Kwa hali hii, Mmarekani hana mpinzani wadau: jiandaeni tu kuolewa!

Kwa hali hii, Mmarekani hana mpinzani wadau: jiandaeni tu kuolewa!

NIMEONA

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2019
Posts
3,862
Reaction score
5,693
Yanayoendelea huko Ukraine na Russia nilifikiri ni mihemko na ujuaji mwingi tu wa wabongo.......kumbe ni kweli mzee mzima putin anakutana na wakati mgumu;

Vyombo vyote ninavyoangalia sasa, hata vile visivyo rafiki wa marekani, vinatangaza tu sasa kuyumba kwa urusi.

Nikikumbuka jinsi dunia 'yetu sisi wengine' ilivyokuwa inamuogopa putin hadi akawa anaitwa 'the most powerful person in the world', nachoka kabisa.

Nikifikiria jinsi 'babu' Joe Biden alivyokuwa anaongea huku anasinzia kuhusu nini wanaenda kuifanyia Russia, nilikuwa nacheka tu kipindi kile kwa kudhani kuwa hawa marekani wameishiwa. Leo yanatimia yaleyale aliyoyaongea 'the sleepy' Joe.

Nikifikiria jinsi nchi za ulaya zilivyoamrishwa na marekani kukata mahusiano haraka na urusi nilishangaa sana kwanini zote zinafuata tu hata zile zinazoathirika moja kwa moja kwenye uchumi wake; kumbe walijua aisee nini kingewapata kama wangeenda against. Aisee tumwache tu mmarekani aitwe mmarekani!!

Nikiangalia yaliyomkuta macho madogo mchina, ya kupelekewa vifaa vya kijeshi barazani kwake huku akiwa anafokafoka tu asijue la kufanya, nimechoka. Ikumbukwe kuwa, kama ilivyo kwa mrusi, mchina nae alikuwa anatukuzwa mno humu.

Lakini kumbukumbu zangu kama ziko sawa, nakumbuka mwaka fulani kama sio 2001 basi 2002 marekani hii iliwahi kuiingia ndege yake ya kijeshi huko anga la China.

China akatuma ndege na yeye kwenda kuifukuzia, kilichotokea ziligongana zile ndege na ya China kuanguka huku askari wake kadhaa wakifariki huku ile ya marekani ikipata hitilafu na wakaishia kukamatwa.

Mgogoro ulikuwa mkubwa wa kutaka kuachiwa hao askari lakini mwishowe mchina aliufyata na kuwaachia hao makomandoo.

Walipokelewa kwa sherehe kubwa sana na Bush. Miaka 20 baadae leo, nilijua mchina ameshajidhatiti vya kutosha kuweza kumkabili mmarekani kumbe wapi!!! Tumwache tu mmarekani aitwe mmarekani!

Kwa hali hii, na kwakuwa huyu mtemi anahusudu na kupambania ndoa za jinsia moja; wadau jiandaeni tu kuolewa!!
 
Yanayoendelea huko Ukraine na Russia nilifikiri ni mihemko na ujuaji mwingi tu wa wabongo.......kumbe ni kweli mzee mzima putin anakutana na wakati mgumu;
- vyombo vyote ninavyoangalia sasa, hata vile visivyo rafiki wa marekani, vinatangaza tu sasa kuyumba kwa urusi.
-Nikikumbuka jinsi dunia 'yetu sisi wengine' ilivyokuwa inamuogopa putin hadi akawa anaitwa 'the most powerful person in the world', nachoka kabisa.
-Nikifikiria jinsi 'babu' Joe Biden alivyokuwa anaongea huku anasinzia kuhusu nini wanaenda kuifanyia Russia, nilikuwa nacheka tu kipindi kile kwa kudhani kuwa hawa marekani wameishiwa. Leo yanatimia yaleyale aliyoyaongea 'the sleepy' Joe.
-Nikifikiria jinsi nchi za ulaya zilivyoamrishwa na marekani kukata mahusiano haraka na urusi nilishangaa sana kwanini zote zinafuata tu hata zile zinazoathirika moja kwa moja kwenye uchumi wake; kumbe walijua aisee nini kingewapata kama wangeenda against. Aisee tumwache tu mmarekani aitwe mmarekani!!

