Kwa maneno na matendo yake, Rais Samia alikuwa njiapanda wakati wa Hayati Magufuli?

Kwa maneno na matendo yake, Rais Samia alikuwa njiapanda wakati wa Hayati Magufuli?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Kila mmoja sasa anajua kuwa Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa Makamu wa Rais wa Mwendazake Hayati Dr. John Pombe Magufuli. Tunajua pia kuwa Rais Samia alichaguliwa kwa kura zilezile za Mwendazake mwaka 2015 na 2020. Alikuwa msaidizi nambari moja wa Mwendazake. Lakini, kikatiba Mwendazake ndiye aliyekuwa akisema na kutenda yote ya maamuzi ya mwisho. Mama sasa ndiye muamuzi wa mwisho.

Pamoja na kusema tena na tena kuwa yeye na Mwendazake ni kitu kimoja, Rais Samia anajipambanua kimaneno na kimatendo kuwa yu tofauti na Mwendazake. Anasema na kutenda tofauti na Mwendazake, angalau kwa muda huu mfupi wa Urais wake. Yeye si muumini wa 'matumizi ya nguvu' kwenye mambo ambayo hata hayakuhitaji matumizi ya nguvu. Yeye ni muumini wa hoja kabla ya uamuzi wa haja.

Yeye havumilii 'ulevi wa madaraka' wa wateule wake ambao wakati ule walilewa na kuwa miungu-watu katika sehemu zao za kiutawala. Anajipamanua kama mpenda demokrasia na maridhiano badala ya kutumia 'amri na nguvu' tu wakati wote wa kusema na kutenda. Hadi hapo, kuna tofauti kati yake na Mwendazake. Kujifananisha na kutuaminisha kuwa wao ni kitu kimoja kile kile ni mambo ya siasa tu.

Sasa, kubadili ni kurekebisha. Kurekebisha ni kutokukubaliana na kilichokuwepo. Kutokukubaliana halafu kutokuwa na uwezo wa kubadili, kupinga au kushauri ipasavyo ni maumivu makubwa. Amini nawaaambia, kwa maneno na matendo yake, Rais Samia alikuwa njiapanda wakati wa Mwendazake. Alikuwa akiishi kwenye maumivu yasiyomithilika. Sasa ana amani na utulivu wa moyo. Anasonga mbele akitekeleza anayoyaamini na aliyokuwa akiyatamani yafanyike wakati ule.

Mama Samia, tupo pamoja kwenye hoja!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
 
Hili ni kweli na linazaa hoja nyingine: Kuna umuhimu mkubwa kabisa wa kubadilisha katiba, ili kama rais aliyepo madarakani atashindwa kuendelea na kazi, basi uitishwe uchaguzi mwingine mpya.

Hii ni kwa sababu kama wananchi walimpa Magufuli kura kwa kuamini approach na misimamo yake ya kufanya kazi, basi sasa hivi tumepata mtu ambaye ni tofauti kabisa na anafanya mambo tofauti kabisa na mtangulizi wake.
 
Kila mmoja sasa anajua kuwa Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa Makamu wa Rais wa Mwendazake Hayati Dr. John Pombe Magufuli....
Ipo siku, utawaza unafki au kuandika unafki juu ya mama. Ila unaa ukizidi uchawi unakaribia.
 
Nina Msalimia Mama wa Taifa kwa Jina la Jamuhuri ya Muungano Wa Tanzania!

Na kazi ziendelee maana zilikwama!
 
Foka Foka Imeenda na mwendazake. Kiongozi ni Kukubali kushauriwa nadhani aliyeendazake Kushauriwa ilikuwa kama kutukanwa.
 
Yes, she's different.

Japo ni CCM ile ile na mtu humezwa na mfumo iwe mbaya au mzuri, lakini at least huyu "kitabia" anaonesha amelelewa vizuri, kuheshimu utu wa mtu.

Mwendazake Magufuli alikuwa ni tatizo kuanzia kwenye culture, malezi mabovu na kwa sababu hiyo kutuathiri sisi sote kama taifa.

It's better that he has gone forever.
 
