Kwa documentary ya Pele hii iliyotoka nitakuwa mpuuzi kuendelea kumlinganisha na watoto wadogo kina Messi

Kwan wee jamaa unataka kusema nini?
 
Watasema yote lkn ukweli utabaki pale pale kuwa hakuna mchezaji aliyewahi kuwa bora duniani kama Pele.

Nakumbuka ile fainali ya World Cup 1970 kule Mexico, Brazil iliichapa Italy 4-1 na ndipo Pele akiwa na miaka 29 aliamua kustaafu kuichezea timu ya taifa kufuatia kuchoshwa na rafu za mabeki kwani enzi hizo Strikers hawakulindwa na marefa kama zama za akina Maradona na wengine.

Maradona aliwika tu kwenye World Cup moja tu, ile ya 1986 pia kule Mexico walipoitoa England semi final kwa goli la mkono kabla ya kuichapa West Germany 3-2 ktk fainali.

Baada ya hapo Maradona "Was a pale shadow of what he was in the year 1986", na Maradona na Argentina hawakuweza kuleta tena impact ktk international football stage. Pele akiwa na Brazil walishinda World Cup mara tatu 1958, 1962 na 1970.

In my view, Pele remains the greatest soccer superstar of all time and hence the living soccer legend.

Nashangaa eti leo hii mtu anataka kuwalinganisha hawa wachezaji wa leo wanaopenda ku-dive na akina Pele, Didi, Garrincha, Tostao, Franke Puskas, Eusebio, Charlton, Best, Bobby Moore, Banks, Gerd Muller, Frank Backenbbaur, Cryff, Van de Kekoff, Kempes, Burruchagga, Luis Brown, Pasarella, Ardilles, Zico, Socrates, Falcao, Boniek, Latto, Rossi, Scirea, Zoff and the list goes on.......... Truly speaking, you can't draw comparison. Hao walikuwa moto wa kuotea mbali.
 


Wewe ndio mwanasoka halisi unaejua nini maana ya soka,,,na sio shabiki kama wengine,walioanza kuangalia mpira miaka mitano nyuma
 


Uzuri hakuna alieweza kopy soka la diego na Messi tokea dunia iumbwe.
 
Walishindanishwa wapi? Jifunze kumkubali mtu anayejua hata km humpendi, achana na siasa kt football, mpira wa miguu sio maneno zinaongea takwimu mkuu.. acha porojo. Mi binafsi smpendi Messi ila nakubali kwa kipind hiki hakuna kama yeye katika soka
Anayebisha kuhusu hii documentary ya Pele atakuwa na matatizo maana aliyeitengeneza ame compare na kucontrast. Pele yupo juu mno. Wengine wanacopy tu kwake.
 
Naunga mkono hoja
 
Kwa hiyo Shwarzineger,Stallone nk walikuwa kweli na uwezo wa kupiga jeshi Zima?
 
Naweza kusema maamuzi hayo yametawaliwa zaidi na fikra za kibaguzi hasa ubaguzi wa rangi japo ukweli utabaki palepale kwamba ktk dunia hii hakuna mchezaji wa kuweza kufikia kiwango cha Pele.

Pele aliiwezesha Brazil kutwaa kombe la dunia kwa mara ya kwanza 1958 nchini Sweden akiwa ndiye mchezaji mdogo kabisa, miaka 17 tu na akiibuka mfungaji bora.

Mwaka 1962 tena kwa msaada mkubwa wa Pele wakatwaa tena kombe, mwaka 1966 Brazil hawakufaulu kutetea taji baada ya Pele kuumizwa na wareno kwenye robo fainali na hivyo Brazil kutolewa.

Mwaka 1970 kule Mexico Pele akaiongoza Brazil kutwaa taji la tatu na hapo ndipo akatangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa baada ya wachezaji wa timu pinzani kuzidi kumchezea rafu za makusudi na wakati ule mastaa walikuwa hawalindwi kama ilivyo leo.

Toka Pele alipostaafu kuchezea timu ya taifa ya Brazil 1970, timu hiyo ilisahau hilo kombe la dunia kwa miaka 24 hali inayoonyesha alivyokuwa "Power House" ktk timu hiyo.

Wakati mnapoongelea wachezaji bora duniani muwe mnamuweka Pele kando kwa sababu hakuwa mchezaji wa kawaida alikuwa ni "The greatest soccer legend of the all time ever emerged on this planet."
 
Nimetazama clip na nimetazama clip zingine za Pele. Labda niulize tena, tunamcompare Pele dhidi Messi na Ronaldo kwa vipengele vipi?

Wachezaji wana vipengele vingi, vikiwemo dribbling, ball controll, vision, streght, stamina, sprint, finishing n.k mpaka sasa bado dunia haijamshuhudia mchezaji aliyekamilika kwa nyanja zote hapo juu, kuna vitu atakuwa navyo na kuna hatoweza kuwa navyo.

Mfano Ronaldo hana ball controll na skills kubwa kulinganisha na Neymar. Xavi ana vision kubwa kuliko Gerald. Iniesta ana vision na skillz kuliko Lampard, hakuna mchezaji alokamilika, huo ndo mpira.

Sasa tunapokuja kusema fulani ni bora kuliko fulani, basi tunatazama vipengele vyote hapo juu jinsi mchezaji anavyovifanya ndani ya uwanja.

KWA KUTAZAMA HIVYO, YAANI UBORA WA MCHEZAJI NDANI YA PITCH, HAJAWAHI KUTOKEA KAMA MESSI.

Huwezi linganisha maisha ya miaka 70 nyuma na maisha ya sasa. Mpira una mabadiliko mengi mno hasa shule, wachezaji wote sasa hivi wanafundishwa how to attach and how to defend. Pele angecheza kwa kizazi hiki, huenda angekutana na upinzani mkubwa kutokana na soka la sasa lilivyo.

Messi anakupa kila kitu ndani ya pitch, hasa matokeo. Ukitaka kuamini nachosema, kawasikilize akina Wenger waliomtazama Pele, kawasikilize akina Anceloti, Diego, Mourinho kisha watakwambia Who is Messi? Wote hawa wanakiri hakuna mchezaji bora aliyewahi kucheza mpira kwa level za juu kama Messi.

Sasa tujiulize watu kama akina Wenger, Guardiola, Anceloti, Diego Simeone, Sir Alex n.k wanaweza wakawa na chuki na Pele? Bado tunaamini kuwa hawampendi kisa ngozi yake? Yaleyale ya Okocha ni alikuwa bora kuliko yoyote ila alkataliwa sababu ya rangi, wakati huohuo Gaucho ni rangi hiyohiyo vilevile.

Kama umemshuhudia Messi, You ar Lucky.
 
Kama wasema hivyo Ronaldinho?
 
Mbona kashindwa kuwapa PSG au PSG wanachezea chumbani?
 
Kuna mahali sir Alex alisema Messi ni bora mbele ya Ronaldo au Pele au umeleta upotoshaji tu?
 
Gaucho sio mweusi bwana wewe vipi. Gaucho ni Red Indian (American Indian)
 
Kwangu mimi mchezaji bora wa muda wote ni Ronaldinho.
Huyu mwamba ndie aliefanya mpira kwangu ukawa ni starehe/burudani kuliko kitu kingine chochote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…