Uchaguzi 2020 Kwa kuwepo "haki" tu, tunamaliza uchaguzi salama

Uchaguzi 2020 Kwa kuwepo "haki" tu, tunamaliza uchaguzi salama

Kama haki ipo kuna haja gani ya magufuli kuiongelea,? Haki anayoiongelea lissu ni kuhusu watu walio mpiga risasi kutokamatwa na kupelekwa mahakamani, na yote lisy anajua ni kwanini hakujakuwa na feedback ya hiyo inshu kutoka kwenye mamlaka..lakini ndo isiwe sababu binafsi kuonekana nchini tz hakuna haki.hatuwezi chagua rais sera zinazo muhusu mambo yake binafsi.
Kutetea haya mambo yahitajika kujing'oa ubongo
 
Kutetea haya mambo yahitajika kujing'oa ubongo
Si kidogo. Hawa ndiyo wale waliooshwa ubongo - brainwashed.

Si bure ile buku 7 ni ya muhimu zaidi kuliko maslahi ya taifa zima. Wako radhi hata wao wa perish Ila buku 7 isalie.

Buku 7 ni kila kitu kwao.
 
Tume wanabeba dhamana yote katika kuonyesha "haki" inatendeka.

"Haki" itarejesha mapolisi, jeshi na wana usalama tunaowaona sasa kwenye harakati mbali mbali makambini mwao kwa maisha ya kawaida.

Maalim Seif anazungumzia "haki", Lissu anazungumzia "haki" vivyo hivyo kwa wagombea wengine.

Kwanini Magufuli haongelei wala kutamka neno "haki" popote pale?

Kuna chama na washirika wao ambao wanakereka mno wanaposikia neno "haki."

Kama amani ni muhimu kwetu sote ikiwamo tume, basi tume na ituthibitishie kwa waziwazi na kwa vitendo kuwa uchaguzi huu utakuwa wa haki.

Wazanzibari na waTanganyika wameamua 2020 kuachana na CCM Mpya

22 October 2020
Zanzibar, Tanzania

Umati wa Maelfu ya Watu Zanzibar wakitoka kampeni za ACT-Wazalendo 2020

Wananchi wakitoka mkutano wa jimbo la Mwera uliofanyika Zanzibar viwanja Garagara


Maelfu ya watu wakirejea toka viwanja vya kampeni 2020 wakiwa wamebeba bendera za ACT-Wazalendo, CHADEMA , mabango yenye jumbe ULIPO TUPO, NI YEYE na bendera za taifa la Zanzibar.

Hakika haki lazima itendeke mwaka huu 2020 ndiyo amani itakuwepo. Watawala wajipime na kukubali maamuzi ya wananchi. Wasikubali kutumia vyombo vya dola kama majeshi, vikosi maalum, usalama wa taifa na mgambo au valentia kujaribu kuzuia kimbunga hiki cha 2020 cha Maalim Seif na Tundu Lissu.
Source : Swahili Villa
 
Zipo figisu figisu nyingi mno CCM hawapo tayari kukaa Benchi hata kawa watakataliwa kwenye sanduku la kura, wana hofu ya kusalia na kesi za kutumia madaraka vibaya hususani kujenga chato Airport kienyeji pasipo idhini ya bunge na pia Ndungai kutumia bilion 12 peke yake akiwa India na ufisadi mwingineo mwingi ikiwemo zile trilion 1.5 walizokwapua kisha kumtoa CAG kafara

Wasipotaka kukaa benchi kwa sanduku la kura wajue zama hizo hazipo tena.
 
22 October 2020
Pemba, Zanzibar

HOTUBA YA TUNDU LISSU, HOTUBA BORA ZAIDI ILIYOWAHI KUTOLEWA NA MGOMBEA WA URAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO VISIWANI ZANZIBAR


KIMBUNGA CHA TUNDU LISSU (CHADEMA) NA MAALIM SEIF (ACT WAZALENDO) LEO PEMBA -ZANZIBAR



Uchaguzi wa mwaka huu 2020 tunaweza kuuita Mama wa Uchaguzi wa chaguzi zote zilizopata kufanyika Tanganyika na Zanzibar nchi zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Machungu yapo mengi watu walikuwa kimya lakini sasa 2020 watu wana jambo lao kote Zanzibar na Tanganyika kutokana na ubabe wa CCM Mpya

ZANZIBAR HATARINI KUKOSA UMEME KUTOKANA NA DENI LA BILIONI 121​

Posted by Chumba-cha-Habari | Mar 6, 2017
Zanzibar hatarini kukosa umeme kutokana na deni la bilioni 121

Rais Dr. John Magufuli jana aliiagiza (Tanesco) kuwakatia umeme wateja wote wenye madeni makubwa ikiwemo serikali ya Zanzibar kutokana marimbikizo ya madeni yanayodaiwa.

