Kwa hili, ninawapa kongore watani zangu

Kwa hili, ninawapa kongore watani zangu

demigod

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
8,292
Reaction score
15,250
Nimeona taarifa ya kuwa Florent Ibengé amethibitishwa kuwa ndiye kocha mkuu wenu. Ningependa kuwapa kongore maana eneo muhimu kwenye timu ni kocha. wengi walikuwa wanawangoja kwa hamu kuona ni namna gani mtaweza kuishughulikia nafasi hiyo.

Bila shaka ni mwalimu mwenye falsafa ya mpira unao endana kabisa na timu yenu, pia ana uzoefu wa kutosha kwenye mashindano ya kimataifa. Sisi huku kwetu kunaonekana kana kwamba tunajaribu kufanya vyema msimu ujao wa michuano ya klabu bingwa.

Ukweli ni mchungu. Sisi watani zenu bado mnatutisha na namna yenu ya usakaji vipaji na usajili kwenye ngazi tofauti tofauti klabuni. Ninatumaini kuwa msimu ujao tutapata chngamoto ya kutosha sana kwenye mitanange ya ligi kuu na ASFC pia.

Kila la kheri.

wenu mtiifu,

Mwanamsimbazi Asiyekubalika na wengi
 
Unamfahamu Ibenge lakin?? Yule ni wa kuifundisha timu inayoshindwa kulipa mishahara wachezaji??
 
Back
Top Bottom