INAUZWA Kwa anayetaka kufungua biashara ya kuuzia watu filamu au nyimbo (softcopy) karibu tufanye biashara

Una La Revenge ile ya Mexico English version?
 
Una La Revenge ile ya Mexico English version?
Hapana sina,Movie ambazo mteja anahitaji na sina kwenye Store Huwa nazi download mteja unaifata movie yako kesho au jioni kutegemea na umekuja saa ngapi na speed ya internet kwa siku husika.

Lakini huwezi fika ofisini ukakosa movie labda uwe huna subira ya kusubiri movie yako ishushwe,kama uvumilivu upo basi hata uje na movie list mkeka mzima utapata movie zote.

Karibu
 
Kwa staili hii vijana hawakupigi kweli au umeweka camera?
Napigwa sana na najua napigwa,Muhimu hesabu yangu ya kila siku ifike,Nina Chat ambayo inaonyesha kila siku hesabu inahtajika sh ngapi.

Sijaweka kama Boda Boda,wao wanaambiwa hesabu sh 10,000 kwa siku,Mimi kwangu ipo tofauti.

Mfano wa Chat ni kama huu (hzi bei n mfano)

J3 = 100,000 (kiti ki 1 @50k)
J4=150,000 (kiti ki 1 @75k)
J5=200,000 (kiti ki 1@100k)
ALH=200,000(kiti ki 1@100k)
IJUM=200,000(kiti ki 1@100k)
JMOS=300,000(kiti ki1@150k)
J.PILI=300,000(kiti ki1@150k)

Nikisema kiti ki 1 maana yake ofisi zote zina computer mbili yani vijana wawili kila mmoja na mashine yake,na kila mmoja ana hesabu anatakiwa afikishe asipofikisha watajua na mwenzake wanasaidianaje jioni nikirudi nipate hesabu kamili.

Kijana atae ingia kazini anajua kabisa leo J3 boss akija kuchukua hesabu anakuja fata kiasi kadhaa, ninapoenda jioni siulizi A wala B nawambia tu wanipe changu.

wao wapate wasipate changu wananipa,na haijawahi tokea siku wakashndwa kunipa,Ofisi ina Generator umeme sio kigezo cha kukosa hesabu yangu.

Wanapiga pesa refu zaidi najua, maana wafanyakazi wangu Siwalipi mishahara wanajilipa wenyewe na ofisi zangu zinaenda,Japo kuibiwa nishaibiwa sana mpk hapo nilipokuja na huu utaratbu wakuweka hesabu.

Maana najua siku gani zina hela na siku gani hazina hela Najua.
 
Mkuu mi nataka nifungue hii mkoa muda baada yakama. Miezi miwili hivi... nilitembelea ofisi ya cipherdot kuchukua series jamaa huwa mnatumia siftware gani...

Je kwa mwanzo ntahitaji nini na nini mkuu kwamtaji wa kama milioni nne hivi
 
Mkuu mi nataka nifungue hii mkoa muda baada yakama. Miezi miwili hivi... nilitembelea ofisi ya cipherdot kuchukua series jamaa huwa mnatumia siftware gani...

Je kwa mwanzo ntahitaji nini na nini mkuu kwamtaji wa kama milioni nne hivi
1.Computer (Yenye Window Ten na SSD 256GB atleast)
2.STORAGE DEVICES (hard disk internal plus external)
3.Mzigo wa kazi

Mengine ni mbwembwe zako kulingana na malengo yako ktk hii kazi huko mbeleni,hivyo malengo yako ndio yatafanya gharama zpande au zishuke,4M unaweza anza na maisha yakaenda. (bila mbwembwe)
 
Ombi
Kwa yeyote mwenye office au atakayefungua office ya Movies kwa dar,kijana wenu nipo hapa naomba Fursa ya kukaa golini,mwaminifu na naijua computer vizuri ,pia nitakusaidia katika kuandaa matangazo ya kuvuta wateja hasa wa online. kwa ujuzi wangu wa Photoshop,After effects na social media .najua nitaongeza value kubwa sana katika biashara yako. Tafadhalini sana wakuu [emoji120]
 
Shukrani sana chief
 
Mkuu hujawahi kuwaza hii ya kuuza online hasa kwa link ama telegram, maana naona hii kama ipo vizuri pia, hasa kwa hizi movie zilizoingizwa maneno ya kiswahili. Maana huwa unanunua mzigo kila wiki wa ofisi, hivyo inakuwa kama unakaba kote. Mfano huyu castillarmovies jamaa yeye anauza online tu promo zake naziona kwenye pages mbalimbali za public figures.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…