Kwa hili swala la wamachinga, Dar tutapaona pagumu

Watu ni vilaza sana, ambacho baadhi ya machinga wanafikiri nchi ilikua ya Magufuli . huu ni Utawala mwingine,

Mamlaka ya Nchi yako kwa
Bi.Samia Suluhu Hassan utawala wa magufuli ulishaisha, kikubwa watu tuache mambo ya kale tuende na wakati.
Na bado subirini huko sokoni mnakopelekwa ushuru wa soko unawafata, kila iitwapo leo.
 
hao wamachinga unaowaonawapumbavu wanamitaji mikubwa tu,wanaingiza kipato kikubwa kuliko wewe uliyesoma,unayejiona geniuos kapuku
 
utawala wa mama samia ambao watu wanapigana bastola msibani,tatizo nchii inaongozwa kisichana
 
Endeleeni kumkumbuka wakati wengine wanasonga mbele, Yeye Magufuli mbona alifanya kinyume na watangulizi wake pia na kuwaambia wanawashwa washwa? Ujinga wenu wa kujifanyia biashara holela bila kufuata utaratibu umekwenda na huyo jamaa yenu, hauna nafasi awamu hii
 
hao wamachinga unaowaonawapumbavu wanamitaji mikubwa tu,wanaingiza kipato kikubwa kuliko wewe uliyesoma,unayejiona geniuos kapuku
Mali bila hekima ni ujinga tu, unakua na mali halafu huna hekima ya kuifanyia mahali salama, likikupata jambo utamwambia nani akusikilize?
Halafu mnatafsiri mbaya kuhusu mali,

Mali kila mtu atapata kwa juhudi zake, ila je dhoruba za maisha zinaponyanyuka hizo mali zinakusaidiaje?
 
Wamachinga wanazuia kila eneo. Kuanzia kwa watembea kwa miguu mpaka kwenye maduka ya watu. Ukiona bodaboda, ambao pia wanapaki kila wanapoona panafaa, lazima mama ntilie awepo. Hakuna utaratibu na hili ni tatizo kubwa sana
 
JPM alikuwa ni baba kweli kweli. Ila hili la wamachinga alikuwa anatengeneza bomu. lazima angekuja kupambana nalo mbele ya safari.
Sio busara nchi ikawa na umachinga usioratibiwa
 
kwahiyo kama unategemewa unaruhusiwa kwenda mbele ya duka la mtu ukaweka bidhaa zako au unaenda kwenye shamba la mtu unalima au kuvuna mazao yake
Acha wehu
nikikuta mnafanya vurugu naungana na polisi kuwapiga
 
JPM alikuwa ni baba kweli kweli. Ila hili la wamachinga alikuwa anatengeneza bomu. lazima angekuja kupambana nalo mbele ya safari.
Sio busara nchi ikawa na umachinga usioratibiwa

Angekuwapo asingeona tatizo kwa sababu ndio fikira zake zilikuwa zimefika hapo
 
kila zama na kitabu chake mkuu mlipewa uhuru mkauchezea mkafanya mji uwe mchafu kupindukia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…