Pre GE2025 Kuzuia uchafu kwenye uchaguzi, tufute mishahara kwa wachaguliwa wote

Pre GE2025 Kuzuia uchafu kwenye uchaguzi, tufute mishahara kwa wachaguliwa wote

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Tunapenda kuwaza yasiyowezekana na kuacha kufikiria kufanya yale yenye kuwezekana hata kama ni kidogo kidogo.
Hebu taja hayo kidogo kidogo yaliyoshindikana miaka zaidi ya 30 Sasa, huku chaguzi zikizidi kuwa za kihayawani.
 
Hebu taja hayo kidogo kidogo yaliyoshindikana miaka zaidi ya 30 Sasa, huku chaguzi zikizidi kuwa za kihayawani.
Sasa mkuu kama hayo madogo tunakubali tumeshindwa kufanya sasa hayo makubwa unafikiri yatatokea kwa miujiza?
 
Nchi Yenye Matatizo makubwa ya umaskini, huduma na mifumo mbalimbali, kama ilivyo Tanzania, ili iweze kutoka ilipo, inahitaji viongozi wenye ubunifu zaidi, akili zaidi, uadilifu zaidi na uzalendo zaidi kuliko Nchi zilizoendelea.

Bahati mbaya, nchi hizi zenye matatizo kama Tanzania, ndiyo zinazoongoza kuwa na viongozi walio duni zaidi katika ubunifu, uadilifu, akili na uzalendo. Wengi wanatafuta uongozi ili waondokane na umaskini au ili wajitajirishe zaidi, na hivyo kuyaongeza matatizo zaidi kuliko kuyapunguza.

Ni vema tukawa na mfumo unaowachekecha wale wote wanaoutafuta uongozi ili kujitajirisha na kujineemesha.

Kwa kuanzia, tungeweka sheria ya kipindi cha mpito, angalao cha miaka 20, viongozi wa kisiasa, wale wanaochaguliwa na wananchi, wasiwe na mishahara. Badala yake walipiwe gharama kama vile malazi, usafiri, matibabu, na chakula tu, pale wanapokuwa mbali na makazi yao. Lengo iwe ni kuwaondoa wale wote wanaoutafuta uongozi kwa dhamira ya kujineemesha.

Kisha kuwe na sheria maalum kwaajili ya kuwadhibiti viongozi ambao watakuwa wamekosa uadilifu kama vile kupokea rushwa au malipo yoyote yanayohusiana na ufisadi. Viongozi hao baada ya kumaliza muda wao, kuwe na kamati maalum ya kufuatilia utendaji wao wakati wakiwa viongozi, na wale wote ambao watathibitika bila shaka kuwa walifanya kazi kwa weledi mkubwa, ujasiri, ubunifu, na kwa uadilifu mkubwa, watapewa vyeti maalum na kupewa malipo ya mara moja ya uongozi uliotukuka. Wale ambao watathibitika kutenda kinyume chake, watatangazwa majina yao kwa umma, na wasiruhusiwe kugombea nafasi yoyote ya uongozi kwa kipindi cha miaka 20.

Hii itawafanya wanaotafuta pesa kupitia uongozi kutogombea uongozi, na waliopo kwenye uongozi kufanya kila wawezalo kutenda vyema ili mwisho wa term yao wapate mafao mazuri, na kuruhusiwa kugombea uongozi.

Tukiwekwa sheria ya namna hii, hakika nami na wengine wengi wasiopenda kuchafuliwa na mifumo ya kifisadi iliyopo, tutagombea uongozi.

Kama kweli mtu unasema unataka kuwasaidia watu na Taifa kupitia uongozi, basi dhamira hiyo ionekane kwa vitendo. Isiwe kinyume chake. Unasema unataka kuwasaidia watu kupitia uongozi kumbe unataka kuwaibia watu na Taifa kupitia uongozi. Nchi inahitaji viongozi wanaoumizwa na matatizo ya Taifa, lakini siyo kuumizwa tu bali wenye uwezo na walio wabunifu wa kuyaondoa au kuyapunguza hayo matatizo yanayowaumiza.
Umeangalia mbali sana... Mkuu
 
Sasa mkuu kama hayo madogo tunakubali tumeshindwa kufanya sasa hayo makubwa unafikiri yatatokea kwa miujiza?
Pitia kilichotekea Libya, Sudan, Egypt, Gabon nk, huko kote hayo madogo hayakuwa yanawezekana, yalikuja kuwezekana hayo makubwa tu. Au ilikuwa ni miujiza?
 
