Kwa huu uzushi Serikali ipige marufuku mahindi kwenda Kenya, badala yake mahindi ya ziada yatumike kuzalisha vyakula vya mifugo

Kwa huu uzushi Serikali ipige marufuku mahindi kwenda Kenya, badala yake mahindi ya ziada yatumike kuzalisha vyakula vya mifugo

Nyumisi

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2010
Posts
13,499
Reaction score
19,292
Hivi karibuni kumetolewa madai na kenya kuhusu mahindi yetu kuwa na sumu kuvu. Swala la milipuko ya watu kuugua na kufa kwa kula mahindi yenye viwango vya juu vya aflatoxin limekuwepo nchini kenya tangu mwaka 1981. Mfano, mwaka 2004 wakenya 317 waliugua na 125 walifariki kutokana na kutumia mahindi yenye viwango vya juu vya sumu kuvu aina ya aflatoxin.

Chanzo cha tatizo yalikuwa ni mahindi yaliyokuwa yamezalishwa na wakulima wenyewe na kuhifadhiwa katika mazingira mabovu. Kwa hiyo utaona hayo mahindi hayakutoka Tanzania.

Nchini kenya kumekuwa na kawaida ya Wafanyabiashara wakubwa kuagiza na kuhodhi mahindi kwa muda mrefu hali inayopelekea sumu kuvu kuendelea kuzalishwa yakiwa yamehifadhiwa, na baadaye kutolewa kwa bei chee kwa watu maskini ambao wanakuwa wamekumbwa na uhaba mkubwa wa chakula, na hivyo kutokea milipuko ya aflatoxin.

Haiwezekani uagize na kuhifadi mahindi, miaka mitano baadaye useme hayo mahindi yenye aflatoxin yametoka Tanzania. Utafiti umeonyesha mahindi yaliyovunwa maeneo mbalimbali nchini Tanzania yana viwango vya chini sana vya aflatoxin ambavyo ni chini ya viwango vya wastani vinavyopendekezwa na mamlaka za usalama wa chakula nchini Tanzania.

Kenya wanapokuja na tuhuma zisizokuwa na mashiko maana yake wana ajenda nyingine ambazo wanakuwa wamebeba na hii si mara ya kwanza. Kwa hiyo ili kuweka mazingira ya kuheshimiana ni bora serikali ichukue hatua mathubuti dhidi ya hizi sarakasi za kila mara kutokea Kenya.
 
Wazo zuri ila chakula cha mifugo mahindi yanatakiwa kuwa ya bei chee, solution ni serikali kununua ziada iliyopo.
 
Naona tu unaishutumu Kenya bila hata kusema kama Kenya wenyewe wametoa shutuma dhidi ya Tz au kuna uthibitisho kuwa si mahindi ya Tz yenye tatizo! Angalau umekiri kuwa kuvu inaweza kuua.

Lawama imekuwa ni moja ya sifa zetu. Tukilaumiwa na sisi tunalaumu!
 
Kenya inatumika vibaya! Msiseme tena sikuwaambia. Uhuru ni kama fimbo kwenye mkono wa mtawala jahili wa London & Washington

Habari ya kuogopa kivuli na kujifanya ujuaji. Hakuna habari za “vita ya kiuchumi”, inaitwa “kuwa na maslahi”. Ni kawaida kwa kila taifa kufanya mambo kwa maslahi. Hata sisi tuwe na maslahi katika mambo yetu, tusifikiri tu tunapigwa vita!!
 
Habari ya kuogopa kivuli na kujifanya ujuaji. Hakuna habari za “vita ya kiuchumi”, inaitwa “kuwa na maslahi”. Ni kawaida kwa kila taifa kufanya mambo kwa maslahi. Hata sisi tuwe na maslahi katika mambo yetu, tusifikiri tu tunapigwa vita!!
You are speaking in circles --- yaani, unarudia mlemle unamokataa 🙂
 
Wazo zuri ila chakula cha mifugo mahindi yanatakiwa kuwa ya bei chee, solution ni serikali kununua ziada iliyopo
Serikali ipi? kwani kila mwaka si huwa wananunua kwa kumkopa mkulima? kwa shilingi 500@kilo!? Mwaka juzi nilikuwa mkoa wa katavi, NFRA, hawapati watu wa kupeleka mahindi, yaani mkulima aache kuuza kwa cash, apeleke akakopwe tena kwa bei iliyochini ya bei ya soko? Tusidanganyane serikali haina uwezo wa kununua mahindi yote yalimwayo nchini!!
 
