Kwa miaka 20 tunashiriki uchaguzi, CHADEMA hatujakubalika, yaliyotokea Zambia hayawezi kutokea hapa Tanzania

CCM ni genge linalotumia mabavu ya vyombo vya dola kuendelea kutawala. Nyie CCM hamkubaliki kabisa
 
OK. Poa tu. Hata Magufuli mlisema atatawala miaka 30!
 
Nakubaliana na wewe Sasa ushauri wangu

1. Leteni tume huru ya uchaguzi
2.;Msitumie dola kabisa
3. Katiba mpya

Haya yakipatikana na chadema isipochukua nchi nitaamini cdm hakipendwi kabiiiisaaaaaaà
 
Yanaweza kutokea usivunje watu moyo,
Imani haijengwi kwa siku moja, ccm Ina zaidi ya 40yr ukiweka na tanu ni 60, lakini bado kuna dalili imani kwa wananchi kushuka
 
Kama viongozi Hawa c madhubuti kwanini mliwapiga risasi 16
 
Vyana tawala Zambia Mungu avilinde kwa kutokuwa wadhalimu kwenye uchaguzi kama ilivyo CCM hapa kwetu.
 
Shida kubwaa kwenye vyama pinzani ni ubinafs na njaa za viongozi. Ubinafsi inakuwa karibu kila kiongozi anataka asimame yeye kama mgombea wa Uraisi ni wagumu sana kukubaliana mmoja asimame kwa niaba ya wote, Na njaa ni kwa viongozi ambao wako kimaslahi kwamaneno mengine wananunulika!
 
Acha kuropoka.
CCM Inapita kwa kutumia polisi na tume mbovu ya uchaguzi.
Bila hivyo,CCM kingekuwa historian jinsi watu wa jawaida walivyo kichoka chama hiki.
CCM si chama cha siasa tena bali ni jeshi linalojiita chama cha siasa. Tanzania tunatawaliwa kimabavu na jeshi hili.
 
Wewe nawe umeshakuwa kama vile una ubongo wa maji, kusema kweli huna akili. Ngoja niishie hapo maana una propaganda zisizo na kichwa wala miguu
 
Machadema yanajifariji kwa kuangalia kinachotokea Zambia yanasahau kwamba hizi nchi zina historia mbili tofauti.

Kana kwamba haitoshi Kenya,Zambia,Ghana na Malawi vyama kubadilishana uongozi ni kawaida haijaanza kwa Hichilema.

Hapa Tzn ni nchi yenye siasa kama China ila upinzani uko kuzugiwa tuu,ccm ni chama dola na hakuna kitu kutoka nje kitabadili hilo.
 
Mlisema Magufuli wenu atatawala miaka 30 huku mkimiminia Tundu Lissu risasi, akafa Magufuli.
Sasa mnawasema Chadema eti miaka 20 hawajakubalika - nyie mtakufa halafu Chadema watakubalika hatimaye!
Ndoto za mchana zinasaidia mtu awe na matumaini ya kuishi.
 
Mlisema Magufuli wenu atatawala miaka 30 huku mkimiminia Tundu Lissu risasi, akafa Magufuli.
Sasa mnawasema Chadema eti miaka 20 hawajakubalika - nyie mtakufa halafu Chadema watakubalika hatimaye!
Sawa, mtasubiri sisi watanzania wote tufe ndiyo Chadema itawale!.
 
UKweli ni kwamba mifumo ya kiusalama na vyombo vya dola havijawakubali wapinzani...na kwa katiba hovyo,tume ya uchaguzi hovyo iliyo na makada wa Ccm..wapinzani wasahau,wanachotakiwa kufanya wafanye yale yaliyowakuta USSR
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…