Kwa mchanganuo huu Yanga mtakufa kwa madeni

xray

Member
Joined
Aug 11, 2013
Posts
26
Reaction score
44
Bajeti ya Yanga Vs TP Mazembe- Lubumbashi
Kwa haraka haraka nlikua najaribu kuitazama / kuitafakari bajeti ya Yanga kwenda Lubumbashi Jumapili tarehe 21 August, 2016 nikizingatia hali ya uchumi ya timu kwa sasa.
Tufanye tiketi ya ndege go and return/kwenda na kurudi ni Tshs
Wachezaji (25) * $ 800
Benchi la Ufundi (8) * $ 800
Kiongozi wa msafara Yanga (1) * $ 800
Mwakilishi wa TFF (1) *$ 800
Jumla ndogo $ 28,000
Hoteli watu 35 * $ 100 kwa usiku 3 = $10,500
Allowances/posho ya safari watu 35*100$ kwa siku 2 = $ 7,000
Bei ya kuweka Camp kwa ajili ya mazoezi = $ 600
Usafiri wa ndani Lugumbasi kwa siku 4 = $ 600
JUMLA $ 46,700 Makadilio ya chini kabisa, ambayo ni sawa na Tshs. 102,740,000

Hapa ndo utaelewa kwanini MO Dewji alisema kwamba Simba na Azam bajeti yao inaizidi Yanga kwa zaidi ya bilioni 1.

Kutokana na mkutano mkuu wa Yanga pale Diamond Jubilee Katibu Mkuu alisikika akisema Yanga ina deni la bilioni 1.5 kwa mwaka huu mmoja tu na kwamba imekuwa ikijiendesha kwa hasara inayosababisha deni lake kuongezeka kila mwaka.

Maana yake Yanga hana hela. Kama Yanga inajiendesha kwa hasara maana yake haikopesheki, maana ni benki gani inayoweza kumkopesha mtu asiye na uhakika wa kulipa deni.

Hata Dr. Charles Kimei alisema hilo Tarehe 17 Agosti 2016 wakati anapokea tuzo ya CRDB.

Sasa najiuliza, imekuaje Yanga amefulia lakini ameweza kwenda Lubumbashi ambapo anakadiliwa kutumia zaidi ya Milioni 100 kwa siku 3.

Ukifikiria vizuri ndio utaelewa kwanini watani wetu wanamlilia Manji.

SIMBA! Nguvu Moja.
 
Sasa ulitakaje,wasiende ili CAF iwafungie?
 
Assume ni Simba SC vs TP Mazembe...

Then piga hesabu ya makadirio ya ghalama katika nyanja kama za hapo juu.

Nia yangu nione tu kama ghalama itqpungua au itazidi.
 
Assume ni Simba SC vs TP Mazembe...

Then piga hesabu ya makadirio ya ghalama katika nyanja kama za hapo juu.

Nia yangu nione tu kama ghalama itqpungua au itazidi.

Kwani Manji kashajitoa?
 
Assume ni Simba SC vs TP Mazembe... Then piga hesabu ya makadirio ya ghalama katika nyanja kama za hapo juu. Nia yangu nione tu kama ghalama itqpungua au itazidi.
Tofauti ni kwamba Yanga wanakataa wadhamini (TBL na Azam TV) badala yake wanakopa hela kwa jamaa mmoja mjanja sana, wakati Simba inavuta mpunga huo na kubaki na relatively madeni machache
 
Assume ni Simba SC vs TP Mazembe...

Then piga hesabu ya makadirio ya ghalama katika nyanja kama za hapo juu.

Nia yangu nione tu kama ghalama itqpungua au itazidi.
Akipiga kwa Simba S.C ghalama lazima itakua kubwa.. Ila kwa Yanga S.C gharama ni ndogo..[emoji3] [emoji3] [emoji3] [just joking Mkuu]
 
Unajua Yanga anapokea shilingi ngapi baada ya mechi za makundi shirikisho kuisha?
 
We toka wamekuondoa udom unaharibikiwa day after day
 
Tofauti ni kwamba Yanga wanakataa wadhamini (TBL na Azam TV) badala yake wanakopa hela kwa jamaa mmoja mjanja sana, wakati Simba inavuta mpunga huo na kubaki na relatively madeni machache


Ni bora unyamaze kuliko kuongea usichokijua.

Ni Simba SC ipi inayovuta pesa kutoka TBL?

Unajua zile pesa za azam ambazo yanga hawajachukua ziko wapi?

Kama ukiweza jibu, kwa usahihi basi utakuwa umefikia viwango vya kuweza kubishana na mimi katika mjadala huu.
 
Akipiga kwa Simba S.C ghalama lazima itakua kubwa.. Ila kwa Yanga S.C gharama ni ndogo..[emoji3] [emoji3] [emoji3] [just joking Mkuu]


Kuna afadhali gani kati ya aliyekula nyama ya nguruwe na yule aliyekunywa mchuzi wa nguruwe ikiwa kwao ni Marufuku?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…