Kuzaa si kupata ni kumuomba Mungu tu

Kuzaa si kupata ni kumuomba Mungu tu

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Jirani yangu Rosa alijaliwa mtoto mmoja wa kiume. Walimsomesha mtotoekatika shule za gharama na walimpa kila kilichokua katika uwezo wao. Rosa na mume wake walijenga nyumba nadhifu na mume alidariki miaka michache iliyopita.

Kijana wa Rosa amekuwa mtu wa hovyo hovyo asiye elewa thamani ya pesa. Kila mara aliomba hela kwa mama yake, mama alijibu unae a kutoa vi akiba vyake, ilifika hatua ikabidi auzewna dhahabu zake.

Mwaka jana Rosa aligundulika na saratani ya kizazi, kwakua alidhoofu sana hata nguvu za kuanza mionzi ya tiba hakuwa nazo. Mtoto wa pekee wa Rosa ameshapata mteja wa kununua nyumba ya mama yake anasubiri tu Israele afanye yake, hata hospitali kumuona mama yake haendi.
 
"Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo"

"Sitaki mwanangu apitie maisha niliyopitia mimi"
Hapa duniani wote tutapambana na mitihani, hata umuandalie vipi mtoto lazima atakutwa a na changamoto tu. Ninadhani kitu muhimu ni kumjengea confidence ya kujiamini.
 
Mi sina mtoto ila kuzaa naona ni raha hata Kama mtoto awe kichaa ni moja ya ukamilifu Kama binadamu
 
Back
Top Bottom