Huwa nikiangalia tamthilia za wazazi kubadilishiwa watoto WODINI Siku ya kujifungua nilikuwa naona kama igizo lisilo na uhalisia.

Baadhi ya watu nina hakika utotoni walibadilishwa wakiwa WODINI. Hongera Sana SASHA wewe ni Orijino!
 
Hili ni kweli na linazaa hoja nyingine: Kuna umuhimu mkubwa kabisa wa kubadilisha katiba, ili kama rais aliyepo madarakani atashindwa kuendelea na kazi, basi uitishwe uchaguzi mwingine mpya. Hii ni kwa sababu kama wananchi walimpa Magufuli kura kwa kuamini approach na misimamo yake ya kufanya kazi, basi sasa hivi tumepata mtu ambaye ni tofauti kabisa na anafanya mambo tofauti kabisa na mtangulizi wake.
Hivi kwa mfano nikitaka niyaone macho mdiliko nauli yake ni kiasi gani?
 
Hakika mkuu.. nimeliwaza sana hili!

Ni kama alikuwa pambo tu.. na kutumwa tumwa ng'ambo
 
Mpaka sasa hivi bado yupo njia panda kwa kuwa kivuli cha Kayafa kinamkaba koo kiendelee kutawala nchi.

Kuthibitisha hili ona anavyoyumba katika suala la kushughulikia Corona,ona anavyoshindwa kuwafutilia mbali wafuasi ovyo wa Kayafa,ona anavyoshindwa kuzuia Chato kuwa mkoa japo Chato haina sifa za kuwa mkoa,ona covid-19 wa Kayafa wanavyoendelea kutamba bungeni na Mama hana cha kuwafanya,ona anavyoshindwa kufutilia mbali masheria kandamizi ya Kayafa na kadhalika.

Kayafa is there for a while.


4jHF.jpg
 
Mpaka sasa hivi bado yupo njia panda kwa kuwa kivuli cha Kayafa kinamkaba koo kiendelee kutawala nchi.

Kuthibitisha hili ona anavyoyumba katika suala la kushughulikia Corona,ona anavyoshindwa kuwafutilia mbali wafuasi ovyo wa Kayafa,ona anavyoshindwa kuzuia Chato kuwa mkoa japo Chato haina sifa za kuwa mkoa,ona covid-19 wa Kayafa wanavyoendelea kutamba bungeni na Mama hana cha kuwafanya,ona anavyoshindwa kufutilia mbali masheria kandamizi ya Kayafa na kadhalika.

Hakika kivuli cha Kayafa bado kinaendelea kutawala Tanzania.Kayafa is there for a while.
View attachment 1805793
He he he.... He will eventually vanish when "Mama" goes.
 
Hili ni kweli na linazaa hoja nyingine: Kuna umuhimu mkubwa kabisa wa kubadilisha katiba, ili kama rais aliyepo madarakani atashindwa kuendelea na kazi, basi uitishwe uchaguzi mwingine mpya.

Hii ni kwa sababu kama wananchi walimpa Magufuli kura kwa kuamini approach na misimamo yake ya kufanya kazi, basi sasa hivi tumepata mtu ambaye ni tofauti kabisa na anafanya mambo tofauti kabisa na mtangulizi wake.
Wananchi gani waliomchagua jiwe?Jiwe alijiweka mwenyewe madarakani!
 
Bado tunaona nchi inajiendesha kwà mfumo wa mwendazake japokuwa Rais anajaribu kutusahaulisha.

Hatujaona mabadiliko yoyote aliyoyafanya Samia tofauti na teuzi.

Hatuwezi kusema kwamba Samia kafanya nini ikiwa Sheria ni zilezile hakuna badiliko la kijamii.

Kimsingi JPM alikuwa na maadui wake ambao Samia hawezi kurithi hivyo nchi imerelax.

Samia hawezi kuwa JPM japo ukweli ni kwamba wengi wanataka awe mkali kama JPM.

Mfano Jana kariakoo watu walifurahi Sana alipo watumbua wafanya Kazi.
 
Back
Top Bottom