Kwa kweli Kiswahili ni kigumu

Kwa kweli Kiswahili ni kigumu

sensor sio kisimbuzi ni king'amuzi

mouse (in computer set) sio kipanya, lipo jina la kiswahili, nimelisahau.

Force sio kani, ni nguvu.

Kani ni neno la kiswahili ambalo lina maana ya neno Torque katika engineering.
 
Mwaka 2007 Niliwahi kufika Kyela kwenye kijiji kimoja kinaitwa IKOLO wakati najaribu kuweka vocha nikapewa ujumbe huu Hakuna Mtandao wa Tandabui kumbe ndio No Network Coverage Kiswahili balaa
 
sensor sio kisimbuzi ni king'amuzi

mouse (in computer set) sio kipanya, lipo jina la kiswahili, nimelisahau.

Force sio kani, ni nguvu.

Kani ni neno la kiswahili ambalo lina maana ya neno Torque katika engineering.

Hayo ya sensor kama ni kisimbuzi ama ni king'amuzi nawaachia wajuvi.

Nitachangia kwenye Force, kani, torque, nguvu na yanayohusiana na hayo.

Force ni kani. Nguvu ni power. Torque sifahamu neno sahihi kwa Kiswahili. Maelezo yanafuata.

Kazi= kani X umbali ambao kile kinachosukumwa na hiyo kani kimesogea kuelekea upande uleule wa msukumo wa kani. (Work=force X distance moved in the direction of the force ). Alama hii 'X'ni alama ya kuzidisha.

Nguvu = kasi ya kufanya kazi(Nguvu =kazi/muda wa kufanya hiyo kazi). (Power is the rate at which work is done. Power=Work/Time). Alama '/'ni alama ya kugawanya.

Sasa Torque. Torque ni matokeo ya kuzidisha kani na umbali. Uelekeo wa kani na uelekeo wa huu umbali vipo perpendicular ...hahaha(hivi perpendicular kwa Kiswahili tunasemaje?). Torque is the product of force and the perpendicular distance from a fixed point to the point where the force is being applied.

Nimejaribu kueleza kadiri ya sayansi na Fizikia niliyojifunza
shule ya msingi na sekondari kwa mfuatano huohuo (yaani respectively🙂
 
Mtoa mada sijui kigumu nini hapo, mbona maneno ya kawaida sana hayo? Isipokuwa machache ambayo uwa hayatumuki sana. Hata hicho Kiingereza mnachodai ni kirahisi si hivyo, ndio maana MAhakama Kuu wasomi wenye Ph.D huwa kinawatoa jasho.
 
Maneno mengi unayoyasema ni ya kitaalamu, na huwa hayatumiki sana kwa hiyo si ajabu kuona watumiaji hawayatumii na hawayafahamu kabisa.
Lugha haipimwi kwa idadi ya msamiati wa kitaalamu anaofahamu/asiofahamu mtu bali uwezo wake wa kutumia lugha hiyo katika mawasiliano ya kila siku na ya msingi.
Kuna kundi la msamiati huitwa msamiati msingi, hakuna neno hata moja kati ya uliyoorodhesha ambalo linaingia katika kundi hili. Uwezo wa kusema lugha/umilisi huamuliwa kwa kiwango cha matumizi ya kundi hili la maneno.
 
Aksante umeniongezea maarifa,ila kwa baadhi ya maneno nikiyaongea nadhani hakuna mtu atanielewa kama KADIWIA kwa SIM CARD.
 
Mmenye...Una kadi ya kiotomela ya benki gani...?

Nilihitaji kununua mweko mbili, mdaki mmoja na vinukuzi viwili..nikaenda mpaka kwenye kiotomotela ya Benki ya Ushirika na Maendeleo vijini; ile nataka kufanya muamala si nikastuka nywila yangu nimeisahau!!!!
 
Bado unasema Kiswahili ni lugha nyepesi eti kwa kuwa tunaelewana tu!!!?Tazama.......
KIINGEREZA------KISWAHILI
Device-------------Kitumi
Photocopier------Kinukuzi...
Duplicating Machine --Kirudufu
Resistor-----------kikinzani
Power Saw-------Msumeno oto
Sensor-----------Kisimbuzi
Lap Top---------Kipakatalishi
ICU--------------Kisadaruki
Microwave-----Tanuri ya miyale
Memory Card-----------Kadi sakima
SIM card----------Kadiwia/mkamimo
Scratch card------------Kadi hela
Business card-----Kadikazi
Identity card----Kitambulisho
ATM---------- -Kiotomotela
Nutrients ----- -Virutubisho
Starch---------- ---------Nisha
Stigma--------- ----------Ntwe
Nectar---------------Mbochi
Humus---------------Mboji
Germ cell----------Celizazi
Femur---------------Fupaja
Green house-------Kivungulio
Esophagus--------------Umio
Sunflower---------------Alizeti
Weevil-------------Fukusi/dumuzi
Distillation--------Ukenekaji
Evaporation-------Mvukizo
Dissolve ----------Uyeyushaji
Stagnant----------------Tuame
Synthesis---------Uoanishaji
Monitor-----------Muwazi
Processor---------Kichakato
Computer Virus-----Mtaliga
Floppy Disk-------------Diski tepetevu
Mouse-----------Kipanya/kisakura
Slot----------------Upenyu
Flash Disk--------------Diski mweko
Scanner-----------------Mdaki
Keyboard-------Kicharazio
Force of Gravity-------Kani ya mvutano
Certificate-----Astashahada
Diploma--------Stashahada
Degree------------Shahada
Masters----------------Uzamili
Phd----------------Uzamivu
Sausage---------------Soseji
Kebab-------------Mshakiki
Crisps--------------Kaukau
Chips-------------------Vibanzi
Juice---------------Sharubati
Password--------------Nywila
Zebra Crossing-------Kivuko milia

Afadhali kuchanganya lugha kwa kweli, tukiongea Kiswahili bila kukopa maneno hatutaelewana kabisa.



Umetisha sana mkuu, tujivunie nakujielimisha zaidi tu ndiyo lugha yetu.
 
Back
Top Bottom