Kwa Benchikha, Simba imeonyesha jeuri ya pesa sasa tunasubiri tuione pia kwa wachezaji wapya

Nadhani huyu atawarudisha uwanjani mashabiki mechi ya nyumbani na wydad ambayo ndio itatoa dira ya simba ktk cafcl
 
Wengi wenu huwa mnasoma au kusikiliza ili mkimbilie kujibu siyo muelewe kwanza mnachosoma au kusikia.

Unajifunza kitu ambacho haukijui, sasa unataka kusema Simba haijui jinsi ya kupata wachezaji wazuri? Ndiyo maana nimetumia neno "mdudu" kwa maana kuna vimelea vya bakteria ndiyo vimevuruga mfumo wa kupata wachezaji pale Simba, vikiondolewa hivyo mambo yatakaa sawa.
 
Duh, kule USMA kocha alivunja mkataba? Au mkataba uliisha haukuongezwa au USMA waliamua kuachana nae kwa makubaliano ya pande zote mbili?

Anacheza nafasi gani huyo mliye msajiri?
Ana umri wa miaka mingapi ukilinganisha na wachezaji wenzake hapo Msimbazi?
Toa hoja yako acha kuuliza maswali ya kiduwanzi. Mtoto wa kiume unaumauma maneno ili iweje?
 
Ushauri mzuri
 
Ili Simba iende vizuri uswahili uondolewe.

Inabidi Dewji aweke mtu wake pale, kama enzi za Babra
 
Unamaanisha hata Bigilimana kumbe ni 10 percent aliyoipiga GSM?

Ni wachezaji wangapi wamekuja Yanga na wakashindwa kuperform Je, zilikuwa 10 percent za nani?

Wakati Simba anachukua taji la VPL mara nne mfululizo ishu ya 10 percent ilikuwa ipo au haipo?

Azam FC ana miaka mingi anasuasua tu upande wa ligi iwe ndani au nje je nako kuna 10 percent inayoleta hayo?

Barcelona imesota karibu 5 years now inasuasua je , ishu ni 10 percent?

Watanzania tusipende kusema mambo kwa hisia sana wakati ukweli hatuujui itatusaidia sana kupiga hatua kubwa katika nyanja zote za maisha.

 
kwani hersi hapigi Ten Percent
angalia Makudubela, Kambole, Gift Fred, Beki la Chan kutoka mali nk sehemu ambayo yanga wamefanikiwa ni kukusanya wachezaji bora wazawa hapa wamefanikiwa sana
 
Namkumbusha aliyehusika kumleta Benchikha ausome tena uzi huu.

Kwa kuongezea, nashauri mwishoni mwa msimu Saido Ntiba aondolewe kwenye roster apewe mkataba wa kukaa kwenye benchi la ufundi kama atakuwa tayari kustaafu kucheza, maana inaonyesha labda wameona chaka la kuendelea kumkumbatia ni msaada kwenye ukalimani ila imetosha kushikilia namba za vijana.

Pia Simba inabidi ibadili fikra kwa kurudi tena kupenda damu changa na kuwakubali. Angalia timu kama Senegal au Ghana, huwa hazioni shida kuingiza vijana wapya katika vikosi vyao vya taifa na maisha yanaendelea na ubora unabaki ule ule. Hii misimu miwili ingetosha kuisuka upya Simba lakini misimu imepotea bila mafanikio na wakati huo huo zoezi la kusuka upya kikosi lilikwama maana damu changa zinazoweza kuibeba upya Simba zinasajiliwa halafu hazipewi nafasi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…