Mkuu unapomtolea mahari au kumhudumia mkeo siyo kwamba unainunua k yake bali ni sehemu ya majukumu ambayo wanaume tuliagizwa kufanya kwa wake zetu yaani ni sawa tu ambavyo wao wanapika wanafua wanaosha vyombo wanafanya usafi wanatunza waume zao na wanalea watoto wao kazi ambazo kwa asilimia kubwa wanaume hatufanyi na bado tunaona kuwa hayo ni majukumu ya wanawake maana sisi wanaume tuliambiwa tutakula kwa jasho letu ila wanawake hawakuambiwa hivyo nadhani ni mgawanyo wa majukumu tu ndo unafanya haya yote yatokee
Kwa sababu sisi tumeng'ang'ania kuwa hizo kazi nilizozitaja hapo juu ni za kike sisi wanaume hatupaswi kufanya na hata tukifanya ni mara moja moja sana na ni kama tunasaidia tu basi hata wao wanaona kuwa kazi za kutafuta hela kuhudumia mke kulipa bills zote na kulipa mahitaji yote ya watoto ni za kwetu na wao hawapaswi kufanya na wakifanya wanasaidia tu japo wapo wanawake wanaofanya ila wanafanya kwa sababu tu hawana jinsi ila siyo majukumu yao kwahiyo mkuu wewe kumhudumia mkeo ambaye na yeye anakuhudumia huko siyo kununua k