Kuyafunua yaliyofunikwa: Historia ya kweli ya Uyahudi na Wayahudi

Kuyafunua yaliyofunikwa: Historia ya kweli ya Uyahudi na Wayahudi

Kisai

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2018
Posts
28,481
Reaction score
28,749
UTANGULIZI
Masiku yamepita huku nikitamani sana kuandika chochote kuhusu Uyahudi na Wayahudi. Kuandika kuhusu chimbuko lao, kuandika kuhusu uhusiano wao na wana wa Israeli,kuandika kuhusu itikadi zao, kuandika kuhusu madai yao kwa nabii wa Mola muumba Musa mwana wa Imraan mwana wa Quhaata mwana wa Lawi mwana wa Yaqoub mwana wa Is'haak mwana wa Ibrahiim.

Lakini kalamu zimeshanyanyuka na wino umeshakauka na historia iliandikwa kitambo sana na wakubwa zetu kwa ubora, wakubwa zetu kwa maarifa na wakubwa zetu kwa umri, na nachokifanya mimi ni kurejea kwao na wala sitaandika jipya ambalo wao hawakuliandika,yaani kwa ufupi sitazua.

Maneno nitakayo yahudhurisha kwenu katika mfululizo wa anuani hii "KUYAFUNUA YALIYO FUNIKWA" ni natija au zao la utafiti wangu wa muda mrefu juu ya historia ya watu hawa. Lakini marejeo yangu hasa hasa yamemili katika vitabu viwili, ambavyo nitavitaja mwishoni mwa mada hii, yaani nikiwa nahitimisha somo hili.

Nini maana ya Uyahudi?
Katika kudurusu tamko hili la "Uyahudi" nitapita katika mapito mawili tofauti, pito la kilugha na pito la kiistilahi.

Maana ya Uyahudi kilugha
Wametofautiana wanazuoni juu ya tamko hili, wapo wanaosema tamko hili limetokana na lugha ya kiarabu katika tamko "al Huud" lenye maana ya toba (kutubia) na kurejea katika utiifu (kutokana na maovu aliyo yafanya mtu).

Wengine wakakataa na kusema hakika tamko hili si lenye asili ya Kiarabu, bali limetokana na mmoja wa watu kutoka katika ukoo (uzao) wa wana wa Israeli naye si mwingine bali ni "YAHUUDHA" (Huyu tutamuelezea kwa undani huko mbeleni) au tamko "Uyahuud/Yahuud" limetokana na ile dola iliyo anzishwa kusini mwa nchi ya Palestina baada kupita nabii Suleyman na hii ndiyo kauli yenye nguvu.

Maana ya Uyahudi kiistilahi
Uyahudi kiistilahi maana yake ni wale watu wanao dai ya kuwa wana mfata nabii Musa.

Sehemu ya pili post #28

Sehemu ya tatu post #113
 
Wayahudi wanakupa tabu sana!

Wako wachache mno ila wana kushuhulisheni kupita maelezo.

Vipi wahindu na mabudha hawawapi shida ingali wako weeeengi sana?
 
Wayahudi wanakupa tabu sana!

Wako wachache mno ila wana kushuhulisheni kupita maelezo.

Vipi wahindu na mabudha hawawapi shida ingali wako weeeengi sana?
Tofauti na Mahindu na Mabudha hawa hawajinasibishi na mtume yeyote ila Mayahudi wanajinasibisha na nabii Musa hali ya kuwa hawana uhusiano wowote na nabii Musa,hili nitalithibitisha huko mbeleni panapo majaliwa.
 
Yaani hata story haijaanza unaleta habari ya itaendelea!
 
Maana ya Uyahudi kiistillahi: Ni kundi la watu wanaofata utamaduni na Mila za Dini ya Kiyahudi ambao asili yao ni waebrania wa kizazi Cha Israel hata Abrahamu.

Na UYAHUDI ni Dini inayo amini katika Mungu mmoja aliyejidhihirisha kwa Abrahamu, Mussa na Manabii wengine wa Kiebrania.

