Kwa kipaji hiki alichonacho, unashauri ajiendeleze kwa namna ipi?

Kwa kipaji hiki alichonacho, unashauri ajiendeleze kwa namna ipi?

Heaven Seeker

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2017
Posts
479
Reaction score
1,071
Heshima kwenu Wakuu.

Mtoto wa binamu yangu hakufanikiwa kupata ufaulu mzuri wa kuendelea na masomo ya kidato cha tano mwaka huu.

Lakini kutokana na kipaji cha uchoraji alichonacho tukaona ni vema ajiendeleze kwa kuongezea taaluma juu ya kipaji chake.

Kulitolewa wazo la kumpeleja VETA na mipango yote ikafanyika. Ikashauriwa asome course inaitwa " Paintig and Sign Writing". Ila baada ya majibu kutoka akawa amechaguliwa hapo VETA Chang'ombe course inaitwa "Pre Press and Digital Printing". Sikujua kama unaweza kwenda VETA kuomba kusoma kitu flani na usipewe ila ukachaguliwa kitu tofauti na ulichoomba. Any way hiki ni kibwagizo tu..

Naomba niwe muwazi kuwa sina ufahamu wa kutosha wa hizo courses zote mbili. Vilevile sina ufahamu wa kutosha wa aina na kiwango cha Elimu ya VETA inavyotolewa. Muda wa mafunzo VETA inaonesha ni miaka miwili na ada ni kama 300K hivi na senti kidogo.

Concern yangu kubwa imekuwa ni thamani ya muda huo atakaokuwa hapo VETA na aina ya ujuzi ama Taaluma atakayoipata. Maana ningefurahi kama angejifunza kitu kitakachomuwezesha kujiajiri na kuendeleza kipaji chake.

Baada ya Tafakari ya muda, nimefikiri labda tumpeleke Training center ambayo ni private hapo Posta akajifunze Graphics designing kwa miezi miwili badala ya kutumia muda wa miaka 2 kujifunza vitu ambavyo hatuvielewi kwa undani. Akijifunza Graphics anaweza kujiajiri huku akiangalia namna ya kuendeleza kipaji chake cha uchoraji.

Naombeni ushauri wenu katika hili. Je, kwa kipaji cha uchoraji alichonacho mtu anaweza kujiendeleza kwa njia gani?

Naambatanisha na picha zake ambazo huwa anachora. Samahani kwakuwa hazionekani vizuri sana.

Natanguliza shukrani zangu kwa dhati Wakuu. Mawazo yenu huwa nayaheshimu sana. JF imekuwa dira katika mambo yangu mengi sana..
10.jpeg

9.jpeg

8.jpeg

7.jpeg

6.jpeg

5.jpeg

4.jpeg

3.jpeg

2.jpeg

1.jpeg
 
Heshima kwenu Wakuu.

Mtoto wa binamu yangu hakufanikiwa kupata ufaulu mzuri wa kuendelea na masomo ya kidato cha tano mwaka huu.

Lakini kutokana na kipaji cha uchoraji alichonacho tukaona ni vema ajiendeleze kwa kuongezea taaluma juu ya kipaji chake.

Kulitolewa wazo la kumpeleja VETA na mipango yote ikafanyika. Ikashauriwa asome course inaitwa " Paintig and Sign Writing". Ila baada ya majibu kutoka akawa amechaguliwa hapo VETA Chang'ombe course inaitwa "Pre Press and Digital Printing". Sikujua kama unaweza kwenda VETA kuomba kusoma kitu flani na usipewe ila ukachaguliwa kitu tofauti na ulichoomba. Any way hiki ni kibwagizo tu..

Naomba niwe muwazi kuwa sina ufahamu wa kutosha wa hizo courses zote mbili. Vilevile sina ufahamu wa kutosha wa aina na kiwango cha Elimu ya VETA inavyotolewa. Muda wa mafunzo VETA inaonesha ni miaka miwili na ada ni kama 300K hivi na senti kidogo.

Concern yangu kubwa imekuwa ni thamani ya muda huo atakaokuwa hapo VETA na aina ya ujuzi ama Taaluma atakayoipata. Maana ningefurahi kama angejifunza kitu kitakachomuwezesha kujiajiri na kuendeleza kipaji chake.

