Kwa Maamuzi haya ya hatima ya Sakata la Mchezaji Bernard Morrison ambayo 'yanahisiwa' yanaendelea 'Kuamuliwa' Kesho nani 'ataathirika' zaidi?

Kwa Maamuzi haya ya hatima ya Sakata la Mchezaji Bernard Morrison ambayo 'yanahisiwa' yanaendelea 'Kuamuliwa' Kesho nani 'ataathirika' zaidi?

acha kujidanganya hakuna mkataba unaombana MO kuondoka simba, ndio maana alitoa taarifa ya kuachana na simba twitter na hakuna kiongozi wa simba aliesema amekiuka mkataba zaidi ya kwenda kumpigia magoti arudi..
Ni kweli alijiondoa ila si kama ulivyoelewa Mo alijiondoa kama Mkurugenzi wa Bodi ya wadhamini ila si kama mdhamini, jua tofauti kati ya hizo kauli.
 
ndicho kitakachotokea, tff wakisema morison ana mkataba na yanga. yanga lazima waishtaki simba kwa kusajili mchezaj wenye mkataba nao, hapo ndio mo atakapoondoka rasmi
Hahahhahaha....kwani ikitokea mchezaji amesajiliwa akiwa na mkataba adhabu yake ni ipi?zaidi ya ile faini Kama yanga aliyopigwa kwa kessy?
 
Hilo la kuhisiwa ipo kwenye hii ramli mpya. Vipi ule uzi wako wa mwanzoni ni batili? Maana ulituaminisha kuwa umepata taarifa kutoka vyanzo vyako nyeti kabisa na ukatupa na hatima ya maamuzi ambayo bila shaka yamekinzana na uzi huu mpya.

Foolish.
 
Hahahhahaha....kwani ikitokea mchezaji amesajiliwa akiwa na mkataba adhabu yake ni ipi?zaidi ya ile faini Kama yanga aliyopigwa kwa kessy?
Ni kweli alijiondoa ila si kama ulivyoelewa Mo alijiondoa kama Mkurugenzi wa Bodi ya wadhamini ila si kama mdhamini, jua tofauti kati ya hizo kauli.
NO, alijiondoa kujihusisha na mambo yote ya timu ya wakubwa ikiwepo udhamini, akabaki na timu ya vijana. mpaka sasa ivi hajulikani kama ni mdhamini au shareholder, hapo ndio ujue simba inaendeshwa kihuni huni
 
Hahahhahaha....kwani ikitokea mchezaji amesajiliwa akiwa na mkataba adhabu yake ni ipi?zaidi ya ile faini Kama yanga aliyopigwa kwa kessy?
kwa mujibu wa kanuni za fifa, adhabu yake ni kufungiwa kusajili kwa miaka 3, sasa yanga wakipeleka malalamiko fifa ndio kitakachotokea hicho.
 
NO, alijiondoa kujihusisha na mambo yote ya timu ya wakubwa ikiwepo udhamini, akabaki na timu ya vijana. mpaka sasa ivi hajulikani kama ni mdhamini au shareholder, hapo ndio ujue simba inaendeshwa kihuni huni
Haya bhana GSM yupo pale kama mdhamini wa jezi tu. Mengine anayofanya ni hisani, kama unataka kujua zaidi Eng Hersi hana mkataba na Yanga kwa lolote ila ndio anaesajili wachezaji. .. hapo ndio utajua huko Yanga ndio hakuna kitu kabisa
 
kwa mujibu wa kanuni za fifa, adhabu yake ni kufungiwa kusajili kwa miaka 3, sasa yanga wakipeleka malalamiko fifa ndio kitakachotokea hicho.

Yanga SC watapelekaje FIFA Hukumu ambayo TFF imetoa na kuonekana kuwa Yanga SC ilikosea? Hivi ukuificha tu huu 'Upumbavu' wako utakufa?
 
Haya bhana GSM yupo pale kama mdhamini wa jezi tu. Mengine anayofanya ni hisani, kama unataka kujua zaidi Eng Hersi hana mkataba na Yanga kwa lolote ila ndio anaesajili wachezaji. .. hapo ndio utajua huko Yanga ndio hakuna kitu kabisa

Na Wewe 'unaniangusha' Mkuu ni kwanini unapoteza muda wako na huyo 'Popoma' hapa? Walishaitwa Nyani, Mbwa na Sokwe na Eymael au hujui?
 
acha kujidanganya hakuna mkataba unaombana MO kuondoka simba, ndio maana alitoa taarifa ya kuachana na simba twitter na hakuna kiongozi wa simba aliesema amekiuka mkataba zaidi ya kwenda kumpigia magoti arudi..
Mo hakusema anaondoka Simba...alisema atafanya tu yale waliyo kubaliana kwenye mkataba na si hisani nyingine anazotoa...kama GSM walivyotaka tu kubaki kwenye mkataba wao wa jezi baada ya kutofautiana na Yanga...kwani hayo mambo mengine anafanya kwa hisani tu,ikiwemo usajili.