Kuwaelezea Wayahudi na Kuja na Hoja nzuri na zakueleweka inatakiwa urejee Vitu hivi

1. Biblia ya kiebrania
2. Biblia ya Wafuasi wa Kristo
3. Ushahidi wa Akiolojia(Archeological eveidence) wa mambo ya kale hapo mashariki ya kati na Historia
4. Talmud ya wayahudi
5. Kuran na Hadithi za wafuasi wa Dini ya Uislamu
 
Usitarajie kueleweka kwenye hii Mada maana utaegemea zaidi kwenye Mtizamo wa Ki-Islamu na Kuran. Mada kama hii inabidi uwe Neutral yaani usiegemee upande wowote.
Unaweza kunionyesha wapi nimeegemea kwenye Uislamu?

Lakini jalia iwe nimeegemea kwenye Uislamu, unachotakiwa ulete hoja pinzani, kisha ujibu utakacho ulizwa, hii ndiyo maana ya elimu, na hatupo hapa kwa ajili ya kuwaridhisha watu au fulani atasemaje au fulani ataelewa au hatoelewa, cha msingi ni kuandika ukweli,ukweli ambao kalamu ulishauandika zamani sana.
 
Maana ya Uyahudi kiistillahi: Ni kundi la watu wanaofata utamaduni na Mila za Dini ya Kiyahudi ambao asili yao ni waebrania wa kizazi Cha Israel hata Abrahamu.
Safi kabisa, sasa vipi Wayahudi wanajinasibisha na nabii Musa huku wakidai wanafata Torati ?

Swali lingine la msingi, sababu Historia imeshaandika, na dhuria ya wana wa Israeli inajulikana, je ni uzao gani au ni nani katika wana wa Israeli walikuwa ni Mayahudi ?
Na UYAHUDI ni Dini inayo amini katika Mungu mmoja aliyejidhihirisha kwa Abrahamu, Mussa na Manabii wengine wa Kiebrania.
Unaweza kulithibitisha hili ? Naomba ushahidi wa hili.
 
Kuwaelezea Wayahudi na Kuja na Hoja nzuri na zakueleweka inatakiwa urejee Vitu hivi

1. Biblia ya kiebrania
2. Biblia ya Wafuasi wa Kristo
3. Ushahidi wa Akiolojia(Archeological eveidence) wa mambo ya kale hapo mashariki ya kati na Historia
4. Talmud ya wayahudi
Hili jukumu nakuomba ulifanye wewe, mimi napita katika mapito yangu, kisha tutakuja kuulizana maswali, ili tuone nani mkweli katika hili.
 
Unaweza kunionyesha wapi nimeegemea kwenye Uislamu ?

Lakini jalia iwe nimeegemea kwenye Uislamu, unachotakiwa ulete hoja pinzani, kisha ujibu utakacho ulizwa, hii ndiyo maana ya elimu, na hatupo hapa kwa ajili ya kuwaridhisha watu au fulani atasemaje au fulani ataelewa au hatoelewa, cha msingi ni kuandika ukweli,ukweli ambao kalamu ulishauandika zamani sana.

Sawa Boss kama una ahidi utakua Neutral.
 
Ila kitu kimoja tu kinaniudhi kuhusu waislamu kujipendekeza kwa wakristo .....

Yaani wanalazimisha Ibrahim wa kwenye Bible awe ndo yule wa kwenye quran yaani Yesu wa kwenye biblia eti ndio issa bin Mariam wa kwenye quran.......huko ni kikosea heshima Ukristo....

Tangu lini daudi wa buza awe ndo yule daudi wa Masaki?
 
Ila kitu kimoja tu kinaniudhi kuhusu waislamu kujipendekeza kwa wakristo .....

Yaani wanalazimisha Ibrahim wa kwenye Bible awe ndo yule wa kwenye quran yaani Yesu wa kwenye biblia eti ndio issa bin Mariam wa kwenye quran.......huko ni kikosea heshima Ukristo....

Tangu lini daudi wa buza awe ndo yule daudi wa Masaki?
Usije wewe ukataka kubadilisha yaliondikwa
 
Ila kitu kimoja tu kinaniudhi kuhusu waislamu kujipendekeza kwa wakristo .....

Yaani wanalazimisha Ibrahim wa kwenye Bible awe ndo yule wa kwenye quran yaani Yesu wa kwenye biblia eti ndio issa bin Mariam wa kwenye quran.......huko ni kikosea heshima Ukristo....

Tangu lini daudi wa buza awe ndo yule daudi wa Masaki?
Hil limeshajadiliwa sanna humu, na elimu iko wazi.

