Kwa hili la kuagiza Umeme Ethiopia, wananchi tunahitaji maelezo ya ziada, tulijenga mitambo ya bwawa la Mwalimu kwa nini?

Kwa hili la kuagiza Umeme Ethiopia, wananchi tunahitaji maelezo ya ziada, tulijenga mitambo ya bwawa la Mwalimu kwa nini?

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
1741686519506.png

Mimi ni mmoja wa watu nisioridhika na maelezo yaliyotolewa na serikali kupitia kwa Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati ndg Felchesmi Mramba, juu ya sababu za kuagiza umeme toka Ethiopia.

Sababu zilizotolewa;
  • Umeme wa mikoa ya kaskazini unapelea au kukosekana kabisa
  • Kukosekana kwa umeme huko kunatookana na umbali kutoka sehemu za uzalishaji umeme, yaani Dar esalaam, kwa umeme kutokana na mitambo ya gesi, na umeme toka Mkoa wa Pwani/Morogroro toka Bwawa la Mwalimu Nyerere
  • Mikoa ya kaskazini inakosa umeme wa uhakika na kupungua sana kwa msongo(voltage)
  • Serikali itaagiza umeme wa 100MW, ili kurekebisha matatizo Moshi, Arusha na Manyara, na kwa kufanya hivyo Songwe itaweza kupata 17MW
Bhati mbaya haya maelezo hayakidhi.
Najiuliza maswali yafuatayo,
  • Je, kuna ukosefu wa Power production? jibu ni hapana kwani sasa hivi umeme unaozalishwa nchini 3,796MW, wakati mahitaji ni 2,200MW(Bwawa la Mwalimu Nyerere bado halijatenngeneza umeme at full caoacity)
  • Katika ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere hapakuwepo Feasibility study? Study ambayo ingeweza kuona jinsi ya kusambaza umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere sehemu zote za nchi?
  • Na je, ni mikakati gani itatumiwa na serikali kuona kwamba umeme wetu unaozaliwa Bwawa la Mwalimu Nyerere unatumika kikamilifu?
  • Na je huko Ethiopia, si tunalipa kwa fedha za kigeni? Hizo gharama si zingetumika kusafirisha na kusambaza umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere

Wananchi tunajiuliza haya maswali mengi maana tunajua mradi wa ujenzi wa umeme wa Bwawa la Mwalimi Nyerere umetugharimu sana, tena sana, kiasi cha karibia Trillioni 7, fedha za kitanzania.

Swali linalotukatisha tamaa, ni je hizo Trillioni 7 za Bwawa la Mwalimu Nyerer ni wasted investment?

Tupate ufafanuzi tafadhali!!
 
View attachment 3266577
Mimi ni mmoja wa watu nisioridhika na maelezo yaliyotolewa na serikali kupitia kwa Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati ndg Felchesmi Mramba, juu ya sababu za kuagiza umeme toka Ethiopia.

Sababu zilizotolewa;
  • Umeme wa mikoa ya kaskazini unapelea au kukosekana kabisa
  • Kukosekana kwa umeme huko kunatookana na umbali kutoka sehemu za uzalishaji umeme, yaani Dar esalaam, kwa umeme kutokana na mitambo ya gesi, na umeme toka Mkoa wa Pwani/Morogroro toka Bwawa la Mwalimu Nyerere
  • Mikoa ya kaskazini inakosa umeme wa uhakika na kupungua sana kwa msongo(voltage)
  • Serikali itaagiza umeme wa 100MW, ili kurekebisha matatizo Moshi, Arusha na Manyara, na kwa kufanya hivyo Songwe itaweza kupata 17MW
Bhati mbaya haya maelezo hayakidhi.
Najiuliza maswali yafuatayo,
  • Je, kuna ukosefu wa Power production? jibu ni hapana kwani sasa hivi umeme unaozalishwa nchini 3,796MW, wakati mahitaji ni 2,200MW(Bwawa la Mwalimu Nyerere bado halijatenngeneza umeme at full caoacity)
  • Katika ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere hapakuwepo Feasibility study? Study ambayo ingeweza kuona jinsi ya kusambaza umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere sehemu zote za nchi?
  • Na je, ni mikakati gani itatumiwa na serikali kuona kwamba umeme wetu unaozaliwa Bwawa la Mwalimu Nyerere unatumika kikamilifu?
  • Na je huko Ethiopia, si tunalipa kwa fedha za kigeni? Hizo gharama si zingetumika kusafirisha na kusambaza umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere

Wananchi tunajiuliza haya maswali mengi maana tunajua mradi wa ujenzi wa umeme wa Bwawa la Mwalimi Nyerere umetugharimu sana, tena sana, kiasi cha karibia Trillioni 7, fedha za kitanzania.

