Kuzingatia "vichwa": Wanawake sio ubaguzi huu??

Kuzingatia "vichwa": Wanawake sio ubaguzi huu??

Tuko

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2010
Posts
11,180
Reaction score
7,346
Katika stori na mdada fulani ambaye tumefahamiana mda mrefu aliniambia kuwa ana mimba, but sio ya boyfriend wake. Nilianza kumshushia lawama za u-infidelity hadi akapata mimba 'nje', yeye akasema hapana, it was planned. Anasema boyfriend aliye naye hawana mpango wa kuoana, bali kuondoleana upweke.

Akasema kwa age aliyo nayo, hana tena mpango wa kuolewa na ameamua kuzaa akizingatia kuwa ana kipato kizuri so kujilea na kulea watoto walau wawili sio shida kwake.

Then nikamuuliza why asizae na huyo boyfriend, akasema amemsoma akagundua kichwani sio mkali sana. Anasema huyo jamaa hata darasani hakuwa 'mzuri', na pamoja na kusoma shule nzuri matokeo yake hayakuwa ya kuridhisha.

So, ameamua kwenda kuzaa na mtu mwingine (tena mme wa mtu), ambaye anaijua historia yake kuwa darasani zilikuwa zinachemka kisawasawa, na hata kazini alipo sasa wanamkubali.

Eti ameamua kufanya hivyo kwani anajijua hata yeye sio kichwa sana, so anaona akizaa na mtu kama yeye tena, mtoto atakayezaliwa hata kuandika jina lake itahitajika kazi kubwa.

Anaamini akizaa na mwanaume 'kichwa' uwezekano wa kupata 'average' au 'kakichwa' ni mkubwa!!!! na nasema siku hizi wapo wanawake wengi tu wanafanya hivyo, wengine wakichagua wacheza mpira, wanamuziki, waigizaji maarufu nk ili tu watoto ikitokea waje wafananie baba zao ...

Ingawa alisimamia sana hoja yake, but mwishoni mi nilibaki na msimamo wangu kuwa huo ni ubaguzi kwani tukiangalia mambo kama hayo, wale 'mabongolala' tutakuwa extincted.

Kama kuna mwanamke ana mawazo kama haya humu, naomba tu ayaache, na aache ubaguzi...
 
mimi nataka mrefu mweusi awe na mvuto maana mimi sina kuviile
ila division ziro hapana kwa kweli......
ziro ni noma heri lasaba wazazi wakakosa ada ......
 
Sasa we unataka watu wawaandae kabisa watoto wao kuwa wazembe?

Alafu eti unasema ubaguzi. . .mbona nyie wanawake hua mnachagua (kwakuzingatia yale mpendayo) na sio mnachukua chukua tu?
 
Unajua sheria ya nature inataka only the fittest to survive
Zamani kua fit ilikua ni kukimbia, kuwinda na kulima sana
Leo kua fit ni uwezo wa kufikiria, uwezo wa kazi nzuri etc.
Basi dada katumia law of nature selection, only the fittest...
But sijui kama akili nazo ni hereditary kama anavo pendekeza
 
craziness ya 'human cloning' ndipo inapoanzia...
 
Sasa mie kilaza, nitafuta kilaza mwenzangu, hivi kweli huyo mwanangu mtarajiwa namtakia nini?

Kwa weli hata mie namsapoti tu

Mtoto kujua 'a' hadi akaombewe?

Hivi mshaona trend za familia fulani fulani???? Wala msiseme kitu kabisa hapa.
 
Kumbe hii kitu ipo serious namna hii! Sasa wale wanaofaulu kwa kuiba pepa na kudesa inakuwaje hapa! Si unaweza ingia chaka!?
 
Kuanzia leo natembea na vyeti vyangu kabisa kumbe imefika huko.....Halafu mkuu siku hizi watu hawana aibu kuzaa nje ya ndoa ama kuzaa na mume wa mtu..Kifupi wamehalalisha style hiyo ya maisha.
 
Tena kweli, aliyepata wani ya 7 fomu 4 na wani ya 3 fomu six, nina yai moja mkononi nauza.
Au leta viazi tutengeneze chips yai.
 
Kuanzia leo natembea na vyeti vyangu kabisa kumbe imefika huko.....Halafu mkuu siku hizi watu hawana aibu kuzaa nje ya ndoa ama kuzaa na mume wa mtu..Kifupi wamehalalisha style hiyo ya maisha.

sio kutembea na vyeti tu, pia personality ... how gentle, caring and nurturing you are, how think is your pocket etc.

Poleni vijana wa leo.
 
Sasa mie kilaza, nitafuta kilaza mwenzangu, hivi kweli huyo mwanangu mtarajiwa namtakia nini?

Kwa weli hata mie namsapoti tu

Mtoto kujua 'a' hadi akaombewe?

Hivi mshaona trend za familia fulani fulani???? Wala msiseme kitu kabisa hapa.
tatizo wanaume wanatuona wajinga sana... kwanza mtu kaamua kujizalia mwenyewe ... lazima awe selective atii
kuna genias mmoja ni dokta muhimbili ndo nammendea....
 
Kumbe hii kitu ipo serious namna hii! Sasa wale wanaofaulu kwa kuiba pepa na kudesa inakuwaje hapa! Si unaweza ingia chaka!?
hata iyo ni akili .... unadhani kuiba paper bila kushikwa upite form 4 upite six ..upite chuo semister 6 au zaidi .... si mchezo mkuu ... wewe ni mkali pia
 
He he he he, mie natafuta roketi sayantisti

tatizo wanaume wanatuona wajinga sana... kwanza mtu kaamua kujizalia mwenyewe ... lazima awe selective atii
kuna genias mmoja ni dokta muhimbili ndo nammendea....
 
mm nimekutana na sista mmoja kama huyo ,yaan mama ameshazeeka ana watoto watatu lakin anachokiwaza yy na ameachika na wanaume wawili lakin mawazo yake kama hayo ,sasa kusema la kweli sifahamu inakuwaje ata mtu akawaza yasio wazika ,,hahaha
 
Ila ndo maana wanasayansi wanashauri kabla ya kuoa uangalie history ya familia. Mie nimeamini its true. We unaoa mwanamke kashindwa shule, kichwa ya biashara hana, unataka nini hapo? Unazaa mataahira!
 
he he he he, mie natafuta roketi sayantisti
teh mtu karisiti paper ya form foo weeee anafundisha chekechea ..... Mmmh ngoja ninyamaze wasije nipasulia server humu
 
nimependa hiyo aidia ya dada....katumia akili sana.....
 
Back
Top Bottom