Kwa mechi ya jana misri vs Tanzania tujiandae na saikolojia

Kwa mechi ya jana misri vs Tanzania tujiandae na saikolojia

Nina maoni tofauti. Mimi binafsi siridhishwi na style na personality ya Amunike. Lakini hii haininyimi nafasi ya kuona ubora na uzuri wa kitu anachokifanya na timu inavyocheza.

Kwanza timu imecheza kwa mfumo mzuri unaoeleweka. Wamekaba vizuri hasa kuzuia krosi za Wamisri japo walifanikiwa kupiga krosi kadhaa na kupata goli kwa mojawapo ya krosi hizo. Wachezaji wote wamecheza vizuri na wameonyesha ushindani. Timu ina mwelekeo sahihi, lakini kocha akubali kubadilika kidogo, apokee ushauri ili timu ifanye vyema zaidi.

Kwanza, ni kweli huwezi kucheza na timu ya kiwango cha Misri halafu eti ukataka mgawane possession! Hatujafikia kiwango hiki, kwa hiyo approach ya mwalimu ni sahihi. Lakini tatizo ni nafasi anazowapanga wachezaji. Anapocheza John Bocco alipaswa kucheza Simon Msuva.

Msuva ana kasi na maamuzi ya haraka, anahitaji eneo kubwa kwenye mianya ili kuisumbua defence. Anaweza kujaribu kukaba kiasi fulani kwenye winger (tracking), lakini uwepo wake eneo la kulia ni dhahiri timu ya Misri ingerudi nyuma angalau upande ule.

John Bocco, ana kimo, na nguvu. Anaweza kusimama katikati ya mabeki wawili nao wakakosa raha hasa kwa mipira ya juu. Ni mzuri anapotokea katikati na kuivuta timu kulia. Timu ikipangwa hivi ule utulivu wa defence kupanga mashambulizi kama walivyofanya Wamisri usingekuwepo. Kumpanga Bocco kama winga wa kupanda na kushuka, ni matumizi mabaya ya rasilimali watu uwanjani.

Kuhusu defence, Amunike anataka timu ianze kucheza mpira nyuma. Bahati mbaya Aggrey Morris si mzuri katika hili. Mbaya zaidi kiungo wa chini Himid Mao si mzuri pia wa kutawala mpira na kuichezesha timu. Pressing ya Wamisri kwenye kiungo ilikuwa kubwa sana, na bahati mbaya timu yetu haigusi pasi mojamoja ya haraka, na ndio maana mipira ikawa inapotezwa kwa haraka. Hatuwezi pia kuificha mpira isipokuwa Samatta pekee ndio alikuwa akikaa na mpira unakuwa salama kiasi fulani.
Hapa ndio Erastho Nyoni anapohitajika kuwa kiungo wa ulinzi ambaye anakaba, na kuituliza timu. Tungeweza kuupata ubora wa Feisal Toto zaidi ya vile. Viungo wangekuwa wanapiga pasi ndefu pembeni kulia kama Msuva angekuwa anapitia kule.

Amunike ajaribu, machache tu, Bocco katikati, Msuva kulia na Nyoni kiungo, timu italeta kitu fulani kizuri zaidi ya sasa.
Salute mkuu.
Haya ndio maoni ya kiunamichezo.
 
Mripa haupo bila mashabiki.

Nianze na wewe mtoa mada umecheza 0/10 ya wajibu wako.

Sababu:
1. Natanguliza disclamer kwani sina CV yako, lakini kwanza ulipaswa kulinganisha vitu vinavyolingana, (Misri na Tz) na pia (wewe na Amunike!!!?) eti wewe unamkosoa Kocha kwa uelewa wa mpira upi unaoujua. Lakini si wewe tu bali wa Tz wengi wanajua mpira wa maneno. Tz kimpira tupo mbali (chini) sana na mpira wa leo ni wa kisayansi na mpira ni pesa na uzoefu. Sasa linganisha vyote hivyo vya misri na sisi wapi na wapi?
2. Ulipaswa kazi yako kubwa iwe kuwatia moyo vijana wetu na umeshindwa na kukosa fadhila. Tilia maanani kuwa kwa timu zetu hizi changa mpira kwa mchezaji ni kujitolea na kuna uwezekano akavunjika mguu na biashara ikawa imeishia hap hapo lakini bado wewe unawalaumu kama vile umewalipa.
3. Tusisahau malengo yetu mpaka sasa ni kuweza kufika finali hizi za African cup of Nations na Amunike kafanikiwa hata kama atapoteza mechi zoote zikiwemo za majaribio. Tugange ijayo ili tuvuke hatua kwa hatua. Nawaza tu wala sijaanza kukulaumu ili na mimi nisije nikacheza 0/100.
 
Anatengeneza CV kupitia Tz,wakati anatutia aibu watu zaidi ya 55million,jana nilikuwa naangalia mpira na jamaa yangu ambaye anatoka kule mpira una weledi nilipata aibu sana,nilijaribu kumshawishi tutoke pale baada ya 45 minutes,akasema tumalizie kwanza.