Hivi haiwezekani ukaanzishwa mjadala wa kitaifa juu ya kuondoa malipo kwa wabunge na madiwani ?
Walio tayari ningependa waseme. Kukiwa na uungwaji mkono mkubwa wa wazo hili, na wakawepo walio tayari kujitolea kushirikiana katika kuhakikisha mjadala huu unafanikiwa, mimi nipo tayari kuanzisha kongamano la kitaifa la wapiga kura kwa lengo la kujenga hamasa ya aina ya viongozi sisi wapiga kura tunaowataka..
 
Nchi Yenye Matatizo makubwa ya umaskini, huduma na mifumo mbalimbali, kama ilivyo Tanzania, ili iweze kutoka ilipo, inahitaji viongozi wenye ubunifu zaidi, akili zaidi, uadilifu zaidi na uzalendo zaidi kuliko Nchi zilizoendelea.

Bahati mbaya, nchi hizi zenye matatizo kama Tanzania, ndiyo zinazoongoza kuwa na viongozi walio duni zaidi katika ubunifu, uadilifu, akili na uzalendo. Wengi wanatafuta uongozi ili waondokane na umaskini au ili wajitajirishe zaidi, na hivyo kuyaongeza matatizo zaidi kuliko kuyapunguza.

Ni vema tukawa na mfumo unaowachekecha wale wote wanaoutafuta uongozi ili kujitajirisha na kujineemesha.

Kwa kuanzia, tungeweka sheria ya kipindi cha mpito, angalao cha miaka 20, viongozi wa kisiasa, wale wanaochaguliwa na wananchi, wasiwe na mishahara. Badala yake walipiwe gharama kama vile malazi, usafiri, matibabu, na chakula tu, pale wanapokuwa mbali na makazi yao. Lengo iwe ni kuwaondoa wale wote wanaoutafuta uongozi kwa dhamira ya kujineemesha.

Kisha kuwe na sheria maalum kwaajili ya kuwadhibiti viongozi ambao watakuwa wamekosa uadilifu kama vile kupokea rushwa au malipo yoyote yanayohusiana na ufisadi. Viongozi hao baada ya kumaliza muda wao, kuwe na kamati maalum ya kufuatilia utendaji wao wakati wakiwa viongozi, na wale wote ambao watathibitika bila shaka kuwa walifanya kazi kwa weledi mkubwa, ujasiri, ubunifu, na kwa uadilifu mkubwa, watapewa vyeti maalum na kupewa malipo ya mara moja ya uongozi uliotukuka. Wale ambao watathibitika kutenda kinyume chake, watatangazwa majina yao kwa umma, na wasiruhusiwe kugombea nafasi yoyote ya uongozi kwa kipindi cha miaka 20.

Hii itawafanya wanaotafuta pesa kupitia uongozi kutogombea uongozi, na waliopo kwenye uongozi kufanya kila wawezalo kutenda vyema ili mwisho wa term yao wapate mafao mazuri, na kuruhusiwa kugombea uongozi.

Tukiwekwa sheria ya namna hii, hakika nami na wengine wengi wasiopenda kuchafuliwa na mifumo ya kifisadi iliyopo, tutagombea uongozi.

Kama kweli mtu unasema unataka kuwasaidia watu na Taifa kupitia uongozi, basi dhamira hiyo ionekane kwa vitendo. Isiwe kinyume chake. Unasema unataka kuwasaidia watu kupitia uongozi kumbe unataka kuwaibia watu na Taifa kupitia uongozi. Nchi inahitaji viongozi wanaoumizwa na matatizo ya Taifa, lakini siyo kuumizwa tu bali wenye uwezo na walio wabunifu wa kuyaondoa au kuyapunguza hayo matatizo yanayowaumiza.
Well Said
 
Pitia kilichotekea Libya, Sudan, Egypt, Gabon nk, huko kote hayo madogo hayakuwa yanawezekana, yalikuja kuwezekana hayo makubwa tu. Au ilikuwa ni miujiza?
Sio kila kilichotokea huko kinaweza kutokea na sehemu zengine, hii dunia ina historia nyingi na mifano mingi tu sasa wewe umechagua mifano ya matukio yaliyotokea katika hizo nchi haina maana na sisi lazima tutapita huko huko. Ukiangalia mazingira yetu sioni dalili ya hicho kitu kutokea sasa kukaa na kusubiri kitokee ndio sawa na kusubiri miujiza.

Kama machafuko tungeyaona ile 2020.
 
Back
Top Bottom