Kwa mafao haya manono ya wabunge ukilinganisha na ya watumishi wa umma, tukisema wabunge ni wabinfsi tunakosea?

Kwa mafao haya manono ya wabunge ukilinganisha na ya watumishi wa umma, tukisema wabunge ni wabinfsi tunakosea?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
MAFAO YA KIINUA MGONGO; WABUNGE WANAOGELEA.

Kiinua mgongo kwa mbunge mmoja wa Bunge la Tanzania ni Sh272 milioni baada ya kipindi cha miaka 5 akihudumu kama mbunge wa Bunge la Tanzania.

Jumla ya idadi yote ya wabunge ni 393. Wabunge wa majimbo ni 264. Wabunge wa viti maalum ni 113. Wabunge kutoka katika baraza la wawakilishi ni 5.

Wabunge wa kuteuliwa na Rais ni 10. Mwanasheria Mkuu wa Serikali 1. Jumla ya wabunge wote katika Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania ni 393.

Ukichukua kiinua mgongo Sh272 milioni ukazidisha kwa jumla ya idadi ya wabunge wote katika Bunge la Tanzania 393 unapata Sh106,896,000,000.

Malipo ya kiasi cha shilingi 272 milioni kwa kila mbunge kama mafao ya kustaafu, ni sawa na madawati 1,916 kwa bei ya shilingi 120,000 kwa dawati moja.

Kiasi hicho cha fedha za umma kinaweza kujenga nyumba tano za walimu. Kiinua mgongo cha wabunge 393 kinaweza kujenga nyumba 1,965 za walimu

.Lakini mbunge mmoja katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atapata kwa kufanya kazi miaka 5 akiwa bungeni akigonga meza kutetea Serikali.Wakati waliostaafu

Bunge la 8 lililoongozwa na Spika Pius Msekwa, wabunge waliokuwepo bungeni walilipwa mafao ya kustaafu shilingi 20 milioni kila mmoja.

Bunge la 9 lililokuwa likiongozwa na Spika Samuel Sitta, wabunge waliokuwepo katika bunge hilo walilipwa mafao ya kustaafu shilingi milioni 72 kila mmoja

.Bunge la 10 lililoongozwa na Spika Anna Makinda, wabunge waliokuwepo bungeni walilipwa mafao ya kustaafu, shilingi 230 milioni kwa kila mbunge.

Bunge la 11 lililoongozwa na Job Ndugai, wabunge waliokuwepo katika bunge hilo walilipwa mafao ya kustaafu, shilingi 272 milioni kwa kila mbunge.

Malipo ya kustaafu yanajumuisha kiinua mgongo (gratuity) hii ni 40% ya malipo ya mshahara ya mbunge katika jumla ya kipindi alichotumikia bungeni.

Posho ya hitimisho la kazi (winding up allowance) ambayo ni 40% ya kiinua mgongo), posho ya usumbufu (relocation allowance) 40% ya kiinua mgongo.

Pia, inajumuisha posho ya mpito (transitional allowance). Mishahara ya mbunge ya miezi 3 na mafao ya utumishi wa mbunge. Wanaogelea mapesa.

Mafao ya Uzeeni hulipwa kwa Mwanachama aliyetimiza umri wa kustaafu kwa mujibu wa Sheria ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma ya 2018.

Awe Mwanachama wa PSSSF. Awe amechangia kwenye Mfuko kwa kipindi kisichopungua miezi 180 au miaka 15. Awe ametimiza umri wa kustaafu kisheria,

Mwanachama mstaafu aweze kupata Pensheni ya Uzeeni, inabidi kuwasilisha fomu PS-BEN.1 ambayo imejazwa vyema pamoja na viambatanisho.

Umri wa kustaafu kwa hiari wa miaka 55 na kwa lazima ni miaka 60. Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anahitaji miaka 5 tu kulipwa mafao.

MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila.

Kiutoka mtandao wa X
 
Anafahamu tofauti ya watawala (viongozi wa wananchi) na watendaji (watumishi wa umma)

Hilo kwanza analifahamu?
 
