Kwa hilo la UMEME Nchi nzima hongera Serikali.

Li ngunda ngali

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2023
Posts
707
Reaction score
2,572
Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni.

Nachukua fursa hii kuipongeza Serikali kwa KUTIMIZA WAJIBU wake kwa kuhakikisha Tanzania nzima inao mtandao wa mwanga wa nishati ya umeme karibu Miji na Vijiji vyote.

Tunaweza kuona ni jambo dogo lakini kwa wenzetu hiyo ni habari kubwa na maendeleo ya kupigiwa mfano!

Leo hii Nchi yetu yapo mambo baadhi tunaweza kujivunia kama Taifa pasipo kujali Itikadi zetu. Mtandao mpana wa barabara za lami na mtandao wa umeme hadi vijijini ni mambo yanayotupasa tujivunie kama Taifa.

Kwa mara nyingine, naipongeza Serikali kwa kutimiza wajibu wake kwalo.

TANESCO
 
Tumeambiwa kuna maboresho TANESCO wanafanya kwenye mita, sijui wanaboresha nini. Kuna mdau kanijaza hofu kuwa wanafanya configuration itakayofanya upate kiasi cha umeme kisicholingana na pesa uliyolipia.

Mwingine anadai kinachofanywa ni tariff merger. Anayejua kinachofanywa atujulishe tulio gizani.
 
na huo ndio ungwana,
well done serikali sikivu ya awamu ya6🐒
 
Kwa hili.... Hata Mimi naipa Kongole serikali....
 
Basi mnapotuletea umeme huku vijijini, tufungieni transfoma kubwa. Sio hizi 50KvA. Tuna mahitaji makubwa pia ya umeme sio tu kuwasha Tv na taa. Kijiji kinawekewa transfoma amabayo inasua sua hata kusukuma motor moja tu ya 40HP! TANESCO
 
0ngea mambo mengine suala la umeme bado sana, asilimia kubwa umeme umefika ila asilimia kubwa sana watu hawana umeme na wahitaji ni wengi sana, serikali imeweza kufikisha umeme sehemu za mijini na sehemu yaliko makao makuu ya kijiji au vijiji na sehemu ambako kuna huduma za kijamii kama shule za sekondari au vituo vya afya lakini vitongoji vingi sana umeme hamna, nakupa mfano hai,kuna vitongoji vingi sana vimo ndani ya km zisizo zidi mbili au tatu kutoka yalipo makao makuu ya wilaya au miji lakini hakuna umeme. Mbali na mijini, ni wilaya moja tu ambako hapa Tanzania umeme umefika kwa zaidi 97 %
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…