Kwa majibu haya ya daktari nina hofu na afya yangu

Kwa majibu haya ya daktari nina hofu na afya yangu

wiki iliyopita nilikwenda hospitali ambayo ni private, ni baada ya kutojisikia vizuri kiafya, baada ya maelezo yangu ilionekana nipime malaria (bs) pia dr akaandika na kipimo kingine kilichosomeka correctol katika karatasi lao. Majibu yalipotoka, kwenye bs ilikuwa nil lakini hiki kipimo kingine kiliandikwa positive. Na niliambiwa hicho ni kipimo cha typhoid. Nikahoji hiyo typhoid iko ngapi? Wakasema haionyeshi ni ngapi na nikitaka kujua ni ngapi ni mpaka vipimo vikae masaa 24. Naombeni msaada kwa wanaojua haya mambo napata hofu isije kuwa ni positive ya hiv na pengine nimedanganywa tu kuambiwa ni typhoid asanteni

h.i.v cku hizi hawafichi kabisa wangekuambia wanakuogopa nini? Achana na hizo hofu za kujijengea.
 
Naona kuna vitu vinanichanganya hapa.

Wewe uliona nini hasa..chorrectol au chorestol? Maana umetumia maneno yote mawili interchangably. Maana kama huna hakika na nini hasa kilichokuwa kwenye hilo karatasi,huna sababu ya kumlaumu huyo dr wako..maana pengine alialichoandika kiko sahihi ila wewe ndiye uliona vibaya.

Pili umesema hospitali hiyo inatumia cheap labours.Inanipa shida kidogo kujua ni busara gani ilitumika kwenda kule ilhali unaelewa kuwa hakuna cha maana kinachoweza kufanyika na cheap labours..na hayo ndiyo uliyategemea.

Mimi nadhani tunapokuwa tunamlaumu huyo dr wako,ni vema pia na wewe ukajitathmini uhusika wako katika kadhia hii.

Niliona hilo neon la pili yaani chorestol, mwanzo nilichanganya spelling, fani za watu hizo, Pili nimesema cheap labour, ni kweli na nilikwenda hapo kwa sababu mimi ni mfanyakazi wa kampuni na kampuni yetu imeingia mikataba na hizi hosp za private, na ukiingalia kwa haraka haraka mjengo ni wa uhakika, lakini ukija kwa upande wa wafanyakazi ni majanga imekuwa ni mahali pa kufanyia field za kila kitengo hasa manesi na ma dr kwa uchache. au dr anaekosa ajira serialini pale hakoso kazi..vile2 nilijiahidi kuto kutibiwa hapo baada ya miaka ya nyuma kutaka kuua mtt wangu mdogo 9 months kwa kutaka kumchoma sindano ya ugonjwa ambao hakuwa nao, thanks to God kwamba pamoja na kulazimisha kwa means zote za kutafuta mshipa zilishindikana, ndiyo ilikuwa pona pona yangu. ni kwa muda mrefu saaana sijaenda pale, sasa juzi naenda mimi tena naambiwa juu juu tu kwamba eti POSITIVE na nijuavyo mimi typhoid ina viwango tofauti tofauti. hosp iko karibu na kibaruani kwangu pia niliona ni tatizo ambalo ni dogo lingeweza kupatiwa ufumbuzi bila complication kama hizo za ku generalize maadam ni bacteria haimpi uhalali dr kuandika majibu ya jumla kama mafungu ya nyanya sokoni. asante
 
h.i.v cku hizi hawafichi kabisa wangekuambia wanakuogopa nini? Achana na hizo hofu za kujijengea.

Ni kweli mkuu wangeniambia, ila tu pale endapo ningekuwa na utayari wa kuambiwa, japo najua sana kuwa wanatupima kila siku tuendapo kutibiwa na hawatuambii kwa kuwa tunakuwa hatuko tayari kupokea majibu ambayo ni positive, naamini wao wana symbols zao wanazozitumia ambazo sisi tunakuwa hatuzijui. eti wanakusanya data ambazo mimi nasema ni wrong data.
 
ahaaaaaa 3bora nimecheka thana mm ni mbili bora

Kama ni kweli basi wewe ni sawa sawa na mimi na nadhani tungefahamiana tungeelewana vizuri maana ndege wafananao huruka pamoja.
 
Back
Top Bottom