Tuje na mkakati wa kuwa na wabunge wa kujitolea siyo hawa wa kuuana ili waingie madarakani, hivi sasa kuna vijana wengi wasomi, wenye uzalendo na wabunifu hawana kazi, hao ndiyo wangefanya hiyo kazi kwa malipo ya kawaida kama watumishi wengine
 
Kama kuwa mbunge kunalipa kiasi hicho, kwanini na yeye Maranja Masese (kwa kiswahili maana yake MBWA) asifanye utaratibu akawa mbunge (kiongozi wa wananchi) akafute hizo posho na pensheni ili bunge liwe chombo cha kujitolea?
 
Tuje na mkakati wa kuwa na wabunge wa kujitolea siyo hawa wa kuuana ili waingie madarakani, hivi sasa kuna vijana wengi wasomi, wenye uzalendo na wabunifu hawana kazi, hao ndiyo wangefanya hiyo kazi kwa malipo ya kawaida kama watumishi wengine
Nina Imani duniani Kate wabunge wanajitolea. Hivyo tumechelewa sana kufika huko.

Tuanze sasa, katika mapambano ya katiba mpya hili nalo tuliweke, na Rais pia awe anajitolea.

Hii wenzangu watanzania mnaionaje?
 
Kama kuwa mbunge kunalipa kiasi hicho, kwanini na yeye Maranja Masese (kwa kiswahili maana yake MBWA) asifanye utaratibu akawa mbunge (kiongozi wa wananchi) akafute hizo posho na pensheni ili bunge liwe chombo cha kujitolea?
Unaleta jibu jepesi kwa hoja fikirishi, yaani hii ni typical CCM style, kwa vile hoja imetoka kwa mpinzani basi wajibu wao ni kuipinga tena kwa kejeli.
 
Kama kuwa mbunge kunalipa kiasi hicho, kwanini na yeye Maranja Masese (kwa kiswahili maana yake MBWA) asifanye utaratibu akawa mbunge (kiongozi wa wananchi) akafute hizo posho na pensheni ili bunge liwe chombo cha kujitolea?
Umeishia darasa la ngapi?
 
Kama kuwa mbunge kunalipa kiasi hicho, kwanini na yeye Maranja Masese (kwa kiswahili maana yake MBWA) asifanye utaratibu akawa mbunge (kiongozi wa wananchi) akafute hizo posho na pensheni ili bunge liwe chombo cha kujitolea?
Nyie UWT ni wajinga sn nchi inatafunwa na wachache nyie mnaishia kununuliwa pombe, nyama na ngono
 
Yawezekana ni kweli hawa wabunge ni wabinafsi sana. Ila tujaribu kuvaa viatu vyao hasa nyakati wanapotafuta huo ubunge.

Tujiulize
Huwa wanatumia kiasi gani kuupata huo ubunge?

Pesa wanazopatia vikundi vya kina mama, bodaboda, machinga, mabonanza, Kanga, fulana, kofia n.k huwa wanazitoa wapi na wanazirudisha vipi?

Kwanini huwa wako tayari kutoa kiasi chochote cha pesa ama kufanya jambo lolote ili mradi washinde?

Huwa wanatarajia nini kwenye huo ubunge?

Kwanini huwa tunafurahia kupewa pesa na vitu vya bure wakati wa kampeni na uchaguzi?
Je, hiyo bure ni bure kweli?

Je, hatuwezi kuchagua viongozi bila kupata chochote kitu kutoka kwao?

Kwanini wengi wao wakigombea na kushindwa huwa wanarudi chini kiuchumi kama siyo kufirisika kabisa?

Kwanini kila tunayemchagua kuwa mbunge tabia ni zile zile bila kujali chama anachotokea?

Je, hawa wabunge wanatoka kwenye jamii zetu ama jamii za nje?

Huu ubinafsi na urafi huwa wanajifunza kabla ya kuwa wabunge ama baada ya kuwa wabunge?

Je, sisi tunaolalamika hatuna ubinafsi? Siyo warafi?

Ama tunalalamika kwasababu tumekosa fursa ya kuonyesha ubinafsi na urafi wetu?

Binafsi naamini mfumo wa kuwapata wabunge unatatizo kubwa, hivyo lazima wabunge pia wawe na matatizo na sisi wananchi ni sehemu ya hilo tatizo, hivyo tusiishie kulalamika bali tuwe sehemu ya suluhisho la hili tatizo. Kulalamika kwetu hakutobadilisha chochote, ndio maana kadri tunavyolalamika maslahi ya wabunge yanaongezeka badala ya kupungua.
 