Swali linalotukatisha tamaa, ni je hizo Trillioni 7 za Bwawa la Mwalimu Nyerer ni wasted investment?

Tupate ufafanuzi tafadhali!!
Viongozi wa nchi hii Motivation siyo Maendeleo ya nchi. Motivation ni kupiga dili; dili ikishakwisha wanatafuta nyingine. Hii ya bwawa kwisha, hamna dili tena.
 
Namsikiliza Msigwa anahojia Dutch well utumbo mtupu!!

Aibu aibu tupu
Serikali iwatumie wataalam haswa wa masuala ya umeme walitolee ufafanuzi suala hili
Wasiwape wanasiasa,machawa kulizungumzia maana wanaleta taarifa tofauti itakuwa na watu hawaelewi...inawezekana mpango ukawa ni mzuri tu lakini wanavyoufikisha ujumbe ukawa siyo kwa watu

Ova
 
Ujuzi wa kufikiria kwa pamoja kupata kitu kikubwa kilichokamilika kimfumo ni tatizo.

Huwa tuna timu kibao, timu ya wanasiasa mahiri, timu ya mainjinia kabambe, timu ya system analyst wabobezi, timu ya wagavi (suppliers) tajwa, timu ya raia wenye mawazo mapana (JF) n.k

Ila tunawezaje kuchukua kila mawazo ya timu hizi kuyaunganisha kuwa kitu kimoja kukamimilsha jambo kubwa moja endelevu hapo ndipo tumeshindwa.

Kila mtu anavutia kwake na kwenda kivyake mwisho wa siku ndipo tunagundua kumbe kuna wale tuliwaacha na ndiyo maana tunakwama baada ya kukamilisha eneo moja kwa gharama kubwa lakini linaloleta gharama nyingine zaidi kutokana na kukosa ushirikishwaji.

MFANO ENEO LA UMEME TULIKAZANIA UJENZI WA BWAWA BILA USHIRIKISHWAJI, KUTOKANA NA KUWEPO TIMU MAHIRI YA MAINJINIA:

'Timu ya Taifa' ya Wahandisi katika mradi wa Umeme Rufiji​


Mhandisi Robert Kabudi mwenye miaka 20 ya kusimamia miradi mikubwa ya ujenzi nje ya Tanzania pamoja na wahandisi wengine mahiri wazalendo wapo ktk mradi wa ujenzi wa Bwawa la Umeme la Rufiji linatotegemewa kuzalisha 2115 MW wa umeme Tanzania. Mhandisi Robert anaitaja timu hiyo ya watu 21, kikosi anacho kibainisha kama timu ya kutizamwa duniani.


View: https://m.youtube.com/watch?v=f0hbNi7VHhY

Timu hiyo ya wahandisi wa kiTanzania walio na ujuzikazi kwa vitendo, kuna mhandisi aliyepata kusimamia mradi wa kiwanja cha ndege cha Dubai kilichokuwa na bajeti ya zaidi ya US$ 3.5Bn. Miradi mikubwa ya Qatar, Abu Dhabi, Botswana , World Cup Africa Kusini wachezaji wake waTanzania wazalendo walishiriki ktk ujenzi huko ughaibuni.

Wahandisi hao chini ya kitengo cha Tanroads Engineering Consultanting Unit TECU wana kiu ya kuongeza CV zao ktk mradi huu wa Rufiji wenye bajeti kubwa kuliko iliyotumika ktk ujenzi wa Uwanja Mkubwa Mpya wa Ndege Dubai na hivyo si tu kuitambulusha Tanzania bali hata wahandisi wazalendo kwa ulimwengu kukitokea mradi wowote mkubwa nje ya Tanzania
 
Tanzania Bado inahitaji umeme mwingi kuliko uliopo Ili ipate kujikwamua kwa maendeleo ya kiuchumi (viwanda, IT and service sectors ) na kijamii.
Umeme wa Ethiopia utasaidia kusambaza sehemu za kaskazini. Usipo chukua Sasa wapi wengine watauchukua.
Umeme tulionao ni kidogo sana sababu sio taa tu shida yetu. Ukiwa na umeme wa msimamo Fursat nyingi sana zitafunguka.
 
Kawapa na trillioni mbili ya kuboresha miundombinu ya umeme. Leo bado wana hadithi za umeme kupotea njiani.

Yaani ukijumlisha kila kitu alichowafanyia huyo mama inasikitisha sana TANESCO kuwa hapo na bado kutengeneza hasara.

Very sad.
 
Kuna Mramba hapo basi tena tule majani umeme utanunuliwa Ethiopia.
 