Kwanini hamsikilizi habari kwa umakini?
 
Mkuu ndio wenzetu hawa...... tunaishi nao kwa maarifa

Sokwe, Mbwa na Nyani FC ( Yanga SC ) watakuwaje tena ni Wenzetu Mkuu? Labda ni Wenzako Wewe kama Wewe, ila siyo Sisi Wana Simba Mkuu.
 
UTANGULIZI
Kama hujaelewa au huelewi maana ya neno la Kiswahili la 'yanahisiwa' tafadhali mtafute Mtu akueleweshe kuliko 'Kuukurupukia' huu Uzi tafadhali.

UDUKUZI ULIOFANYIKA
Baada ya Sakata zima la huyu Mchezaji Bernard Morrison ambalo hadi leo halijatolewa Maamuzi kuanza kuonyesha kuwa kumbe 'Mkosaji' wa Kwanza ni Shirikisho lenyewe la Soka nchini Tanzania (TFF) kutokana na kwamba 'Watendaji' wake ndiyo wamehusika kwa 100% na huu 'Upuuzi' wote.

KAMATI HUSIKA NA MPANGO MZIMA WA KUILINDA TFF
Ni kwamba kinachoendelea sasa baada ya Kikao cha Jana ambacho pia kimeendelea leo na kimelala tena 'Kugundua' kuwa TFF ni 'Mkosaji' Mkuu wanachohangaika kufanya sasa ni kutaka 'Kujilinda' Wao kama Wao kwa 'Gharama' ya 'Kuzikandamiza' Klabu za Simba na Yanga ili wao ( TFF ) wabaki salama na mambo yaende.

MAAMUZI YANAYOHISIWA KWENDA KUTOLEWA KESHO JUU YA SAKATA HILI ZIMA
Za chini ya Kapeti zinasema kwamba ili TFF 'Kujilinda' na 'Lawama' dhidi yao na ili kuweka na kuleta 'Usawa' na Kushusha 'Presha' za Mashabiki wa Vilabu Vikongwe viwili nchini Simba na Yanga watakachoamua Kesho ni moja kati ya haya Mambo mawili ambayo nayaweka hapa chini...

1. Mchezaji Bernard Morrison Kufungiwa kwa muda usiojulikana kwa Kusaini Vilabu viwili
2. Mchezaji Bernard Morrison Kuhusishwa na Uhalifu na Udanganyifu hivyo kutakiwa kutocheza Soka nchini Tanzania
3. Usajili wa Mchezaji Bernard Morrison ulikiukwa na Vilabu Vikongwe viwili hivyo yupo Huru na aamue Yeye Timu ya Kuichezea

OMBI LANGU KUBWA KWA SERIKALI KUPITIA WIZARA HUSIKA
Kama itawapendeza naiomba 'Serikali' iimulike kwa Jicho Kali TFF na Kamati zake kwani inavyoonekana huko kuna 'Madudu' yasiyovumilika kabisa.

NENO LANGU LA KUMALIZIA
Soka la Tanzania litakuwa na Tija na Mafanikio pale tu huu 'Usimba' na 'Uyanga' utakufa lakini pia Timu hizi 'Kudekezwa' vilivyo na Serikali Kisiasa.
kwa njia yoyote ile, kutuliza hili fukuto ni lazima Morrison afungiwe, bila hivyo hii case haitaisha leo wala kesho.
 
Na Maamuzi yakitolewa kwa 'Kuifaidisha' Yanga SC zaidi Simba SC nao hawatakubali kwani nao wana 'Ushahidi' hivyo TFF ndiyo itaumbuka vibaya.
Morrison alisajiliwa na yanga wakati dirisha dogo la usajili likiwa limefungwa. TFF ndiyo wa kuwajibika Kwa upuuzi wao. Sasa basi Kamati iamue Tu kuwa mchezaji hakuwa halali kucheza ligi, points Kwa mechi alizocheza ziondolewe tujue kama ni playoff au religation.
 
kwa mujibu wa kanuni za fifa, adhabu yake ni kufungiwa kusajili kwa miaka 3, sasa yanga wakipeleka malalamiko fifa ndio kitakachotokea hicho.
FIFA watataka details za kutosha kuhusu alisajiliwa lini na ilikuwa ndani ya muda! Hapo ndipo Kamati inachoogopa kukisema kuwa tff walikula mrungula ili kupitisha usajili nje ya dirisha la usajili.
 
FIFA watataka details za kutosha kuhusu alisajiliwa lini na ilikuwa ndani ya muda! Hapo ndipo Kamati inachoogopa kukisema kuwa tff walikula mrungula ili kupitisha usajili nje ya dirisha la usajili.
Kwani shauri lilioko mezani nila miaka 2 au miezi6?
 
Back
Top Bottom