Kwa kugawa wanyama wetu tumeuza upekee wetu. Tumebaki na nini?

Kwa kugawa wanyama wetu tumeuza upekee wetu. Tumebaki na nini?

Waachiwe kwenda jangwani?

Wataweza kumuona cheetah anawinda swala kama Serengeti?

Wataona Wilderbeast migration
Kinachoshindikana nini?.kama watu wa jangwan wanaweza kufanya mazingira wakalima mazao na wakatuletea kutuuzia unafikiri kinashindikana nini kutengeneza hifadhi.
 
Wee acha tu mkuu, wapenda asili tupo wengi ila hao wasiojali wana laana leo na kesho

Mkuu tuna farm mkoani huko na kuna maji tuliochimba wenyewe kwa kunywesha mifugo
Ndege wa aina zaidi ya kumi wanakuja hapo
Tatizo likawa kwa watoto wenye manati ikawa ndio sehemu ya mawindo yao

Ilibidi nitume vijana kukamata na kuwanyan'ganya manati
Huwezi kuamini within three weeks walijaza ndoo nne za manati na mwisho watoto wakaacha kuja kabisa
Ila kila wakikamatwa walikuwa wanapewa na darasa kuhusu kuwalinda badala ya kuwauwa

Haya yote tulikuwa tunafundishwa shuleni na manyumbani ila sio siku hizi
Unafanya jambo la kizalendo sana. I hope tutaamka. Na wengine wanaweza kusema usilalamile tu toa ushauri nini kifanyike.

Ushauri wangu ni huu, hili jambo lingefanywa kwa uwazi kabisa. Moja ya faida za kufanya hivyo ni pride. Watanzania wakijua wanasaidia kujenga mataifa mengine kwa fadhila kama hizi, watatembea vifua mbele kwa pride badala ya kuishi kinyonge kama sasa.

Pili tungeingia ubia na hizo kampuni zinazoendesha hizo zoo na parks. Hii itatuhakikishia mapato ya vizazi vijavyo. Hizi pesa za kulipana chini kwa chini kwanza zina harufu ya ufisadi na zinaweza kuishia kufanyia matumizi yasiyo na tija. Pia tukiwa kwenye management za uendeshaji, tutajifunza mengi ambayo tunaweza kuja kuyatumia hata huku kwetu.

Yote haya yanahitaji viongozi na watendaji waadilifu sana.
 
Hiyo mbuga inayotengenezwa dubai ni replica au ni mfanano na mbuga ya serengeti, hivyo ni tishio kubwa la utalii wetu hapo mbeleni........viongozi waliopewa dhamana wanahujumu nchi kwa maslahi yao binafsi, na kama ulivyodokeza, mbali na tishio la kutoweka wanyama adimu huko serengeti kutokana na kulegalega kwa shughuli za uhifadhi, pia hujuma zinaweza kufanyika dhidi ya wanyama tulio nao ili kuipa nguvu hiyo mbuga ya mchongo huko dubai...​
Huwa nashangaa sana ninapoona viongozi wanaenda huko nje na kuomba wafundishwe mbinu mbalimbali, najiulizaga hivi dunia hii tunaijua kweli?

Kama tunataka tujifunze vitu, peleka vijana wakasomee hayo mambo, wakimaliza wape mitaji warudi wafanye hizo biashara. Hivyo ndiyo Wachina, Wajapan na Wakorea wamefanya. Sisi tunapeleka uswahili wa kumuomba jirani chumvi nyanja za kimataifa.
 
Sijasema hivyo. Kwa hiyo unabisha kuwa ukiacha wale tausi tuliompa Kenyatta hatujawahi kugawa wanyama wetu kwa mataifa mengine?
Mkuu kwamba Tanzania ndiyo asili ya wanyama waliojaa dunia nzima?
 
Just imagine daraja la Tanzanite tumelijenga kwa mkopo, tena mkopo tunaoulipia kwa kukamuana kwa tozo. Leo hii tunalingishia lile lipastic tuliloweka juu pale hatujiulizi kwa nini hatukujenga hilo daraja kwa mapato yatokanayo na madini hayo ili kweli tuwe na kitu tangible kuonyesha faida za madini hayo.
Mambo mengine yanaudhi mpaka mtu unatamani kulia. Mwalimu alikuwa ameacha madini ili baadae yaje kuchimbwa wakati tunaweza kupata faida iliyo stahiki.

