Kwa hali niliyoiona sitashawishika tena kupima UKIMWI

Umakini unahitajika usimpime mtu kwa macho hakuna kitu kizuri kama kuwa na afya bora ngwengwe ipo tusirahisishe,huwa nawashangaa sana watu wanavojifariji eti bora nipate ukimwi ntatumia doz nitasogeza siku kulko cancer au kisukari..ukimwi bado ni hatari tuwe makini hakuna kitu kibaya katika maisha kama kuishi kwa matumaini.
 
Tena kama una mkono wa sweta hauchelewi .....!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole saana mkuu,
 
Mkuu wiki iliyopita tumemzika baba mdogo wangu baada ya kuishi na mwanamke miaka sita kumbe kaathirika pasipo yeye kujua. Alipoenda hospitali kupima alifariki siku ya pili baada ya majibu kutoka tena bila hata kupungua mwili.
 
Nakumbuka wakati nipo Chuo kuna jamaa aliulizwa unasoma wapi na mwaka wa ngapi? Alivyojibu tu ni finalist Dr akamuuliza kwa nini unapima, akasema nataka tu kujua Afya yangu akajibiwa rudi Chuo ukasome ukishamaliza ndio upime.
 
Sasa usipopima utajuaje hali yako kijana?

Pima uishi kwa amani, maana kama utakuwa negative itakufanya uwe makini na uache kabisa kudinyana dinyana kusiko na mpango...
Bora kutojua kama ninao hata kama nikiwa nao kwakuwa itanipunguzia hata speed ya utafutaji wa maisha kwa kujiona kuwa ni waleo wa kesho na kukube besha dhambi nyingne ya kutokula kwa jasho lako kama neno la mungu lisemavyo na kupunguza komborela za kikubwa japo kuupata ni ktk njia nyingi tofauti.
"Bora kuondoka ukiwa unajua kuliko kujua kuwa unaondoka"
 
Asante saana mkuu kwa kuelimisha jamii kwa ujumla na pole sana tatito wabongo siku hizi wakiona kalio tuu wanadata kumbe ni umeme.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…