Baada ya Tafakari ya muda, nimefikiri labda tumpeleke Training center ambayo ni private hapo Posta akajifunze Graphics designing kwa miezi miwili badala ya kutumia muda wa miaka 2 kujifunza vitu ambavyo hatuvielewi kwa undani. Akijifunza Graphics anaweza kujiajiri huku akiangalia namna ya kuendeleza kipaji chake cha uchoraji.

Naombeni ushauri wenu katika hili. Je, kwa kipaji cha uchoraji alichonacho mtu anaweza kujiendeleza kwa njia gani?

Naambatanisha na picha zake ambazo huwa anachora. Samahani kwakuwa hazionekani vizuri sana.

Natanguliza shukrani zangu kwa dhati Wakuu. Mawazo yenu huwa nayaheshimu sana. JF imekuwa dira katika mambo yangu mengi sana..
View attachment 2060815
View attachment 2060816
View attachment 2060817
View attachment 2060818
View attachment 2060819
View attachment 2060820
View attachment 2060821
View attachment 2060822
View attachment 2060823
View attachment 2060824
Nakushauri uende Veta Ukasome Syllabus za hiyo course aliyochaguliwa..

Sent from my M2006C3MG using JamiiForums mobile app
 
Goliath ana vinywele kama njomba nchumali

Anyway zote ni sahihi hatma itamuamulia
 
bora akasome graphic design.ingawaje veta napo pazur.akisoma veta ni mpk diplpma? hawez ingia chuo akapige bachelor ya fine arts?
 
My best Artist kwenye kuchora ni Jack Kirby na Steve Ditko (Both RIP), kwa kipaji chake hicho anaweza kua Cartoonist/Comics painter mzuri sana kama hao nilio wataja (Google kazi zao)
Besides...!
Yeye binafsi ndoto yake ni kua mchoraji au anafanya kama hobby ila wazazi mmemshinikiza kusomea uchoraji?
 
Yeye anandoto gani?
Kumbuka kuna dreams halafu kuna maisha. Pia kuna watu wanaishi dreams zao. Wengine huishi drema zao kwa kuchelewa. Ongea naye kwanza
 
bora akasome graphic design.ingawaje veta napo pazur.akisoma veta ni mpk diplpma? hawez ingia chuo akapige bachelor ya fine arts?
Sijajua Mkuu. Nadhani wana madaraja yao. Sasa sina uhakika kama atafikia hadi diploma. Ila concern yangu ilikuwa either aendeleze kipaji chake ama ajifunze kitu kitakachomfanya ajiajiri. Sasa naona kama miaka miwili ya VETA kusoma 'Pre press and Digital Printing' kisha arudi mtaanai si bora ajifunze graphics atakuwa anapata angalau pesa ya kujikimu kwa kazi mbili tatu huku akitafuta mtaji wa kuendeleza fani yake taratibu? Umri nao unasonga, jinsia yake ni KE.
 
My best Artist kwenye kuchora ni Jack Kirby na Steve Ditko (Both RIP), kwa kipaji chake hicho anaweza kua Cartoonist/Comics painter mzuri sana kama hao nilio wataja (Google kazi zao)
Besides...!
Yeye binafsi ndoto yake ni kua mchoraji au anafanya kama hobby ila wazazi mmemshinikiza kusomea uchoraji?
Nashukuru kwa maoni yako mkuu. Mzee wake (binamu) katangulia mbele za haki mwaka huu. Kwakweli yeye anapenda kujiendeleza kwa kipaji chake. Zaidi navyoona yeye hana uchaguzi sana, yaani anategemea ushauri wetu. Na mie ndio kama mshauri mkuu kwa sasa.
Mkuu, hata mie naona anweza kuwa cartoonist mzuri sana. Ila sasa sijui pakuanzia ndio maana nimekuja kupata ushauri hapa. Ningekuwa na connection ma Masoud Kipanya ningemuomba ushauri moja kwa moja.
 
Yeye anandoto gani?
Kumbuka kuna dreams halafu kuna maisha. Pia kuna watu wanaishi dreams zao. Wengine huishi drema zao kwa kuchelewa. Ongea naye kwanza
Ahsante sana kwa ushauri wako Mkuu. Ninaufanyia kazi.. Japokuwa navyoona yeye ni kama anasikiliza sana anachoshauriwa. Ni Binti..
 