Nikiangalia yaliyomkuta macho madogo mchina, ya kupelekewa vifaa vya kijeshi barazani kwake huku akiwa anafokafoka tu asijue la kufanya, nimechoka. Ikumbukwe kuwa, kama ilivyo kwa mrusi, mchina nae alikuwa anatukuzwa mno humu. Lakini kumbukumbu zangu kama ziko sawa, nakumbuka mwaka fulani kama sio 2001 basi 2002 marekani hii iliwahi kuiingia ndege yake ya kijeshi huko anga la China. China akatuma ndege na yeye kwenda kuifukuzia, kilichotokea ziligongana zile ndege na ya China kuanguka huku askari wake kadhaa wakifariki huku ile ya marekani ikipata hitilafu na wakaishia kukamatwa. Mgogoro ulikuwa mkubwa wa kutaka kuachiwa hao askari lakini mwishowe mchina aliufyata na kuwaachia hao makomandoo. Walipokelewa kwa sherehe kubwa sana na Bush. Miaka 20 baadae leo, nilijua mchina ameshajidhatiti vya kutosha kuweza kumkabili mmarekani kumbe wapi!!! Tumwache tu mmarekani aitwe mmarekani!

Kwa hali hii, na kwakuwa huyu mtemi anahusudu na kupambania ndoa za jinsia moja; wadau jiandaeni tu kuolewa!!
Utaolewa wewe na babako nyumbu wahed!
 
Vita sio 'kidali poo'...kuna kusukuma na kusukumwa pia(Vuta nikuvute).

Russia kuachia hiyo miji haina maana ya moja kwa moja kwamba ameshindwa. Kuna kuiachia kimkakati.

Btw, kumbuka mrusi anapigana na NATO sio Ukraine/Marekani pekee.
 
Nasema tena hii nchi kuna mashoga wengi sasa hivi wameamua kujitokeza hadharani bila kificho oneni uyu nae anataka kuolewa dah 🤣🤣🙌
 
Niliwahi sema huko nyuma hasa baada ya kusoma waraka wa siri, wa NATU,Kwa kuwa mrusi ndio aliyeanza watahakikisha wanapigana vita vya muda mrefu wakiamini watamchosha babu Putin na malengo yanakwenda kutimia mwishowe atachoka tu na kukata pumzi hilo litakapotimia "tutaivunja vunja urusi.
 
Nasema tena hii nchi kuna mashoga wengi sasa hivi wameamua kujitokeza hadharani bila kificho oneni uyu nae anataka kuolewa dah 🤣🤣🙌
Ulibahatika kufika angalau kidato cha tatu ndugu ambako kidogo tunatambulishwa somo la literature?!!!
 
Vita sio 'kidali poo'...kuna kusukuma na kusukumwa pia(Vuta nikuvute).

Russia kuachia hiyo miji haina maana ya moja kwa moja kwamba ameshindwa. Kuna kuiachia kimkakati.

Btw, kumbuka mrusi anapigana na NATO sio Ukraine/Marekani pekee.
Ni kweli lakini kwa usuper power wake ilitakiwa awe ameshamfyekelea mbali, no matter what
 
Bado Putin yupo imara sana nchi zote za magharibi zinatoa siraha mafunzo na wapiganaji lakini wameshindwa kuchukua udhibiti wa nchi mpaka leo
Yeye mrus ndiye aliyeshindwa kwasababu yeye ndiye alieifwata ukrein.kwahiyo alipaswa awe kajiandaa sawasawa.sasa ni zaidi ya miezi 6 kashindwa kufanya hivyo.
 
Vita sio 'kidali poo'...kuna kusukuma na kusukumwa pia(Vuta nikuvute).