Matokeo yake sasa, madini yamechimbwa na tumeachiwa mashimo na hakuna cha kujivunia

Sent from my SM-J810F using JamiiForums mobile app
 
Just imagine daraja la Tanzanite tumelijenga kwa mkopo, tena mkopo tunaoulipia kwa kukamuana kwa tozo. Leo hii tunalingishia lile lipastic tuliloweka juu pale hatujiulizi kwa nini hatukujenga hilo daraja kwa mapato yatokanayo na madini hayo ili kweli tuwe na kitu tangible kuonyesha faida za madini hayo.
Mambo mengine yanaudhi mpaka mtu unatamani kulia. Mwalimu alikuwa ameacha madini ili baadae yaje kuchimbwa wakati tunaweza kupata faida iliyo stahiki.

Matokeo yake sasa, madini yamechimbwa na tumeachiwa mashimo na hakuna cha kujivunia

Sent from my SM-J810F using JamiiForums mobile app
 
Mambo mengine yanaudhi mpaka mtu unatamani kulia. Mwalimu alikuwa ameacha madini ili baadae yaje kuchimbwa wakati tunaweza kupata faida iliyo stahiki.

Matokeo yake sasa, madini yamechimbwa na tumeachiwa mashimo na hakuna cha kujivunia

Sent from my SM-J810F using JamiiForums mobile app
Labda angeyaruhusu yachimbwe wakati huo ilikuwa rahisi kudhibiti, la kwanza tulikuwa wachache na pili Uadilifu na uaminifu ilikuwa kawaida sana

Hakujua tu kuwa mambo yatabadikika na watakuja majambazi wasiokuwa na uchungu wa nchi ambapo wanaweza hata kuuza hewa tunayovuta ya bure ili tufe wote

Wakati mwingine naona wakuja ni wazalendo kuliko hao wanaojiita wazawa na kutambia makabila bali majizi yasiokuwa na Soni wala aibu
 
Mkuu kwamba Tanzania ndiyo asili ya wanyama waliojaa dunia nzima?
Mbona umekazia sana hilo swali? Na mimi nitakuuliza tena Tanzania hatujawahi kugawa wanyama?
 
Moja ya jambo muhimu katik biashara ni upekee wa bidhaa yako. Watu hawaji kununua kwako bidhaa au huduma kwa sababu ya huruma, ni kwa sababu una kitu wanachohitaji na unakitoa kwa ubora kuliko washindani wako.

Kwa miaka kadhaa huko nyuma Tanzania tumetokea kugawa wanyama wetu kwa mataifa mbalimbali. Inawezekana hii ilifanywa kukuza mahusiano na nchi hizo, inawezekana imefanywa tu kwa sababu ya tamaa ya wachache. Inawezekana pia tulilipwa fidia.

Ila tujiulize tunapoteza nini kwa kufanya hivyo? Je mtalii akiambiwa achague kwenda safari Dubai, sehemu yenye miundombinu na huduma bora kutuzidi, kweli atachagua kuja kwetu aache kule? Tena ukizingatia hawa hawa tunaowapa wanyama tunawapa pia nafasi ya kufungua mahoteli katika mbuga zetu na kuwa agents wa utalii, hawawezi kuwa wanavutia kuwapeleka watalii kwao badala ya kuwaleta huku kwetu?

Ujangili tumeshindwa pia kuudhibiti kwa maana hiyo kuna uwezekano kuna wanyama watapotea huku kwetu ila watakuwepo huko tulipowagawa. Hizi lawama atazibeba nani?

Kwa mtazamo wangu, dunia inahitaji mashirikiano kati ya nchi na nchi ila ni muhimu sana kumaintain competitive advantage uliyo nayo katika uchumi na biashara. Uzalendo unaanzia hapo.
Kwa mtazamo wangu, dunia inahitaji mashirikiano kati ya nchi na nchi ila ni muhimu sana kumaintain competitive advantage uliyo nayo katika uchumi na biashara. Uzalendo unaanzia hapo.[emoji1545][emoji817]
 
Back
Top Bottom