Kwa miaka 18 sijawahi kushudia ugumu wa biashara kama awamu hii ya Tano

Kwa miaka 18 sijawahi kushudia ugumu wa biashara kama awamu hii ya Tano

Mkuu bora wewe bado unakomaa na biashara.. Wenzako tulishafunga muda mrefu, wanunuzi wako hoi na hawana pesa hizo bidhaa utamuuzia nani??

Kabla ya huyu jamaa nilikuwa nakuja dar kufunga mzigo kila mwezi, lakini alivyoanza sarakasi zake tu kila kitu kilikwenda kombo!!
 
Bandiko la maana sana hili na naunga mkono hoja,mtaani hali ni mbaya sana tunadumu kwa sababu ya uzoefu na kudra za Mungu tu kwamba biashara ametupa ndiyo vipawa vyetu tunavitumikia.

Ila mkuu believe me,utawala huu mfanyabiashara utakayefanikiwa ku-survive ukaenda na mchezo unavyotaka huko mbele hakuna kitakachokusumbua.tusisahau mfanyabiashara daily unajifunza kutokana na changamoto zilizo mbele yako na kadiri unavyozivuka ndivyo unavyozidi kujijengea mizizi.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Kwa mtu ambaye hajawahi fanya biashara atakejeli ulichosema, ila kiuhalisia hali siyo kabisa. Kunasehemu ya biashara mahitaji ya nyumbani kipindi cha nyuma ilikuwa afadhali ila sasa kila anayepita anasema na kile nahitaji ila ngoja nitafute hela means uwezo wa kununua umepungua sana. Kusipokuwa na sababu na nia ya dhati ya kunusuru uchumi tutakwama.
 
Nina miaka 18 kwenye biashara katika kipindi chote hicho,Nimepitia milima na mabonde.” Yani changamoto” Kitu ambacho ni cha kawaida kwenye biashara yoyote.

Lakini leo nakiri kwamba, Awamu hii imeuwa juhudi za watu wengi kufikia malengo yao kibiashara, Biashara zimeyumba kabisa, Mauzo yameshuka kwa asilimia zaidi ya 70, huku mitaji mingi ya wajasiria mali ikiteketea.

Kinachoogopesha zaidi, Sioni juhudi zozote za makusudi kuokoa hali hii mbaya. Jamaa zangu wengi wameshindwa kulipia school fees,Wengine wameshindwa kulipia mapango ya frem,Wengine ndoa zao zimevunjika na wengine wamepata stroku.
Lakini tukiwasikiliza viongozi wetu wanasema tupo pazuri. Najiuliza pazuri wapi?

Mwanzoni nilijua labda baba anafanyia nyumba usafi, Cha kushangaza tunamaliza miaka tano hali imekuwa tete zaidi ya tulipo toka.

Kuna hitajika jitihada za ziada kwenye uchumi wetu tena kwa speed kubwa la sivyo tutazalisha taifa la wamachinga na wapiga vibomu. Maana soon kodi za pango na serekali hazitalupika tena.

Natamani hii biashara yangu nimpe bure Dr mpango aiendeshe kwa miezi tu ili ajue hali halisi sio kukaa ofisini huku tukimlipa mshahara mnono bila kusaidia uchumi wetu.

Dr. Mpango mweleze rais hali mtaani ni mbaya,Watu tunapiga kazi asubuhi mpaka jioni lakini tunatoka kapa kila siku.

Halafu nimegundua ukiwa na hali mbaya mfukoni na majukumu ndio yanabisha hodi kwa kasi kweli kweli.

Hivi ilani ya chama ndio ilinadiwa kutekeleza hali iwe ngumu hivi? Tukutane mwakani october tuelezane kwa vitendo.

Niko golini hapa toka saa mbili kamili asubuh mpaka sasa hv nna buku 7 tu dadeki utadhan mtoto wa lumumba.
 
Hivi ilani ya chama ndio ilinadiwa kutekeleza hali iwe ngumu hivi? Tukutane mwakani october tuelezane kwa vitendo.
ukizoea kunyonga,kuchinja huwezi
Sasa ni kulipa kodi tu,kwa kua ulizoea kulipalaki tano kwa mwaka,lazima hali uone ngumu
 
Kitu nimegundua jf ina watu wengi wanakula ugali wa shikamoo mama, shikamoo baba wakishiba na wakaomba buk la bando wanaropoka tu, kimsingi hawajijui haya yote yaliyoandikwa na mtoa uzi yanalogic kwa mtu anayejitambua

Sent using Jamii Forums mobile app
Humu unataja unafanya biashara wakati watu wako frustrated na hiyo biashara mtu hajui hata ikoje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kitu nimegundua jf ina watu wengi wanakula ugali wa shikamoo mama, shikamoo baba wakishiba na wakaomba buk la bando wanaropoka tu, kimsingi hawajijui haya yote yaliyoandikwa na mtoa uzi yanalogic kwa mtu anayejitambua

Sent using Jamii Forums mobile app
Humu unataja unafanya biashara wakati watu wako frustrated na hiyo biashara mtu hajui hata ikoje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunalalamika sisi ila kuna watu hata hawaelewi ukisema hiki kitu..Juzi kuna wateja wamekuja Kazini kwangu Madili ya hela waliyokua wanapiga Tena ni ya Halali kabisa wala sio wezi wala mafisadi Si ya kawaida watu wanapiga hela bwana..Nikasema Awamu hiii ina biashara na biashara na Mitaji na Mitaji.
 
Back
Top Bottom