VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,137
- 17,908
Wakurugenzi wa Majiji, Manispaa, Miji na Miji Midogo ndiyo waliopanga na kupangika kwa mipango iliyoiwezesha CCM kushinda kwa kishindo. Wao ndiyo walioratibu taratibu bila tabu mbinu zote za ushindi wa CCM kwa mwamvuli wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Wakurugenzi ndiyo walipokea maagizo ya kufanikisha ushindi 'kwa vyovyote vile'. Wakatekeleza. Ushindi ukapatikana.
Kitendo cha kuwabana, kuwasema, kuwasimanga na kuwaumbua Wakurugenzi kwa ununuzi tu wa magari aina ya V8 ni kitendo cha kuwasaliti kichama na kiserikali. Ni kitendo cha kutowalipa vyema fadhila kwa wema walioufanya kwa chama na Serikali wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Sote tunajua, mchakato wa ununuzi wa magari hayo unahusisha ofisi mbalimbali za kiserikali.
Tunajua kuwa ununuzi ulifuata taratibu na kupata baraka zote. Kuwafanya Wakurugenzi ni mbuzi wa kafara katika hili la ununuzi wa ma-V8 si sawa wala si jambo la afya. Wakurugenzi wanastahili heshima pamoja na uwezekano wa kutumbuliwa muda wowote aupendao Mteule wao. Wakurugenzi walikibeba chama uchaguzini, nao wabebwe kwenye utumishi wao. Waachwe, wenye Halmashauri zenye uwezo, kununua ma-V8 ili nao walie kivulini.
Lengo lilikuwa kuufuta upinzani, imekuwaje sisi wenyewe tena kulazimisha uwepo Bungeni?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)
Kitendo cha kuwabana, kuwasema, kuwasimanga na kuwaumbua Wakurugenzi kwa ununuzi tu wa magari aina ya V8 ni kitendo cha kuwasaliti kichama na kiserikali. Ni kitendo cha kutowalipa vyema fadhila kwa wema walioufanya kwa chama na Serikali wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Sote tunajua, mchakato wa ununuzi wa magari hayo unahusisha ofisi mbalimbali za kiserikali.
Tunajua kuwa ununuzi ulifuata taratibu na kupata baraka zote. Kuwafanya Wakurugenzi ni mbuzi wa kafara katika hili la ununuzi wa ma-V8 si sawa wala si jambo la afya. Wakurugenzi wanastahili heshima pamoja na uwezekano wa kutumbuliwa muda wowote aupendao Mteule wao. Wakurugenzi walikibeba chama uchaguzini, nao wabebwe kwenye utumishi wao. Waachwe, wenye Halmashauri zenye uwezo, kununua ma-V8 ili nao walie kivulini.
Lengo lilikuwa kuufuta upinzani, imekuwaje sisi wenyewe tena kulazimisha uwepo Bungeni?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)