Hall huwa anasepa na kurudi Azam kwa kuwa kuna figisu za Kibongo kutoka kwa uongozi.
Azam ililazimika kuwachukua wafitini wa Bongo Soka ili kukabiliana na hujuma nyingi kutoka kwa timu za Kariakoo, sasa jamaa wamekuwa pia wajasiriamali na kuingilia mambo ya kiufundi ya timu.
Hii aliisema mwenyewe mwaka juzi wakati akitupa mafunzo ya ukocha pale Chuo Kikuu Mlimani. Kufanya kazi kitaalamu kwenye mazingira yetu ni vigumu sana, hata Serikalini!
Hiyo ni picha ya jinsi walivyo viongozi wetu. afu huwa wanakuwa kama hawajaenda shule. sijui wanakuwa wamesoma wapi au ni makusudi
Apendaye, chongo huita kengeza. Kama Hall ni kama anavyotakaswa, ni kipi kinachomfanya awe akirejearejea kwenye timu anayoijua haiendeshwi kitaalamu? Waswahili husema 'kugombana kutaka', Waingereza wao 'It takes two to make a quarrel' au 'it takes two to tango'. Sasa kama yeye hana tatizo, figisu zitamfikaje? Atagombanaje? Fikiri zaidi.Hall huwa anasepa na kurudi Azam kwa kuwa kuna figisu za Kibongo kutoka kwa uongozi. Azam ililazimika kuwachukua wafitini wa Bongo Soka ili kukabiliana na hujuma nyingi kutoka kwa timu za Kariakoo, sasa jamaa wamekuwa pia wajasiriamali na kuingilia mambo ya kiufundi ya timu. Hii aliisema mwenyewe mwaka juzi wakati akitupa mafunzo ya ukocha pale Chuo Kikuu Mlimani. Kufanya kazi kitaalamu kwenye mazingira yetu ni vigumu sana, hata Serikalini!
Apendaye, chongo huita kengeza. Kama Hall ni kama anavyotakaswa, ni kipi kinachomfanya awe akirejearejea kwenye timu anayoijua haiendeshwi kitaalamu? Waswahili husema 'kugombana kutaka', Waingereza wao 'It takes two to make a quarrel' au 'it takes two to tango'. Sasa kama yeye hana tatizo, figisu zitamfikaje? Atagombanaje? Fikiri zaidi.
Labda kuna anachokihitaji kutoka Azam, nasikia mazingira ya Soka letu ni bora na rafiki kuliko ligi nyingi za ukanda huu. Jamaa alihapewa fursa pia kwenye Kituo cha Soka cha Serikali pale Kidongo Chekundu, akiwa kama Mkurugenzi, hii ilikuwa mwaka jana. Sijui ilikuwaje akarejea tena Azam.
Kinachoiangusha Azam ni kukubali kuiga mfumo wa fitina baada ya kufanya kazi kitaalamu kushindikana. Azam FC ni kati ya taasisi za Baharesa zinazofanya hovyo na kuendeshwa kifitina fitina.