MAFAO YA KIINUA MGONGO; WABUNGE WANAOGELEA.

Kiinua mgongo kwa mbunge mmoja wa Bunge la Tanzania ni Sh272 milioni baada ya kipindi cha miaka 5 akihudumu kama mbunge wa Bunge la Tanzania.

Jumla ya idadi yote ya wabunge ni 393. Wabunge wa majimbo ni 264. Wabunge wa viti maalum ni 113. Wabunge kutoka katika baraza la wawakilishi ni 5.

Wabunge wa kuteuliwa na Rais ni 10. Mwanasheria Mkuu wa Serikali 1. Jumla ya wabunge wote katika Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania ni 393.

Ukichukua kiinua mgongo Sh272 milioni ukazidisha kwa jumla ya idadi ya wabunge wote katika Bunge la Tanzania 393 unapata Sh106,896,000,000.

Malipo ya kiasi cha shilingi 272 milioni kwa kila mbunge kama mafao ya kustaafu, ni sawa na madawati 1,916 kwa bei ya shilingi 120,000 kwa dawati moja.

Kiasi hicho cha fedha za umma kinaweza kujenga nyumba tano za walimu. Kiinua mgongo cha wabunge 393 kinaweza kujenga nyumba 1,965 za walimu

.Lakini mbunge mmoja katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atapata kwa kufanya kazi miaka 5 akiwa bungeni akigonga meza kutetea Serikali.Wakati waliostaafu

Bunge la 8 lililoongozwa na Spika Pius Msekwa, wabunge waliokuwepo bungeni walilipwa mafao ya kustaafu shilingi 20 milioni kila mmoja.

Bunge la 9 lililokuwa likiongozwa na Spika Samuel Sitta, wabunge waliokuwepo katika bunge hilo walilipwa mafao ya kustaafu shilingi milioni 72 kila mmoja

.Bunge la 10 lililoongozwa na Spika Anna Makinda, wabunge waliokuwepo bungeni walilipwa mafao ya kustaafu, shilingi 230 milioni kwa kila mbunge.

Bunge la 11 lililoongozwa na Job Ndugai, wabunge waliokuwepo katika bunge hilo walilipwa mafao ya kustaafu, shilingi 272 milioni kwa kila mbunge.

Malipo ya kustaafu yanajumuisha kiinua mgongo (gratuity) hii ni 40% ya malipo ya mshahara ya mbunge katika jumla ya kipindi alichotumikia bungeni.

Posho ya hitimisho la kazi (winding up allowance) ambayo ni 40% ya kiinua mgongo), posho ya usumbufu (relocation allowance) 40% ya kiinua mgongo.

Pia, inajumuisha posho ya mpito (transitional allowance). Mishahara ya mbunge ya miezi 3 na mafao ya utumishi wa mbunge. Wanaogelea mapesa.

Mafao ya Uzeeni hulipwa kwa Mwanachama aliyetimiza umri wa kustaafu kwa mujibu wa Sheria ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma ya 2018.

Awe Mwanachama wa PSSSF. Awe amechangia kwenye Mfuko kwa kipindi kisichopungua miezi 180 au miaka 15. Awe ametimiza umri wa kustaafu kisheria,

Mwanachama mstaafu aweze kupata Pensheni ya Uzeeni, inabidi kuwasilisha fomu PS-BEN.1 ambayo imejazwa vyema pamoja na viambatanisho.

Umri wa kustaafu kwa hiari wa miaka 55 na kwa lazima ni miaka 60. Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anahitaji miaka 5 tu kulipwa mafao.

MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila.

Kiutoka mtandao wa X
Gombea ubunge nawewe! Uchawi na umaskini utakuua.
 
Kwa kifupi wabunge ni wakoloni weusi. Tofauti na wale waliowatesa mababu zetu ni kuwa wale walikuja kwa meli hawa weusi wamezaliwa hapa hapa na wananchi masikini wanalazimika kuwapigia kura kuingia bungeni kutunga sheria za ajabu ajabu za kuwanufaisha wao tu. Bata wahed!
 
Back
Top Bottom