MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,018
- 16,802
Yeye kama Waziri tokea Mchakato mzima wa Uwekezaji wa Klabu ya Simba alikuwepo, alihusishwa na natambua huku nikiwa na uhakika kuwa mara nyingi kama Waziri alikuwa anakuwa Consulted na akawa anabariki yaliyokuwa yakiendelea na mpaka Siku ya mwisho ya Maamuzi ambayo yalifanywa na Wanachama huku Yeye akiwa Mgeni rasmi alibariki Uwekezaji wa Mo Dewji wa 49% ndani ya Simba SC hatimaye leo tena huyo huyo Waziri anageuka na kutaka kuleta Mtafaruku na matatizo ndani ya Klabu ya Simba.
Kama kuna Watanzania ambao wanaziaibisha PhD's walizonazo Wasomi wengine basi ni huyu Waziri Mwakyembe na nadhani kama anaweza atuombe Radhi upesi wana Simba SC kwani Kauli yake imetuchanganya na imetukwaza mno tu. Na kwa upande wa Serikali watambue kuwa kama kuna Timu ambazo zinaamua pia Rais wa nchi hii awe nani basi ni Wapenzi na Wanachama wa hii Timu hivyo kuna uwezekano mkubwa Kauli hii ya Kipumbavu ya Waziri Mwakyembe ikawa na Athari kubwa Kwao Kisiasa na wakajuta huku wakiwa hawaamini kitakachotokea.
Hivi ni kwanini Serikali ya Awamu hii tokea Kutekwa na Kupatikana kwa Mwekezaji wa Simba SC Mo Dewji mmeanza Kuonyesha Chuki zenu za wazi wazi Kwake huku mkiwakumbatia kwa ukaribu mno Maadui zake wa Kibiashara? Mo Dewji wa Watu amewakoseeni nini? Hivi hizi Juhudi zake anazozifanya kwa Simba SC nyie hamuoni kuwa anailetea nchi Sifa lakini pia anaunda Fursa kadhaa za Kiajira kwa Watanzania hivyo Kuwapunguzieni mzigo mkubwa wa Tatizo la Ajira ambalo linawashindeni kila Siku hapa nchini?
Na kama mnajua fika kuwa sasa hamumpendi tena Mo Dewji labda mna Hasira nae pengine kwakuwa amekataa Kuchangia Kitu fulani Kwenu huku mzikidi Kumfilsi Mali zake huko Tanga na Kumkomoa kwa hapa na pale kwanini msimwambie tu wazi wazi bila Unafiki kuwa hamumtaki ili awaachie Simba SC hao Wafanyabishara wenu ambao huwa mnawatisha hadi wanawalambeni Miguu ili wawasaidie kwa Pesa ili muendelee Kutawala na kuwa Madarakani?
Kwa mfano kwa aina ya Uwekezaji mkubwa hasa wa Kiufadhili ambao tayari Mo Dewji ameshaanza Kuuweka ndani ya Simba SC leo hii akiamua Kujitoa na Kuachana na Simba SC nyie ( Serikali ) hasa kupitia Waziri Mwakyembe mtakuwa na uwezo wa Kulipa Mishahara Wachezaji na Watendaji wengine wa Simba SC na Kuendesha Operations za Klabu? Kwanini mnapenda Kuliangalia Jambo hili kwa upeo Wenu mfupi mlionao japo wengi wenu mnajifanya mna PhD's wakati kumbe ni za hovyo hovyo, Feki na bado mnaonyesha tu Upumbavu wenu?
Mwisho kabisa naomba leo niwaambie wana Simba SC japo najua wengi wenu mlikuwa hamjui kwamba kama kuna Jasusi ambaye anatumika na Waziri husika ( kwa Uratibu mzima wa Serikali ) ili Kuipeleleza Simba SC na kuhakikisha kuwa Mwekezaji Mo Dewji anasumbuliwa hadi akate Tamaa kuwa Mwekezaji wa Simba SC ni Ndugu Ismail Aden Rage na labda niwaombe tu wana Simba hasa Mwekezaji, Mwenyekiti na Bodi nzima ya Wadhamini na Uongozi mzima wa Simba SC wawe nae makini sana na ikiwezekana wamuepuke kwani Ismail Aden Rage ndiyo Kirusi katika Kufanikisha Mo Dewji anafanikiwa na ndiyo huyu huyu yupo nyuma ya Mzee Kilomoni ili hatimaye wote hawa wakishafanikiwa basi Tajiri Mmoja mkubwa nchini Tanzania ( aliyefiwa na Watumishi wake hivi karibuni ) anayewatumia ( anayependwa pia na Serikali ) mwenye Kuitaka sana Simba SC afanikiwe na Wao waule.