Aliniuliza yaani timu yenu hata pasi tatu haipigi,halafu kocha amekaa tu.Aliendelea,hii ni mechi ya kirafiki kujaribu wachezaji mbona Kocha wa Egypt anafanya mabadiriko mapema wenu haoni hilo jambo.

Kutengeneza mfumo kipindi cha mashindano ni ngumu kufanikiwa,eti boko na Chilunda winger midfielders

Tukipata points hata tatu Afcon itakuwa maajabu ya soka
 
Nina maoni tofauti. Mimi binafsi siridhishwi na style na personality ya Amunike. Lakini hii haininyimi nafasi ya kuona ubora na uzuri wa kitu anachokifanya na timu inavyocheza.

Kwanza timu imecheza kwa mfumo mzuri unaoeleweka. Wamekaba vizuri hasa kuzuia krosi za Wamisri japo walifanikiwa kupiga krosi kadhaa na kupata goli kwa mojawapo ya krosi hizo. Wachezaji wote wamecheza vizuri na wameonyesha ushindani. Timu ina mwelekeo sahihi, lakini kocha akubali kubadilika kidogo, apokee ushauri ili timu ifanye vyema zaidi.

Kwanza, ni kweli huwezi kucheza na timu ya kiwango cha Misri halafu eti ukataka mgawane possession! Hatujafikia kiwango hiki, kwa hiyo approach ya mwalimu ni sahihi. Lakini tatizo ni nafasi anazowapanga wachezaji. Anapocheza John Bocco alipaswa kucheza Simon Msuva.

Msuva ana kasi na maamuzi ya haraka, anahitaji eneo kubwa kwenye mianya ili kuisumbua defence. Anaweza kujaribu kukaba kiasi fulani kwenye winger (tracking), lakini uwepo wake eneo la kulia ni dhahiri timu ya Misri ingerudi nyuma angalau upande ule.

John Bocco, ana kimo, na nguvu. Anaweza kusimama katikati ya mabeki wawili nao wakakosa raha hasa kwa mipira ya juu. Ni mzuri anapotokea katikati na kuivuta timu kulia. Timu ikipangwa hivi ule utulivu wa defence kupanga mashambulizi kama walivyofanya Wamisri usingekuwepo. Kumpanga Bocco kama winga wa kupanda na kushuka, ni matumizi mabaya ya rasilimali watu uwanjani.

Kuhusu defence, Amunike anataka timu ianze kucheza mpira nyuma. Bahati mbaya Aggrey Morris si mzuri katika hili. Mbaya zaidi kiungo wa chini Himid Mao si mzuri pia wa kutawala mpira na kuichezesha timu. Pressing ya Wamisri kwenye kiungo ilikuwa kubwa sana, na bahati mbaya timu yetu haigusi pasi mojamoja ya haraka, na ndio maana mipira ikawa inapotezwa kwa haraka. Hatuwezi pia kuificha mpira isipokuwa Samatta pekee ndio alikuwa akikaa na mpira unakuwa salama kiasi fulani.
Hapa ndio Erastho Nyoni anapohitajika kuwa kiungo wa ulinzi ambaye anakaba, na kuituliza timu. Tungeweza kuupata ubora wa Feisal Toto zaidi ya vile. Viungo wangekuwa wanapiga pasi ndefu pembeni kulia kama Msuva angekuwa anapitia kule.

Amunike ajaribu, machache tu, Bocco katikati, Msuva kulia na Nyoni kiungo, timu italeta kitu fulani kizuri zaidi ya sasa.
Well said bro!
 
K
Kama Stars imefungwa 1-0 pongezi kubwaaaaa kwa amunike . Ametufikisha mbali sana. Misri ndiyo bingwa mtarajiwa wa mashindano haya , kumbuka mwaka jana walikuwa kombe la dunia.zamani tulikuwa tukifungwa 5-0 na misri. Kufungwa moja tu tumefanya kazi ya ziada kama vile tumeshinda. Vile vile vijana walikuwa hawajapiga kambi muda mrefu ili kuelewana . Amunike ongezewe mkataba wa miaka 5. Kubadilish wachezaji na position ilikuwa nia ya Kocha ili aone kama kuna badiliko.
Kenya tunawafunga, Senegal tunawafunga au droo . Algeria watatupa shida kidogo . Aina ya uchezaji wa Algeria na misri ni Sawa Mpira wa kazi .
Yote kwa yote sijaona Dalali mbaya bado.
Tatizo la Tanzania kila mtu ni mtaalamu wa mpira.
Kuna mtu yoyote hapa jukwaa la Michezo au Tanzania Anajua Mpira kuliko amunike?
Amunike amechukua kombe la afrika Enzo hizo kuna kina roger Mila , yeboah, abedi pele , hossam Hassan , kalusha nk
Amecheza kombe la dunia na maradona Nigeria ikaisumbua Argentina ya maradona sio Argentina ya messi na di maria
Kaka u-simba na U-Yanga vinasumbua sana vichwa vyetu. Kiujumla Jana timu ilicheza vizuri sana, mie nimeangalia mpira mwanza mwsho, Timu inacheza kwa pattern tofaout na wapondaji wanaosema eti butua butua. Acha hixo bwana, hata wamisiri kupata kigoli ilikuwa ni Nazi kwelikweli. Tupunguze ubinafsi ndg zangu na tuache kocha achague timu yake. Hao kina mkude unaowasifia ndiyo wanapigwaga mikono kila Mara (Ref. Algeria Vs Tz ) 7-0
 
watu mpira hamjui mnajifanya kujua,unaweza kushindana na misri kumiliki mpira kwa wachezaji wa kutoka hananasif,ambao njia za mpira wameenda kujifunza simba na yanga wakiwa tayari wameanza kunyoa ndevu!?
 