Naishauri serikali yetu imfungulie Uhuru jalada ICC kule The Hague la kuruhusu kisiwa chetu cha Amani kichafuliwe hadhi kiasi hiki. This is complete controversial nonsense!
 
Kenya wanapokuja na tuhuma zisizokuwa na mashiko maana yake wana ajenda nyingine ambazo wanakuwa wamebeba na hii si mara ya kwanza.
Umefanya vipimo kwa sampuli husika, au na wewe unaleta uzushi kwa kutuhumu tu?!
 
Sikiliza ndugu yangu. Unayoyasema inawezakana yakawa na ukweli na yanaweza yasiwe ya kweli. Jambo la msingi linalotakiwa kufanywa hapa ni kurudisha mahusiano mazuri na Nchi jirani kama ilivyokuwa katika utawala wa Kikwete. Nasema hivi kwasababu kubwa moja, tukiendelea kutumia nguvu kutatua huu mgogoro baadae litakuja kuibuka jambo lingine kubwa zaidi ya hili.

Kama unakumbuka katika kipindi cha mwaka jana tu yametokea matukio mawili baina yetu na Nchi hiyo hiyo ya Kenya. La kwanza ni lile la kuzuia madereva wa Tanzania wasiingie Kenya kwa ajili ya CORONA na la pili ni lile la kuzuia ndege za Tanzania zisingie Kenya. Suluhisho lilikuwa ni kutumia nguvu kwa kuwalipizia.

Je? Kwa maamuzi yale unafikiri yameleta muafaka wa kuzuia mambo mengine yasitokee? Jibu ni hapana na ndio maana unaona hadi limekuja tena kuibuka hili la Mahindi mwaka huu. Kimsingi inaonyesha kuna mambo mengine nyuma yake ambayo mimi na wewe hatuyajui.

Hivyo jambo la msingi la kufanya ni lazima Diplomasia itumike katika kutatua matatizo haya yenye viashiria vya kisasi baina ya Kenya na Tanzania kwa kutafuta suluhisho la kudumu badala ya kila wakati kutunishiana misuli. Yangu ni hayo tu.
 
Kenya inatumika vibaya! Msiseme tena sikuwaambia. Uhuru ni kama fimbo kwenye mkono wa mtawala jahili wa London & Washington
Hili ni la ndani kwa ndani, halihusu hizo nchi nyingine, pamoja na kukubaliana na wewe juu ya ukibaraka na undumila kuwili wa huyo kiongozi.

Hili la mahindi ni la wafanya biashara wanaochezesha kinyago kila wanapotaka kufanya hivyo.

Uchaguzi wao unakaribia 2022; ni wakati wa kujipanga kupata mavuno toka kwa wanasiasa.
 
Tz tunahitaji Nuclear Capable weapons.

Tukifanikiwa. tutakua na uwezo wa kujilinda na kuwalinda mataifa mengine ya Kiafrica.

Kenya usaliti wao kwa tz haujaanza leo.

Ukitaka kujua, Rejea ya Nyerere na kenya juu ya EAC ya kipindi kile.

Kwa hili huyu kijana Kenyata anatumiwa na mabeberu.
 
Kenya wanapokuja na tuhuma zisizokuwa na mashiko maana yake wana ajenda nyingine ambazo wanakuwa wamebeba na hii si mara ya kwanza. Kwa hiyo ili kuweka mazingira ya kuheshimiana ni bora serikali ichukue hatua mathubuti dhidi ya hizi sarakasi za kila mara kutokea Kenya.
Kwani jiwe yupo wapi saivi?
 
Habari ya kuogopa kivuli na kujifanya ujuaji. Hakuna habari za “vita ya kiuchumi”, inaitwa “kuwa na maslahi”. Ni kawaida kwa kila taifa kufanya mambo kwa maslahi. Hata sisi tuwe na maslahi katika mambo yetu, tusifikiri tu tunapigwa vita!!
Nakubaliana na wewe. Ni sawa na mtu anayeogopa kulogwa. Anawaza na kuogopa kila mtu, hata ndoto anaiogopa.
Ni hulka ya binadamu kuvutia kwake, wewe vuta pia kama nguvu ndogo kula na fanya mazoezi sio kulalamika.
 
Hili swala ni dogo wala halipaswi kukuzwa hivi.

Suluhu ni wataalzmu kutoka Kenya na Tanzania wangepima sample chache na waseme walichoona.

Pili wafanye uchunguzi kuhusu ununuzi, uhifadhi na usafirishaji na muda.

Wakulima na wafanya biashara wanaumia huku wakubwa wanalumbana. Haisaidii zaidi ya kuzidisha bifu.
 
Back
Top Bottom