Kwa Maamuzi haya ya hatima ya Sakata la Mchezaji Bernard Morrison ambayo 'yanahisiwa' yanaendelea 'Kuamuliwa' Kesho nani 'ataathirika' zaidi?

Kwa Maamuzi haya ya hatima ya Sakata la Mchezaji Bernard Morrison ambayo 'yanahisiwa' yanaendelea 'Kuamuliwa' Kesho nani 'ataathirika' zaidi?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
UTANGULIZI
Kama hujaelewa au huelewi maana ya neno la Kiswahili la 'yanahisiwa' tafadhali mtafute Mtu akueleweshe kuliko 'Kuukurupukia' huu Uzi tafadhali.

UDUKUZI ULIOFANYIKA
Baada ya Sakata zima la huyu Mchezaji Bernard Morrison ambalo hadi leo halijatolewa Maamuzi kuanza kuonyesha kuwa kumbe 'Mkosaji' wa Kwanza ni Shirikisho lenyewe la Soka nchini Tanzania (TFF) kutokana na kwamba 'Watendaji' wake ndiyo wamehusika kwa 100% na huu 'Upuuzi' wote.

KAMATI HUSIKA NA MPANGO MZIMA WA KUILINDA TFF
Ni kwamba kinachoendelea sasa baada ya Kikao cha Jana ambacho pia kimeendelea leo na kimelala tena 'Kugundua' kuwa TFF ni 'Mkosaji' Mkuu wanachohangaika kufanya sasa ni kutaka 'Kujilinda' Wao kama Wao kwa 'Gharama' ya 'Kuzikandamiza' Klabu za Simba na Yanga ili wao ( TFF ) wabaki salama na mambo yaende.

MAAMUZI YANAYOHISIWA KWENDA KUTOLEWA KESHO JUU YA SAKATA HILI ZIMA
Za chini ya Kapeti zinasema kwamba ili TFF 'Kujilinda' na 'Lawama' dhidi yao na ili kuweka na kuleta 'Usawa' na Kushusha 'Presha' za Mashabiki wa Vilabu Vikongwe viwili nchini Simba na Yanga watakachoamua Kesho ni moja kati ya haya Mambo mawili ambayo nayaweka hapa chini...

1. Mchezaji Bernard Morrison Kufungiwa kwa muda usiojulikana kwa Kusaini Vilabu viwili
2. Mchezaji Bernard Morrison Kuhusishwa na Uhalifu na Udanganyifu hivyo kutakiwa kutocheza Soka nchini Tanzania
3. Usajili wa Mchezaji Bernard Morrison ulikiukwa na Vilabu Vikongwe viwili hivyo yupo Huru na aamue Yeye Timu ya Kuichezea

OMBI LANGU KUBWA KWA SERIKALI KUPITIA WIZARA HUSIKA
Kama itawapendeza naiomba 'Serikali' iimulike kwa Jicho Kali TFF na Kamati zake kwani inavyoonekana huko kuna 'Madudu' yasiyovumilika kabisa.

NENO LANGU LA KUMALIZIA
Soka la Tanzania litakuwa na Tija na Mafanikio pale tu huu 'Usimba' na 'Uyanga' utakufa lakini pia Timu hizi 'Kudekezwa' vilivyo na Serikali Kisiasa.
 
Kwenye Namba tatu hapo labda nikupe hints kdg, Endapo huyo Morison alikula hela ya Ku extend kweli mkataba na Yanga unadhan wana Yanga watakubali awe huru tu, na je endapo alikula hela ya mkataba mpya na simba na akasema anaenda Yanga je
 
Kwenye Namba tatu hapo labda nikupe hints kdg, Endapo huyo Morison alikula hela ya Ku extend kweli mkataba na Yanga unadhan wana Yanga watakubali awe huru tu, na je endapo alikula hela ya mkataba mpya na simba na akasema anaenda Yanga je

Nimeanza na ANGALIZO hapo juu kwa kusema kuwa kama huelewi maana ya neno 'yanayohisiwa' mtafute Mtu akueleweshe. Haukunielewa Mkuu?
 
Hilo la kuchagua timu ya kuchezea KATU yanga hatulikubali.

Na Maamuzi yakitolewa kwa 'Kuifaidisha' Yanga SC zaidi Simba SC nao hawatakubali kwani nao wana 'Ushahidi' hivyo TFF ndiyo itaumbuka vibaya.
 
Na waambie tu kuwa hilo halitokuja kutokea kwani Mo Dewji anaihitaji zaidi Simba SC 'Kibiashara' kuliko ambavyo Simba SC inamuhitaji Kiudhamini.
Kitu kingine Mo hafanyi hisani kama GSM yupo pale kimkataba.
 
Kuna Watu hapa huwa 'mnanilazimisha' niwajibu vibaya kisha 'mkasirike' tu kama kawaida yenu. Hivi niliposema 'yanayohisiwa' umenielewa lakini?
Hilo la kuhisiwa ipo kwenye hii ramli mpya. Vipi ule uzi wako wa mwanzoni ni batili? Maana ulituaminisha kuwa umepata taarifa kutoka vyanzo vyako nyeti kabisa na ukatupa na hatima ya maamuzi ambayo bila shaka yamekinzana na uzi huu mpya.
 
Kwenye Namba tatu hapo labda nikupe hints kdg, Endapo huyo Morison alikula hela ya Ku extend kweli mkataba na Yanga unadhan wana Yanga watakubali awe huru tu, na je endapo alikula hela ya mkataba mpya na simba na akasema anaenda Yanga je
Siku ambayo morrison alipeleka mkataba wake tff Yanga wakamuingizia milioni70 morisson.akawataka bank.wazirudishe zilikotoka

Sent from my M4 using JamiiForums mobile app
 
Kitu kingine Mo hafanyi hisani kama GSM yupo pale kimkataba.
Kitu kingine Mo hafanyi hisani kama GSM yupo pale kimkataba.
acha kujidanganya hakuna mkataba unaombana MO kuondoka simba, ndio maana alitoa taarifa ya kuachana na simba twitter na hakuna kiongozi wa simba aliesema amekiuka mkataba zaidi ya kwenda kumpigia magoti arudi..
 
Back
Top Bottom