Russia kuachia hiyo miji haina maana ya moja kwa moja kwamba ameshindwa. Kuna kuiachia kimkakati.

Btw, kumbuka mrusi anapigana na NATO sio Ukraine/Marekani pekee.
Imekuaje tena Nato wakaingia wakati putin alipiga mkwara kua atakayekanyaga mguu kuisaidia ukrein atamfumua.Au ulikua mkwara mbuzi.
 
Mleta uzi mjinga sana, inaonyesha ulishachumbiwa tayari hapa unazuga tu
 
Niliwahi sema huko nyuma hasa baada ya kusoma waraka wa siri, wa NATU,Kwa kuwa mrusi ndio aliyeanza watahakikisha wanapigana vita vya muda mrefu wakiamini watamchosha babu Putin na malengo yanakwenda kutimia mwishowe atachoka tu na kukata pumzi hilo litakapotimia "tutaivunja vunja urusi.
Hii mbinu inaweza ikafanikiwa kwa kiasi kikubwa kwasababu najua hata mrusi mwenyewe aamini hii vita ingeweza kuchukua zaidi ya miezi 6 sasa.alafu wenzake shughuli zao zinaendelea kama kawaida.Sasa hivi kabakia kutishia tishia mambo ya gas bila kujua ndo anafilisika ivyo.
 
Yanayoendelea huko Ukraine na Russia nilifikiri ni mihemko na ujuaji mwingi tu wa wabongo.......kumbe ni kweli mzee mzima putin anakutana na wakati mgumu;
- vyombo vyote ninavyoangalia sasa, hata vile visivyo rafiki wa marekani, vinatangaza tu sasa kuyumba kwa urusi.
-Nikikumbuka jinsi dunia 'yetu sisi wengine' ilivyokuwa inamuogopa putin hadi akawa anaitwa 'the most powerful person in the world', nachoka kabisa.
-Nikifikiria jinsi 'babu' Joe Biden alivyokuwa anaongea huku anasinzia kuhusu nini wanaenda kuifanyia Russia, nilikuwa nacheka tu kipindi kile kwa kudhani kuwa hawa marekani wameishiwa. Leo yanatimia yaleyale aliyoyaongea 'the sleepy' Joe.
-Nikifikiria jinsi nchi za ulaya zilivyoamrishwa na marekani kukata mahusiano haraka na urusi nilishangaa sana kwanini zote zinafuata tu hata zile zinazoathirika moja kwa moja kwenye uchumi wake; kumbe walijua aisee nini kingewapata kama wangeenda against. Aisee tumwache tu mmarekani aitwe mmarekani!!

Nikiangalia yaliyomkuta macho madogo mchina, ya kupelekewa vifaa vya kijeshi barazani kwake huku akiwa anafokafoka tu asijue la kufanya, nimechoka. Ikumbukwe kuwa, kama ilivyo kwa mrusi, mchina nae alikuwa anatukuzwa mno humu. Lakini kumbukumbu zangu kama ziko sawa, nakumbuka mwaka fulani kama sio 2001 basi 2002 marekani hii iliwahi kuiingia ndege yake ya kijeshi huko anga la China. China akatuma ndege na yeye kwenda kuifukuzia, kilichotokea ziligongana zile ndege na ya China kuanguka huku askari wake kadhaa wakifariki huku ile ya marekani ikipata hitilafu na wakaishia kukamatwa. Mgogoro ulikuwa mkubwa wa kutaka kuachiwa hao askari lakini mwishowe mchina aliufyata na kuwaachia hao makomandoo. Walipokelewa kwa sherehe kubwa sana na Bush. Miaka 20 baadae leo, nilijua mchina ameshajidhatiti vya kutosha kuweza kumkabili mmarekani kumbe wapi!!! Tumwache tu mmarekani aitwe mmarekani!

Kwa hali hii, na kwakuwa huyu mtemi anahusudu na kupambania ndoa za jinsia moja; wadau jiandaeni tu kuolewa!!
Hahahahaaaa
 
Back
Top Bottom