Sina elimu ya chuo ya uchumi, lakini ninachojua hakuna kisichoathirika uchumi ukiyumba.
Hiko chakula kama Muuza cement hauzi tena mifuko 50 kwa siku kama zamani upo uwezekano mchana asije kula kwenye mgahawa wako, akasubiri usiku akale nyumbani kwake.
Muuza fenicha akikaa mwezi mzima hajauza meza, akisikia mwili unauma haendi hospitali ataishia kumuuliza shangazi amwambie chemsha majani ya mchunga unywe.
Mwenye salon akikosa Wateja usitegemee atasafiri kwenda kumuona Mama mgonjwa Mwanza, mwaka mzima ni meseji tu.
Nyumba za kupanga nazo zinategemea hao Mama ntilie, wenye Hardware...watakulipaje kodi nao hawauzi?