Nilipokuwa kinda ndoto yangu ilikuwa ni kuwa pilot🤣 sasa hivi ni pilot wa maisha yangu
 
Nimeshangaa zaidi kujua kumbe ni binti.

1. VETA walikuwa sahihi kutompeleka kwenye kozi mliyoomba maana pia teknolojia ya uchoraji na uhifadhi picha inabadilika kwa kasi. Labda ndio maana amepangiwa kusoma Pre Press and Digital Printing.
Labda wanataka kuhusianisha kipaji chake na taaluma ya ku-design bidhaa kabla na kisha kuprint digitally.
Pale VETA ya Chang'ombe wana kiwanda cha printing na wana digital machine za kuprint na wanapata zabuni nyingi sana za kuprint bidhaa mbali mfano vitabu, kalenda, diaries, mitihani, stickers, vifungashio, labels n.k labda wameona kuna future huko ndio maana wamemuweka kwenye hiyo kozi.
Vipo pia viwanda vingi vya digital printing hapo mjini Dar.

2. Graphic design ni nzuri zaidi hasa kwa kuwa tayari ana kipaji cha kuchora, kwahivyo kwake itakuwa rahisi zaidi kuchora kwa kutumia teknolojia. Lakini nionavyo hapa atahitaji kujiajiri zaidi kuliko kusubiri kuajiriwa na pia ushindani ni mkubwa. Kipaji na upekee wa mtu ndivyo humletea mtu kazi na pesa.

3. Kama ni mtu sharp na anapenda kujifunza na kipato mnacho cha kum-support basi anaweza kusoma hiyo kozi ya VETA na wakati huohuo anasoma/jisomea Graphic design. Wako watu wanaweza kusoma mambo mawili kwa wakati mmoja. Anaingia darasani VETA asubuhi kisha akitoka anaenda kwenye kusoma Graphic design ama chuoni ama mtandaoni.

NB: Kupanga ni Kuchagua. Tunamtakia uchaguzi mwema.

Cha muhimu ni kuweka juhudi kwenye kile ulichochagua na kuwa positive. Mengine yatajipa mbele huko.
 
Nimeshangaa zaidi kujua kumbe ni binti.

1. VETA walikuwa sahihi kutompeleka kwenye kozi mliyoomba maana pia teknolojia ya uchoraji na uhifadhi picha inabadilika kwa kasi. Labda ndio maana amepangiwa kusoma Pre Press and Digital Printing.
Labda wanataka kuhusianisha kipaji chake na taaluma ya ku-design bidhaa kabla na kisha kuprint digitally.
Pale VETA ya Chang'ombe wana kiwanda cha printing na wana digital machine za kuprint na wanapata zabuni nyingi sana za kuprint bidhaa mbali mfano vitabu, kalenda, diaries, mitihani, stickers, vifungashio, labels n.k labda wameona kuna future huko ndio maana wamemuweka kwenye hiyo kozi.
Vipo pia viwanda vingi vya digital printing hapo mjini Dar.

2. Graphic design ni nzuri zaidi hasa kwa kuwa tayari ana kipaji cha kuchora, kwahivyo kwake itakuwa rahisi zaidi kuchora kwa kutumia teknolojia. Lakini nionavyo hapa atahitaji kujiajiri zaidi kuliko kusubiri kuajiriwa na pia ushindani ni mkubwa. Kipaji na upekee wa mtu ndivyo humletea mtu kazi na pesa.

3. Kama ni mtu sharp na anapenda kujifunza na kipato mnacho cha kum-support basi anaweza kusoma hiyo kozi ya VETA na wakati huohuo anasoma/jisomea Graphic design. Wako watu wanaweza kusoma mambo mawili kwa wakati mmoja. Anaingia darasani VETA asubuhi kisha akitoka anaenda kwenye kusoma Graphic design ama chuoni ama mtandaoni.

NB: Kupanga ni Kuchagua. Tunamtakia uchaguzi mwema.

Cha muhimu ni kuweka juhudi kwenye kile ulichochagua na kuwa positive. Mengine yatajipa mbele huko.
Nashukuru sana kwa inputs zako Mkuu. Umetoa ushauri mzuri sana.
 
Kawaida tu.Kibongo mmh kupiga pesa itakua ngum sana
 
Back
Top Bottom