Hata wewe mpaka unakufa huwezi kuthibitisha ya kuwa Ibrahiim wa Biblia siyi wa Qur'aan, Yesu wa Biblia siyo Issa wa Qur'aan.

Shida yenu huwa mnayaandika haya tatizo linakuja kwenye kuthibitisha haya mnayo yaandika.
 
SHUKRANI KWA MASWALI MAZURI BOSS, MAJIBU YANGU NI KAMA IFUATAVYO;

Safi kabisa, sasa vipi Wayahudi wanajinasibisha na nabii Musa huku wakidai wanafata Torati ?

WAYAHUDI wanajinasibisha na NABII MUSA kwa Mantiki ya kwamba Wao ni Muendelezo wa Uzao wa Kabila la YUDA(Ref Biblia Kitabu Cha MWANZO 29:35),
Na YUDA alikua ni Mmoja kati ya Watoto Kumi na Wawili wa Uzao wa YAKOBO(ISRAEL), Katika hao Watoto 12 wa YAKOBO mmoja wao Aliitwa LEVI( Ref Biblia kitabu cha MWANZO29:34)
Na kutoka Uzao wa LEVI alizaliwa KEHATH(Ref Biblia kitabu cha MWANZO46:11, Biblia kitabu cha MAMBO YA NYAKATI 1-6:1) KEHATH aliyekuwa Baba Wa AMRAM(Ref Biblia Kitabu cha HESABU26:59) Na Huyu AMRAM ndo Baba Mzazi wa NABII MUSA.....Kwahiyo Ukiangalia hii Family Lineage utaona WAYAHUDI na NABII MUSSA Ulikua Muendelezo wa Uzao wa YAKOBO( ISRAEL)

Kuhusu Torati kwa Mujibu wa Dini ya UYAHUDI ni Mjumuiko wa Vitabu Vitano Vya Mwanzo katika BIBLIA YA KIYAHUDI vinavyeleza MAFUNDISHO, MWONGOZO na SHERIA kwa Wana Wa ISRAEL, Na hii Torati Iliandaliwa na MUSSA kwa Maono Ya MUNGU WA ISRAEL...Kwahiyo Kwa Mantiki hii WAYAHUDI Moja kwa Moja Lazima wajinasibishe na TORATI ya MUSSA.



Swali lingine la msingi, sababu Historia imeshaandika, na dhuria ya wana wa Israeli inajulikana, je ni uzao gani au ni nani katika wana wa Israeli walikuwa ni Mayahudi ?

MAJIBU: Hili swali nimeshakujibu hapo Juu kwamba WAYAHUDI wanajinasibisha ni Muendelezo wa Uzao wa Kabila la YUDA(Ref Biblia Kitabu Cha MWANZO 29:35),
Na YUDA alikua ni Mmoja kati ya Watoto Kumi na Wawili wa Uzao wa YAKOBO(ISRAEL)


Unaweza kulithibitisha hili ? Naomba ushahidi wa hili.

MAJIBU:
Katika BIBLIA YA KIEBRANIA MUNGU amejitanabaisha kua ni MMOJA kwa Mantiki hii

KITABU CHA KUTOKA20:2-3 inasema "Mimi ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.
Usiwe na miungu mingine ila mimi".......Ukiangalia hapa MUNGU katua Neno "MIMI" kuashiria ni MMOJA.

KUMBUKUMBU LA TORATI 4:39 inasema "Kwa hiyo ujue, leo hivi, ukaweke moyoni mwako, ya kuwa Bwana ndiye Mungu katika mbingu juu, na katika nchi chini; hapana mwingine. "

Kuna mistari mingine Mingi sana Inayooneshwa katika BIBILIA YA KIEBRANIA KUWA NI MMOJA....Unaweza pitia Na Hii...KUMBUKU LATORATI 6:4, 2 SAMUELI 7:22, NEHEMIAH 9:6.

Pia Tukiangalia kwenye KURAN Utaona kuna Mkanganyiko Kidogo Kuhusu Wana wa Israel kuabudu MUNGU MMOJA Mfano Ukiangalia
SURAH AT-TAWBA 9:30 inasema wana wa Israel wanasema kua UZAIR ni Mwana Wa Mungu na Wanamuabudu.....Lakini pia kwene KURAN pia kuna Mistari Inasema Wana wa Israel waliabudu katika Mungu Mmoja.

Na Hayo ni baadhi ya Majibu yangu Boss.
 
Back
Top Bottom