Waziri Mwakyembe awe makini na asije Kutulaumu wana Simba SC kama na Sisi tukisema liwalo na liwe Kwake. Tumemchoka!
Kama kuna Watanzania ambao wanaziaibisha PhD's walizonazo Wasomi wengine basi ni huyu Waziri Mwakyembe na nadhani kama anaweza atuombe Radhi upesi wana Simba SC kwani Kauli yake imetuchanganya na imetukwaza mno tu. Na kwa upande wa Serikali watambue kuwa kama kuna Timu ambazo zinaamua pia Rais wa nchi hii awe nani basi ni Wapenzi na Wanachama wa hii Timu hivyo kuna uwezekano mkubwa Kauli hii ya Kipumbavu ya Waziri Mwakyembe ikawa na Athari kubwa Kwao Kisiasa na wakajuta huku wakiwa hawaamini kitakachotokea.
Hivi ni kwanini Serikali ya Awamu hii tokea Kutekwa na Kupatikana kwa Mwekezaji wa Simba SC Mo Dewji mmeanza Kuonyesha Chuki zenu za wazi wazi Kwake huku mkiwakumbatia kwa ukaribu mno Maadui zake wa Kibiashara? Mo Dewji wa Watu amewakoseeni nini? Hivi hizi Juhudi zake anazozifanya kwa Simba SC nyie hamuoni kuwa anailetea nchi Sifa lakini pia anaunda Fursa kadhaa za Kiajira kwa Watanzania hivyo Kuwapunguzieni mzigo mkubwa wa Tatizo la Ajira ambalo linawashindeni kila Siku hapa nchini?
Na kama mnajua fika kuwa sasa hamumpendi tena Mo Dewji labda mna Hasira nae pengine kwakuwa amekataa Kuchangia Kitu fulani Kwenu huku mzikidi Kumfilsi Mali zake huko Tanga na Kumkomoa kwa hapa na pale kwanini msimwambie tu wazi wazi bila Unafiki kuwa hamumtaki ili awaachie Simba SC hao Wafanyabishara wenu ambao huwa mnawatisha hadi wanawalambeni Miguu ili wawasaidie kwa Pesa ili muendelee Kutawala na kuwa Madarakani?
Kwa mfano kwa aina ya Uwekezaji mkubwa hasa wa Kiufadhili ambao tayari Mo Dewji ameshaanza Kuuweka ndani ya Simba SC leo hii akiamua Kujitoa na Kuachana na Simba SC nyie ( Serikali ) hasa kupitia Waziri Mwakyembe mtakuwa na uwezo wa Kulipa Mishahara Wachezaji na Watendaji wengine wa Simba SC na Kuendesha Operations za Klabu? Kwanini mnapenda Kuliangalia Jambo hili kwa upeo Wenu mfupi mlionao japo wengi wenu mnajifanya mna PhD's wakati kumbe ni za hovyo hovyo, Feki na bado mnaonyesha tu Upumbavu wenu?
Mwisho kabisa naomba leo niwaambie wana Simba SC japo najua wengi wenu mlikuwa hamjui kwamba kama kuna Jasusi ambaye anatumika na Waziri husika ( kwa Uratibu mzima wa Serikali ) ili Kuipeleleza Simba SC na kuhakikisha kuwa Mwekezaji Mo Dewji anasumbuliwa hadi akate Tamaa kuwa Mwekezaji wa Simba SC ni Ndugu Ismail Aden Rage na labda niwaombe tu wana Simba hasa Mwekezaji, Mwenyekiti na Bodi nzima ya Wadhamini na Uongozi mzima wa Simba SC wawe nae makini sana na ikiwezekana wamuepuke kwani Ismail Aden Rage ndiyo Kirusi katika Kufanikisha Mo Dewji anafanikiwa na ndiyo huyu huyu yupo nyuma ya Mzee Kilomoni ili hatimaye wote hawa wakishafanikiwa basi Tajiri Mmoja mkubwa nchini Tanzania ( aliyefiwa na Watumishi wake hivi karibuni ) anayewatumia ( anayependwa pia na Serikali ) mwenye Kuitaka sana Simba SC afanikiwe na Wao waule.
Waziri Mwakyembe awe makini na asije Kutulaumu wana Simba SC kama na Sisi tukisema liwalo na liwe Kwake. Tumemchoka!