Kwa hali ilivyo, unamshauri nini Luhaga Mpina mbunge wa Jimbo la Kisesa CCM?

Kwa hali ilivyo, unamshauri nini Luhaga Mpina mbunge wa Jimbo la Kisesa CCM?

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
kama mdau wa siasa, harakati na demokrasia nchini,

ni upi ushauri wako muafaka kwa kiongozi huyo wa kisiasa, kulingana na joto na uelekeo wa siasa za Tanzania, kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa baadae mwaka huu2024, na ule uchaguzi mkuu wa mwaka ujao 2025?

afanye nini, aamue nini, na achukue uelekeo gani kisiasa kwa unavyoona 🐒
 
kama mdau wa siasa, harakati na demokrasia nchini,

ni upi ushauri wako muafaka kwa kiongozi huyo wa kisiasa, kulingana na joto na uelekeo wa siasa za Tanzania, kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa baadae mwaka huu2024, na ule uchaguzi mkuu wa mwaka ujao 2025?

afanye nini, aamue nini, na achukue uelekeo gani kisiasa kwa unavyoona 🐒
aachane na ccm maana haindani na kasi yakwe
 
kama mdau wa siasa, harakati na demokrasia nchini,

ni upi ushauri wako muafaka kwa kiongozi huyo wa kisiasa, kulingana na joto na uelekeo wa siasa za Tanzania, kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa baadae mwaka huu2024, na ule uchaguzi mkuu wa mwaka ujao 2025?

afanye nini, aamue nini, na achukue uelekeo gani kisiasa kwa unavyoona 🐒
Kulipia mabomu kama Mrema na Slaa hakutomfikisha popote, awaulize waliishia wapi.
 
Ninachomshauri huyu mzalendo wa Nchi aliyebaki peke yake ni kuwa,1 aedelee kuwapiga supana Hawa Wala rushwa Kwa kuitisha mkutano na kuongea na wananchi wake ili wananchi wake tuyajue haya madudu ya hawa mafisadi kama haya ya sukari na mengineyo mengi na tuchukue hatua ya kuwaondoa madarakani hata Kwa coup d'etat
 
Ninachomshauri huyu mzalendo wa Nchi aliyebaki peke yake ni kuwa,1 aedelee kuwapiga supana Hawa Wala rushwa Kwa kuitisha mkutano na kuongea na wananchi wake ili wananchi wake tuyajue haya madudu ya hawa mafisadi kama haya ya sukari na mengineyo mengi na tuchukue hatua ya kuwaondoa madarakani hata Kwa coup d'etat
ushauri mzuri sana na wakijasiri kisiasa, japo lugha ulotumia ni ya rika moja tu kuielewa bila utata...

ila hitimisho linachekesha 🤣
 
Kama kayaweka wazi yale kiuzalendo na sio kiunafki , azidi kusongo mbele wala asitishwe na chochote , sisi wananchi tunapenda viongozi wa aina yake na sio hawa wa kusifu na kuabudu kwa kila kitu .
Yes,
hapo ndio penyewe, ushauri wa mujarabu kabisaa kisiasa 🐒
 
kama mdau wa siasa, harakati na demokrasia nchini,

ni upi ushauri wako muafaka kwa kiongozi huyo wa kisiasa, kulingana na joto na uelekeo wa siasa za Tanzania, kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa baadae mwaka huu2024, na ule uchaguzi mkuu wa mwaka ujao 2025?

afanye nini, aamue nini, na achukue uelekeo gani kisiasa kwa unavyoona 🐒
Asiwe na wasiwasi, abaki CCM hata Mzindakaya hakuwahi kutoka CCM. Hapaswi kuyakimbia Manyang’au
 
Namshauri kama anaamini uganga basi mganga wake amlipe vzr ili aendelee kumkinga na mabomu ya kichawi toka pande zote nne za nchi...
 
Mkuu usipo jihusisha na harakati za kichawa utakuja kuwa bonge la kiongozi , kwa sababu tu ni muelewa na hauna ego za kijinga .
Gentleman,
Bila Neema na Baraka za Mungu ni vigumu kudumu kwa uhakika, amani, utulivu na upendo mahali Fulani popote ulipo, iwe kazini, masomoni, michezoni, siasani, uongozini na mahali pengine kokote...

nikuhakikishie tu,
binafsi kwa kudra za Mungu mpaka hapa nilipo ni bonge la kiongozi 🤣

kwasababu isingekua hivyo, mwanainchi gani angeniskiza, msomi gani angenisoma hata humu JF tu, nani angethubutu kufollow account yangu na kunicheck inbox kwa mashauriano, urafiki na salamu?

kwa Imani yangu kwa Mungu, uelewa na ufahamu wangu kidogo mathalani kuhusu siasa na uongozi sina hakika kama kuna ninae muona adui, ispokua labda yeye huyo mwanasiasa mwingine ndio anione mimi adui yake....

binafsi naamini,
siasa ni ushindani tu wa mawazo, fikra mipango, mbinu, ubunifu bora zaidi ya mwingine, wa kuleta au kuchochewa, mageuzi au mabadiliko chanya ya kijamii kisiasa na kiuchumi miongoni mwa jamii fulani...

na duniani, uchaguzi huamua nani au yupi kupitia ilani na sera kua ni bora zaidi ya mwingine...

so,
kwa siasa za Tanzania sijamuona adui yangu bado, bali namuona mshindani ambae pia ni ndugu, jirani, jamaa, rafiki, baba na mama yangu.

afanye siasa zake kwa uhuru nami zangu kwa amani lakini mwisho wa siku udugu wetu uwe Imara zaidi kati hali zote za shida na raha....

nimeeleza kwa kirefu hivi, ili kuondoa hofu na huenda kama kuna sintofahamu au utata dhidi ya siasa na hoja zangu kisiasa humu ndani 🐒
 
Back
Top Bottom