Erasto Nyoni pale nyuma hasa akitulia namba 6, ana mchango mkubwa sana. Viungo hawakuchangamka kabisa. Fei Toto si mchangamfu na hilo linafahamika. Himid Mao, nguvu nyingi bila sababu.

Pasi nyingi za timu yetu hazikuwa na macho kutokana na kukosa kujiamini. Nadhani Mudathir Yahya ndiye tegemeo pekee pale kati. Timu ilijilinda kwa dk zote 90 hivyo kufungwa kulikua hakuepukiki.
 
Amunike HAFAI na anatupotezea Muda tu.
Baada ya kuona Misri wametutawala kwenye kiungo, kulikuwa na haja gani ya kumuingiza Ulimwengu? Pale ilitakiwa wabaki washambuliaji wawili tu mbele: Samata na Msuva halafu angeimalisha kiungo kwa kuweka wakabaji na watoa pasi za mwisho kama Mudathir na Domayo. Vilevile angalau angemweka Erasto namba 6 ili atulize timu.
Badala yake anachezesha beki wawili wa kushoto kwa mpigo: Tshabalala na Gadiel!! Huu mfumo wa wapi??????
Timu inabutua tu, hakuna structure au pattern inayoeleweka, yaani tunavyocheza hata dunia itatushangaa tuliingiaje Afcon!
TFF TUONDOLEENI HUYO BOYA AMUNIKE BAADA YA AFCON, ANATUHARIBIA TIMU TU.
Una lessen ya ukocha lakin? We unafikiri rahis hivyo eti...
 
Achei ujuaji... hivi misri vs stars unataka maajabu gani?

Ila yule sijui anaitwa Warda wa misri ni hatari sana
 
kw mfumo wa Amunike M<chezaji pekee anayeweza kuonwa na mawakala atakuwa Aishi Manula kina Samatta hawawezi kuoneka sanasana atabebwa na sifa za Genk kwa viungo walishindwa kabisa kuicheza timu na kuchezesha washambulia, rafu za kijinga, kujilinda kama tuko ugenini tunatafuta pointi ya ugenini,
Kocha anatakiwa abadilike Msuva anatakiwa atokee pembeni sio kumweka katikati pamoja naa kujilinda hana plan hata za kufanya counter attack
 
nilisubiri nimwone yule mshambuliaji anayeongoza kwa magoli Uingereza lakini bado hata mabadiliko yaliyofanywa ni kuongeza ulinzi
 
Nilijiuliza sana kwa nini tulizidiwa pasi kiasikile, baada ya kusoma maoni ya wadau hapa nimeona kuwa Amunike ana sababu, hakutaka kuiweka timu mezani mwa adui zake, ile ni janja, kama Senegal kawaza kuwa ule ndo uwezo wetu amekwisha, Amunike ataipanga timu vzuri siku ya mashindano, tusubiri, mmeona mbali lakini Amunike kaona mbali zaidi, lakini pia nafkiri alitaka kujaribu mfumo wa kuzuia pale tunapozidiwa, kwa jana alifanikiwa ingawa sifa zimwendee kipa Aishi Manula, tuwe na subira wadau
 
Nilijiuliza sana kwa nini tulizidiwa pasi kiasikile, baada ya kusoma maoni ya wadau hapa nimeona kuwa Amunike ana sababu, hakutaka kuiweka timu mezani mwa adui zake, ile ni janja, kama Senegal kawaza kuwa ule ndo uwezo wetu amekwisha, Amunike ataipanga timu vzuri siku ya mashindano, tusubiri, mmeona mbali lakini Amunike kaona mbali zaidi, lakini pia nafkiri alitaka kujaribu mfumo wa kuzuia pale tunapozidiwa, kwa jana alifanikiwa ingawa sifa zimwendee kipa Aishi Manula, tuwe na subira wadau
mkuu umemaliza..kuna watu manyumbu sana...mtu hata kubetua mpira hawez ila anamponda amunike...nafkiri mwalimu alijaribu kufcha mbinu kwa wapinzani..na stratergy aliyotumia ya ku defence ni nzuri kwakua misri ni hatari..tunaweza tusifike mbali ila angalau tumetoa gundu
 
Tusibadili utaratibu....tutapata taabu sana...na tutajuta kwa nini tulienda huko
 
Back
Top Bottom