuchaguliwa kimojawapo kwa wanawake kiwe ni makalio makubwa"! [emoji38][emoji38][emoji38]

Sielewi mantiki ya kujali jali sana hivyo vitu!
 
Wawe na vipaji vya comedian!

Siku moja nikasikia mtu anasema:"hata kwenye uongozi, kigezo cha kuchaguliwa kimojawapo kwa wanawake kiwe ni makalio makubwa"! [emoji38][emoji38][emoji38]

Sielewi mantiki ya kujali jali sana hivyo vitu!
Kwamba kuna systematic preferences ya makalio makubwa? Wonder shall never cease
 
Back
Top Bottom