Ni GENTAMYASS a.k.a OMOYOGWANE ndiye anaweza akaielewa hii serikali na matendo yake Kwa Kuwa ni PUNGUANI!

Watu wenye akili kubwa kama Mimi ni ngumu kuwaelewa Vibaka tunao ongozwa nao!
Kaka mimi ni mlala hoi wa gamboshi usinifananishe na hao ma braza men wala kiepe wa dasalama
 
Kama yametushinda tuwaite wenyewe kampuni kama SIEMENS waje watuboreshee miundombinu ya Gridi ya Taifa.

Tusione aibu kusema kuwa tumeshindwa.
 
Kila kiongozi anakuja na mpango wake wa kupiga mpunga. Jk na umeme wa gesi, jiwe na mradi wa bwawa, bi mkubwa na umeme wa Ethiopia.
Luwassa na Richmond, dowans
Na Bomba la mafuta kubwa, lile la mkapa lilikua dogo. Kakopa fedha China billioni na billioni dola, na ukisikia zilizofichwa Dubai tu, unachoka Kabisa na ulafi wa viongozi wa nchi hii. Siku hizo Albert, siku hizi Abdul.
 
View attachment 3266577
Mimi ni mmoja wa watu nisioridhika na maelezo yaliyotolewa na serikali kupitia kwa Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati ndg Felchesmi Mramba, juu ya sababu za kuagiza umeme toka Ethiopia.

Sababu zilizotolewa;
  • Umeme wa mikoa ya kaskazini unapelea au kukosekana kabisa
  • Kukosekana kwa umeme huko kunatookana na umbali kutoka sehemu za uzalishaji umeme, yaani Dar esalaam, kwa umeme kutokana na mitambo ya gesi, na umeme toka Mkoa wa Pwani/Morogroro toka Bwawa la Mwalimu Nyerere
  • Mikoa ya kaskazini inakosa umeme wa uhakika na kupungua sana kwa msongo(voltage)
  • Serikali itaagiza umeme wa 100MW, ili kurekebisha matatizo Moshi, Arusha na Manyara, na kwa kufanya hivyo Songwe itaweza kupata 17MW
Bhati mbaya haya maelezo hayakidhi.
Najiuliza maswali yafuatayo,
  • Je, kuna ukosefu wa Power production? jibu ni hapana kwani sasa hivi umeme unaozalishwa nchini 3,796MW, wakati mahitaji ni 2,200MW(Bwawa la Mwalimu Nyerere bado halijatenngeneza umeme at full caoacity)
  • Katika ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere hapakuwepo Feasibility study? Study ambayo ingeweza kuona jinsi ya kusambaza umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere sehemu zote za nchi?
  • Na je, ni mikakati gani itatumiwa na serikali kuona kwamba umeme wetu unaozaliwa Bwawa la Mwalimu Nyerere unatumika kikamilifu?
  • Na je huko Ethiopia, si tunalipa kwa fedha za kigeni? Hizo gharama si zingetumika kusafirisha na kusambaza umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere

Wananchi tunajiuliza haya maswali mengi maana tunajua mradi wa ujenzi wa umeme wa Bwawa la Mwalimi Nyerere umetugharimu sana, tena sana, kiasi cha karibia Trillioni 7, fedha za kitanzania.

Swali linalotukatisha tamaa, ni je hizo Trillioni 7 za Bwawa la Mwalimu Nyerer ni wasted investment?

Tupate ufafanuzi tafadhali!!
Maelezo gani sasa watu wanaangalia 10% wanapiga
 
View attachment 3266577
Mimi ni mmoja wa watu nisioridhika na maelezo yaliyotolewa na serikali kupitia kwa Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati ndg Felchesmi Mramba, juu ya sababu za kuagiza umeme toka Ethiopia.

Sababu zilizotolewa;
  • Umeme wa mikoa ya kaskazini unapelea au kukosekana kabisa
  • Kukosekana kwa umeme huko kunatookana na umbali kutoka sehemu za uzalishaji umeme, yaani Dar esalaam, kwa umeme kutokana na mitambo ya gesi, na umeme toka Mkoa wa Pwani/Morogroro toka Bwawa la Mwalimu Nyerere
  • Mikoa ya kaskazini inakosa umeme wa uhakika na kupungua sana kwa msongo(voltage)
  • Serikali itaagiza umeme wa 100MW, ili kurekebisha matatizo Moshi, Arusha na Manyara, na kwa kufanya hivyo Songwe itaweza kupata 17MW
Bhati mbaya haya maelezo hayakidhi.
Najiuliza maswali yafuatayo,
  • Je, kuna ukosefu wa Power production? jibu ni hapana kwani sasa hivi umeme unaozalishwa nchini 3,796MW, wakati mahitaji ni 2,200MW(Bwawa la Mwalimu Nyerere bado halijatenngeneza umeme at full caoacity)
  • Katika ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere hapakuwepo Feasibility study? Study ambayo ingeweza kuona jinsi ya kusambaza umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere sehemu zote za nchi?
  • Na je, ni mikakati gani itatumiwa na serikali kuona kwamba umeme wetu unaozaliwa Bwawa la Mwalimu Nyerere unatumika kikamilifu?
  • Na je huko Ethiopia, si tunalipa kwa fedha za kigeni? Hizo gharama si zingetumika kusafirisha na kusambaza umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere

Wananchi tunajiuliza haya maswali mengi maana tunajua mradi wa ujenzi wa umeme wa Bwawa la Mwalimi Nyerere umetugharimu sana, tena sana, kiasi cha karibia Trillioni 7, fedha za kitanzania.

Swali linalotukatisha tamaa, ni je hizo Trillioni 7 za Bwawa la Mwalimu Nyerer ni wasted investment?

Tupate ufafanuzi tafadhali!!
Uko sahihi kabisa. Hakuna mtanzania ye yote mwenye akili timamu anayeweza kukubaliana na hizo sababu ya sisi kuanza ku import nishati ya umeme badala ya ku export umeme kama tulivyotarajia baada ya JNHPP kukamilika.

Ziada ya umeme tulionao (baada ya kutoa mahitaji yetu ya sasa) ni zaidi ya MW 2,000. Hao Ethiopia ziada yao haiifiki tuliyonayo sisi. Umeme tunaozalisha kwa mitambo ya maji huko JNHPP, Mtera, Kidatu, Nyumba ya Mungu na kwingineko unazidi mahitaji yetu. Ni umeme safi wa bei nafuu sana. Tulitegemea bei ya umeme ishuke hadi kuwa si zaidi ya Tsh 100 kwa unit kama ilivyokuwa ndoto ya JPM. Hii ingaliwezesha viwanda vyetu viongezeke na kuzalisha bidhaa zenye bei nafuu inayoweza kushindana kwenye masoko ya dunia. Pia ingaliwezesha kuboresha maisha ya watanzania hususani kwenye nishati nafuu ya kupikia na viwanda vidogo vidogo.

Umeme unaozalishwa kwa gesi bei yake ni mara 10 ya ule unaozalishwa kwa maji. Hivyo tulitegemea hiyo mitambo yote ya gesi ya pale Kinyerezi kuzimwa hadi hapo tutakapopata soko la nje la kuwauzia (export) na nchi kupata fedha za kigeni inazozihitaji sana. Na tayari miundo mbinu (njia) ya kupeleka umeme hadi Ethiopia, Kenya na Somalia tumeshaijenga kwa pesa zetu nyingi za kigeni za mikopo. Na sasa tulishaanza kujenga njia nyingine hadi South Africa kupitia Zambia. Na tunajenga bomba za kusafirishia gesi hadi Kenya, Uganda na Zambia ili tuweze ku export utajiri wetu wa gesi asilia. Au nazo bomba hizi zitaishia kutumika ku import gesi za nchi zingine?

Iweje sasa njia hizi badala ya kuzitumia ku export umeme wetu wa gesi wenye bei kubwa kupata dola (USD), ghafla tumeamua kuzitumia ku import umeme kuopeteza dola? Nani alimpa ushauri huo raisi wetu kwenye ziara yake huko Tanga? Eti kukatika katika kwa umeme kwenye mikoa hiyo ya Tanga, Kilimanjaro na Manyara kunatokana na mikoa hiyo kuwa mbali sana na vyanzo vya uzalishaji vya umeme vya JNHPP na Kinyerezi? Sasa huko Ethiopia ndiyo karibu kuliko JNHPP na Kinyerezi kweli? Mbona hata Mwanza, Mara, Kagera na Shinyanga ni mbali zaidi na umeme unakatikakatika? Hivyo mikoa hii nayo ipatiwe umeme wa Ethiopia? Ndiyo suluhisho lake kweli? Mwanzoni tuliambiwa tatizo ni njia za usambazaji ikiwemo ma transformers na serikali inalishughulikia na ilianzia kwenye jiji la Dar es Salaam. Baadaye Kafulila akapanga kubinafisha tanesco kwa jina la PPP!

Yaani tangia enzi za Richmond suala la umeme Tanzania limekuwa sarakasi juu ya sarakasi. Nani anaweza kukomesha hizi sarakasi? Bunge lilingilia sarakasi ya Richmond chini ya spika Samwel Sitta. Jee kwa sasa lina ubavu huo chini ya spika Tulia?
 
Back
Top Bottom