chinchilla coat
JF-Expert Member
- May 16, 2016
- 5,107
- 10,969
Najua wengi hawampendi Ndugai, ni kutokana na uvunjifu mkubwa wa katiba na utawala wa sheria alioufanya tokea awamu ya 5, mi binafsi pia simkubali
Sasa kilichonishtua ni hii reaction ya CCM iliyoonyeshwa kwa Ndugai kwa maoni aliyotoa ambayo kimsingi yalikuwa yamelenga kutetea tozo za Serikali
Wamejitokeza viongozi wa CCM kila upande wa nchi wakimshambulia Ndugai hadi wengine kusema kuwa Ndugai ni mgonjwa na Samia anatakiwa akamtibu
Simuonei huruma Ndugai, nashangaa tu kama CCM wameweza kumshabulia vile mtu ambaye wamempa cheo kikubwa kama Uspika kwa ukosoaji wa kawaida tu, je watawafanyaje kwa Wapinzani ambao watatumia lugha kali zaidi kuwakosoa na hawana cheo kama cha Ndugai?
Wapinzani wataungana na CCM kumshambulia Ndugai, sababu Ndugai ni kweli amefanya ufedhuli mwingi dhidi yao, lakini kumbuka kuwa ni CCM hawahawa walikuwa wakimuunga mkono Ndugai au kumtuma kufanya ufedhuli huo
Kwa Polepole ni hivyo hivyo, sasa kuna baadhi ya Wapinzani wameahidiwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mikutano na wakaamini, kwa akili ya kawaida tu, CCM hii ambayo inakuwa kama mbogo aliyejeruhiwa Serikali yake inapokosolewa kidogo tu, ndio itawaruhusu wapinzani wachaguliwe au wafanye mkutano ya kuwakosoa vikali?
Sasa kilichonishtua ni hii reaction ya CCM iliyoonyeshwa kwa Ndugai kwa maoni aliyotoa ambayo kimsingi yalikuwa yamelenga kutetea tozo za Serikali
Wamejitokeza viongozi wa CCM kila upande wa nchi wakimshambulia Ndugai hadi wengine kusema kuwa Ndugai ni mgonjwa na Samia anatakiwa akamtibu
Simuonei huruma Ndugai, nashangaa tu kama CCM wameweza kumshabulia vile mtu ambaye wamempa cheo kikubwa kama Uspika kwa ukosoaji wa kawaida tu, je watawafanyaje kwa Wapinzani ambao watatumia lugha kali zaidi kuwakosoa na hawana cheo kama cha Ndugai?
Wapinzani wataungana na CCM kumshambulia Ndugai, sababu Ndugai ni kweli amefanya ufedhuli mwingi dhidi yao, lakini kumbuka kuwa ni CCM hawahawa walikuwa wakimuunga mkono Ndugai au kumtuma kufanya ufedhuli huo
Kwa Polepole ni hivyo hivyo, sasa kuna baadhi ya Wapinzani wameahidiwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mikutano na wakaamini, kwa akili ya kawaida tu, CCM hii ambayo inakuwa kama mbogo aliyejeruhiwa Serikali yake inapokosolewa kidogo tu, ndio itawaruhusu wapinzani wachaguliwe au wafanye mkutano ya kuwakosoa vikali?