Alisema kuwa Zanzibar kupitia shirika la umeme za Zanzibar (Zeco), imekua ikiongoza kwa deni la Tanesco kiasi cha shilingi bilioni 121 za Tanzania jambo ambalo linarejesha nyuma maendeleo ya TANESCO.

Akizungumzaalipokwenda kuweka jiwe la msingi kwenye kituo kipya cha Tanesco mkoani Mtwara, rais Magufuli alizitaka tasisi zote za umma kulipa madeni yao la sivyo zitakatiwa umeme haraka bila kuogopwa.

“Msiogope mnapaswa kukata huduma hii kwa taasisi yoyote ambayo hailipi bili zake.

Nataka kumwambia waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kwamba umeme unapaswa kukatwa hata Ikulu.

Nikilala gizani, halafu maafisa wa Ikulu ambao hawajalipa watawajibika na sio wewe. Una hakikisho langu kwa hili.
Pesa za kulipa bili kawaida hutolewa kwa wizara zetu, lakini badala yake hupelkwa kwingine
.
”Ninaambiwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haijalipa Sh121 billion. Ninyi (Tanesco) si wanasiasa…mnapaswa kuzingatia majukumu yenu ya kitaaluma…kata huduma ya umeme.Nimesema hata kama ni Ikulu , polisi, jeshi ama shule , hakuna mwenye deni anaepaswa kuachwa .

Ni kwa njia hii tu tunaweza kuhakikisha kwamba pesa zilizotengewa wizara kwa ajili ya umeme zinatumiwa kama ilivyopangwa ili Tanesco iweze kuendesha kazi zake na kushughulikia matatizo ya uhaba wa umeme.

”Tanesco haiwezi kuboresha huduma kwa sababu ya madeni ya serikali yasiyolipwa”.

Nae Waziri wa nchi katika ofisi ya makamu wa pili wa rais , Bwana Mohammed Aboud, alisema kuwa Maagizo ya rais Magufuli yako wazi, Madeni lazima yalipwe na yatalipwa na mipango inafanyika kwa ajili ya kuliwezesha shirika la Zeco kulipa madeni ya Tanesco.

” Tumeanza mchakato wa kuhakikishwa suala hili linatatuliwa.Pia tumeiagiza Zeco kuacha kulimbikiza madeni mapya”.



SHEIN - "Magufuli Hatimaye Kafanya Maamuzi, Amesamehe Deni"

Published on 21 Jan 2019
DKT SHEIN - "Magufuli Hatimaye Kafanya Maamuzi, Amesamehe Deni" BARAZA la mawaziri limeridhia utozwaji wa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwa kiwango cha asilimia 0% , kwenye umeme unaouzwa na shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa shirika la Umeme la Zanzibar (ZECO) na kufuta malimbikizo ya deni la kodi ya VAT lililofikia Shilingi Bilioni 22.9 kwa TANESCO kwenye umeme wa ZECO. Kwa upande wake Rais wa Zanzibar, Dkt Shein, pamoja na kuridhia utozaji wa VAT kwa kiwango cha asilimia 0%, Baraza la mawaziri pia limekubaliana kuwa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, ataitisha vikao vya kuzungumzia masuala ya Muungano kila mara kunapokuwa na hoja ya masuala ya Muungano ili kujadili na kutoa maamuzi.
 
Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo (Zanzibar), Nassor Ahmed Mazrui, amechukuwa fomu kuomba ridhaa ya chama chake kuwania uwakilishi jimbo la Mwera. Inakumbukwa kuwa Mazrui amewahi kuwakilisha jimbo la Mtoni 2005-2010 na kisha kuwania na kushinda kuwakilisha jimbo la Mtopepo kwenye uchaguzi wa Oktoba 2015. Je, kwa nini sasa amehamia Mwera? Msikilize hapa.
 
21 October 2020
Unguja, Zanzibar

Vijana na Kampeni za Maalim Seif 2020

 
Mzee afafanua methali ya kabila moja kuwa mdomo wa samaki kamongo ulimponza samaki huyo.


Kutokana na methali hiyo ya wahenga, achambua mgombea anayetaka mitano tena 2020 na kupitia yote aliyosema katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Miaka 5 ya kujinasibu wamewafanyia mengi lakini CCM Mpya imeamua kuweka mabango toka Sirari Musoma mpaka Tunduma mpakani mwa Zambia na idadi hiyo ya mabango ni mengi kuliko idadi ya madawati yote ya shule za mikoa kadhaa Tanzania. Kulikuwa na sababu gani ya kuingia gharama yote hiyo baada ya kuwepo serikalini kwa miaka 5.

Ndege bombadier na flyover za DSM imekuwa kisingizio cha kukosekana soko Pansiasi Mwanza anasema mwenyekiti wa mtaa wa CCM jijini Mwanza kilometa 1,200 toka Dar es Salaam , kweli CCM imekata pumzi, imechoka inafaa kupumzishwa 2020
 
Back
Top Bottom